28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

haliepukiki ikizingatiwa kwamba Shirika lina jukumu zito la kuwahudumia Watanzania wengi zaidi.<br />

Hata hivyo, napenda kuwahakikishia kwamba viwan<strong>go</strong> vya kodi vitaendelea kuwa chini ya<br />

viwan<strong>go</strong> vya soko. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Shirika lilijipanga kutekeleza miradi mikubwa<br />

kwa kuongeza akiba yake ya ardhi kwa ekari 7,967 katika miji ya Dodoma, Musoma, Arusha na<br />

Moro<strong>go</strong>ro. Vilevile Shirika lilifanya maandalizi ya ujenzi wa nyumba za makazi na biashara zipatazo<br />

4,000 katika Wilaya mbalimbali nchini. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Shirika liliendelea na ujenzi wa nyumba za makazi<br />

Arusha (nyumba 52) na Dar es Salaam (34), pamoja na jen<strong>go</strong> la biashara mjini Ki<strong>go</strong>ma. Kadhalika<br />

Shirika liliendelea na utekelezaji wa miradi ya ubia 75 yenye thamani ya shilingi bilioni 300 kwa<br />

kushirikiana na sekta binafsi. Mchan<strong>go</strong> mkubwa wa Shirika katika miradi hiyo ni ardhi.<br />

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Shirika lilikusanya shilingi bilioni 41.9 ambayo ni<br />

sawa na asilimia 108 ya len<strong>go</strong> la mwaka huo. Ongezeko la makusanyo lilitokana na juhudi kubwa<br />

zilizofanyika za kukusanya malimbikizo ya kodi kwa mujibu wa Sheria ya Shirika la Nyumba la Taifa<br />

Na. 2 ya 1990 na Sheria ya Ardhi Na. 4 ya 1999 ambazo zinalipa Shirika uwezo wa kufanya shughuli<br />

zake kwa misingi ya biashara. Kwa mwaka 2011/2012 Shirika limeweka len<strong>go</strong> la kukusanya shilingi<br />

bilioni 43.1 kwa kuendelea kutekeleza mikakati ya kukusanya malimbikizo ya madeni na mapato<br />

yanayotokana na kodi za pan<strong>go</strong>. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Shirika liliendelea kutekeleza mkakati wa<br />

kutenga asilimia 20 ya Bajeti kwa ajili ya kuyafanyia matengenezo majen<strong>go</strong> yake 2,392. Katika<br />

kipindi husika Shirika lilitumia shilingi bilioni 5.06 kwa ajili hiyo. Kwa mwaka 2011/2012 Shirika<br />

limetenga shilingi bilioni 6.8 kwa ajili ya matengenezo ya majen<strong>go</strong> yake. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Shirika lilianza mazungumzo na benki 10 kwa<br />

len<strong>go</strong> la kupata mikopo ya ujenzi wa nyumba na kuwapatia wanunuzi mikopo ya nyumba. Ni<br />

matarajio ya Wizara kuwa wananchi wataweza kupata mikopo kutoka kwenye benki hizo kwa ajili<br />

ya ununuzi wa nyumba zitakazojengwa na Shirika. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2011/2012 Shirika linatarajia kuanza ujenzi wa nyumba za<br />

makazi 2,721 na majen<strong>go</strong> saba ya biashara katika Mikoa ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, Tabora,<br />

Mbeya na Moro<strong>go</strong>ro. Miradi hii itagharimu shilingi bilioni 311.5 na Shirika litatumia shilingi bilioni<br />

164.1 kwa mwaka 2011/2012. Vilevile Shirika litaanza ujenzi wa nyumba nyingine 160 za makazi<br />

katika baadhi ya miji mikuu ya Mikoa na Wilaya mpya. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu huduma za kisheria, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa<br />

Wizara yangu imefanikiwa kuwapata watumishi waandamizi wa kuendesha shughuli za Kiten<strong>go</strong><br />

cha Huduma za Kisheria (Legal Services Unit) za kutoa ushauri wa kisheria kwa Wizara na Taasisi<br />

zake, kushiriki katika majadiliano kati ya Wizara na wadau mbalimbali wa sekta ya ardhi na<br />

kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kufuatilia mashauri yanayoihusu Wizara<br />

Mahakamani. Natoa shukrani kwa msaada na ushirikiano uliotolewa na Mwanasheria Mkuu wa<br />

Serikali katika kuiwezesha Wizara kuanzisha kiten<strong>go</strong> hiki.<br />

Mheshimiwa Spika, suala la mawasiliano Serikalini, Wizara yangu iliendelea kuimarisha<br />

Kiten<strong>go</strong> cha Mawasiliano Serikalini ambacho kina jukumu la kuwasiliana na wananchi na wadau<br />

na kuwapa habari kuhusu shughuli za Wizara. Katika mwaka 2010/2011 elimu kwa umma juu ya<br />

huduma mbalimbali zinazotolewa na Wizara pamoja na sera, mikakati na sheria za sekta ya ardhi<br />

ilitolewa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari na mikutano ya wadau. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu itaendelea kuimarisha Kiten<strong>go</strong><br />

hiki kwa kuajiri wataalam wa mawasiliano ya umma na kuongeza vitendea kazi. Wizara itaboresha<br />

mkakati wake wa mawasiliano na kuzindua mkataba wa huduma kwa mteja. Mabadiliko ya<br />

mkakati yatalenga kujumuisha ipasavyo mipan<strong>go</strong> muhimu inayotekelezwa na Wizara, ikiwa ni<br />

pamoja na mpan<strong>go</strong> wa uendelezaji wa Mji Mpya wa Kigamboni na wa kuzuia uvamizi wa<br />

maeneo ya wazi mijini. Elimu kwa umma itatolewa kupitia vyombo vya habari na majukwaa<br />

34

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!