Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
haliepukiki ikizingatiwa kwamba Shirika lina jukumu zito la kuwahudumia Watanzania wengi zaidi.<br />
Hata hivyo, napenda kuwahakikishia kwamba viwan<strong>go</strong> vya kodi vitaendelea kuwa chini ya<br />
viwan<strong>go</strong> vya soko. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Shirika lilijipanga kutekeleza miradi mikubwa<br />
kwa kuongeza akiba yake ya ardhi kwa ekari 7,967 katika miji ya Dodoma, Musoma, Arusha na<br />
Moro<strong>go</strong>ro. Vilevile Shirika lilifanya maandalizi ya ujenzi wa nyumba za makazi na biashara zipatazo<br />
4,000 katika Wilaya mbalimbali nchini. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Shirika liliendelea na ujenzi wa nyumba za makazi<br />
Arusha (nyumba 52) na Dar es Salaam (34), pamoja na jen<strong>go</strong> la biashara mjini Ki<strong>go</strong>ma. Kadhalika<br />
Shirika liliendelea na utekelezaji wa miradi ya ubia 75 yenye thamani ya shilingi bilioni 300 kwa<br />
kushirikiana na sekta binafsi. Mchan<strong>go</strong> mkubwa wa Shirika katika miradi hiyo ni ardhi.<br />
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Shirika lilikusanya shilingi bilioni 41.9 ambayo ni<br />
sawa na asilimia 108 ya len<strong>go</strong> la mwaka huo. Ongezeko la makusanyo lilitokana na juhudi kubwa<br />
zilizofanyika za kukusanya malimbikizo ya kodi kwa mujibu wa Sheria ya Shirika la Nyumba la Taifa<br />
Na. 2 ya 1990 na Sheria ya Ardhi Na. 4 ya 1999 ambazo zinalipa Shirika uwezo wa kufanya shughuli<br />
zake kwa misingi ya biashara. Kwa mwaka 2011/2012 Shirika limeweka len<strong>go</strong> la kukusanya shilingi<br />
bilioni 43.1 kwa kuendelea kutekeleza mikakati ya kukusanya malimbikizo ya madeni na mapato<br />
yanayotokana na kodi za pan<strong>go</strong>. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Shirika liliendelea kutekeleza mkakati wa<br />
kutenga asilimia 20 ya Bajeti kwa ajili ya kuyafanyia matengenezo majen<strong>go</strong> yake 2,392. Katika<br />
kipindi husika Shirika lilitumia shilingi bilioni 5.06 kwa ajili hiyo. Kwa mwaka 2011/2012 Shirika<br />
limetenga shilingi bilioni 6.8 kwa ajili ya matengenezo ya majen<strong>go</strong> yake. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Shirika lilianza mazungumzo na benki 10 kwa<br />
len<strong>go</strong> la kupata mikopo ya ujenzi wa nyumba na kuwapatia wanunuzi mikopo ya nyumba. Ni<br />
matarajio ya Wizara kuwa wananchi wataweza kupata mikopo kutoka kwenye benki hizo kwa ajili<br />
ya ununuzi wa nyumba zitakazojengwa na Shirika. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2011/2012 Shirika linatarajia kuanza ujenzi wa nyumba za<br />
makazi 2,721 na majen<strong>go</strong> saba ya biashara katika Mikoa ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, Tabora,<br />
Mbeya na Moro<strong>go</strong>ro. Miradi hii itagharimu shilingi bilioni 311.5 na Shirika litatumia shilingi bilioni<br />
164.1 kwa mwaka 2011/2012. Vilevile Shirika litaanza ujenzi wa nyumba nyingine 160 za makazi<br />
katika baadhi ya miji mikuu ya Mikoa na Wilaya mpya. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kuhusu huduma za kisheria, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa<br />
Wizara yangu imefanikiwa kuwapata watumishi waandamizi wa kuendesha shughuli za Kiten<strong>go</strong><br />
cha Huduma za Kisheria (Legal Services Unit) za kutoa ushauri wa kisheria kwa Wizara na Taasisi<br />
zake, kushiriki katika majadiliano kati ya Wizara na wadau mbalimbali wa sekta ya ardhi na<br />
kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kufuatilia mashauri yanayoihusu Wizara<br />
Mahakamani. Natoa shukrani kwa msaada na ushirikiano uliotolewa na Mwanasheria Mkuu wa<br />
Serikali katika kuiwezesha Wizara kuanzisha kiten<strong>go</strong> hiki.<br />
Mheshimiwa Spika, suala la mawasiliano Serikalini, Wizara yangu iliendelea kuimarisha<br />
Kiten<strong>go</strong> cha Mawasiliano Serikalini ambacho kina jukumu la kuwasiliana na wananchi na wadau<br />
na kuwapa habari kuhusu shughuli za Wizara. Katika mwaka 2010/2011 elimu kwa umma juu ya<br />
huduma mbalimbali zinazotolewa na Wizara pamoja na sera, mikakati na sheria za sekta ya ardhi<br />
ilitolewa kwa wananchi kupitia vyombo vya habari na mikutano ya wadau. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu itaendelea kuimarisha Kiten<strong>go</strong><br />
hiki kwa kuajiri wataalam wa mawasiliano ya umma na kuongeza vitendea kazi. Wizara itaboresha<br />
mkakati wake wa mawasiliano na kuzindua mkataba wa huduma kwa mteja. Mabadiliko ya<br />
mkakati yatalenga kujumuisha ipasavyo mipan<strong>go</strong> muhimu inayotekelezwa na Wizara, ikiwa ni<br />
pamoja na mpan<strong>go</strong> wa uendelezaji wa Mji Mpya wa Kigamboni na wa kuzuia uvamizi wa<br />
maeneo ya wazi mijini. Elimu kwa umma itatolewa kupitia vyombo vya habari na majukwaa<br />
34