Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Mheshimiwa Spika, natumia fursa hii kuiagiza Bodi ya Korosho, wanunuzi wa korosho na<br />
wakulima kuhakikisha kwamba mjengeko wa bei (price structure) katika biashara ya korosho<br />
unajadiliwa kwa uwazi katika vikao vya wadau wa korosho ili kuondoa manung’uniko. Aidha,<br />
tarehe 20 A<strong>go</strong>sti, 2011, kikao cha wadau wa korosho kitafanyika hapa Dodoma ambapo pamoja<br />
na mambo mengine, masuala yanayohusu gharama zinazohusiana na mfumo wa stakabadhi<br />
ghalani yanaweza pia kupewa ufafanuzi. Nawashauri Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> wote ambao ni<br />
wadau wa korosho kuhudhuria kikao hicho muhimu.<br />
MHE. CLARA D. MWATUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza<br />
swali la nyongeza. Kwa kuwa, ni kawaida kila mara Serikali inaweza kusema mazuri wakati ule<br />
wanapotaka suala lifanyike, lakini baada ya hapo, matokeo yake yanakuwa ni kinyume na<br />
makubaliano yale yaliyotolewa.<br />
Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutuhakikishia kwamba yale yanayosemwa ndiyo<br />
yatakayotekelezwa au yanatekelezwa (Makofi)<br />
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA (k.n.y WAZIRI WA KILIMO,<br />
CHAKULA NA USHIRIKA): Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> kwamba Serikali<br />
iko makini na inachosema ndicho inachotekeleza. Namwomba tu Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> tarehe 20<br />
A<strong>go</strong>sti, 2011 ahudhurie kikao hiki cha wadau na aweze kutoa madukuduku yake na yatajadiliwa<br />
na kukubaliwa na watu wote katika kikao hicho.<br />
MHE. HAMAD RASHID MOHAMED: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Sababu moja ya<br />
wakulima wetu katika kipindi chote cha miaka 50 ya kuendelea kuwa maskini ni kwa sababu<br />
bado hatujawa na viwanda vya kutosha vya kuweza kuongeza thamani ya mazao tunayozalisha.<br />
Kwa mfano, bado tunasafirisha asilimia tano tu ya pamba ambayo imekuwa processed, Korosho<br />
kwa asilimia 30 tu, karafuu kwa asilimia 15 tu na kadhalika.<br />
Je, Serikali ina utaratibu na mpan<strong>go</strong> gani wa kuhakikisha angalau hili zao moja la korosho<br />
ambalo tayari lina viwanda ambavyo kama vikisaidiwa tunaweza tukasafirisha zaidi ya asilimia 70<br />
ya korosho iliyosafishwa ili wakulima wetu waondokane na umasikini (Makofi)<br />
NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA (k.n.y WAZIRI WA KILIMO,<br />
CHAKULA NA USHIRIKA): Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> anatambua na aliona hivi<br />
karibuni Serikali imeleta mpan<strong>go</strong> wake wa miaka mitano hapa Bungeni, na katika mambo muhimu<br />
yaliyowekewa kipaumbele ni kuhakikisha kwamba tunaendeleza viwanda na kuhakikisha<br />
kwamba tunakuwa na viwanda ambavyo vitaongeza thamani ya mazao yetu ili tuweze kupata<br />
bei nzuri zaidi katika Soko la Dunia. Kwa hiyo, nimhakikishie tu Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> kwamba,<br />
Serikali itaendelea na mpan<strong>go</strong> wake huu wa miaka mitano na itatoa kipaumbele katika maeneo<br />
ambayo vilevile Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> ameyataja.<br />
MHE. MESHACK J. OPULUKWA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Sambamba na<br />
zao la korosho, napenda kumwuliza Mheshimiwa Waziri swali do<strong>go</strong> la nyongeza. Ni lini sasa Serikali<br />
itaacha kuweka zuio kwa wakulima wa Mikoa ya Shinyanga hususan Wilaya ya Meatu la kuwazuia<br />
kuchanganya pamba pamoja na mahindi<br />
Mheshimiwa Spika, ahsante.<br />
SPIKA: Mheshimiwa M<strong>bunge</strong>, nasikitika sana sio swali lenyewe. Nasikitika sana! Mheshimiwa<br />
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Mahusiano na Uratibu) unataka kujibu, lakini swali siyo lenyewe<br />
kabisa!<br />
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU): Mheshimiwa Spika, pamoja na<br />
kwamba swali lililoulizwa ni tofauti na swali la msingi, lakini kwa manufaa ya wakulima wa pamba<br />
katika Mkoa wa Shinyanga ambao wamekuwa wakichanganya pamba na mahindi, ningependa<br />
kusema kwamba kiutaalam na kwa mujibu wa matokeo ya utafiti, mazao ya mahindi kwa<br />
7