28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mheshimiwa Spika, natumia fursa hii kuiagiza Bodi ya Korosho, wanunuzi wa korosho na<br />

wakulima kuhakikisha kwamba mjengeko wa bei (price structure) katika biashara ya korosho<br />

unajadiliwa kwa uwazi katika vikao vya wadau wa korosho ili kuondoa manung’uniko. Aidha,<br />

tarehe 20 A<strong>go</strong>sti, 2011, kikao cha wadau wa korosho kitafanyika hapa Dodoma ambapo pamoja<br />

na mambo mengine, masuala yanayohusu gharama zinazohusiana na mfumo wa stakabadhi<br />

ghalani yanaweza pia kupewa ufafanuzi. Nawashauri Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> wote ambao ni<br />

wadau wa korosho kuhudhuria kikao hicho muhimu.<br />

MHE. CLARA D. MWATUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza<br />

swali la nyongeza. Kwa kuwa, ni kawaida kila mara Serikali inaweza kusema mazuri wakati ule<br />

wanapotaka suala lifanyike, lakini baada ya hapo, matokeo yake yanakuwa ni kinyume na<br />

makubaliano yale yaliyotolewa.<br />

Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutuhakikishia kwamba yale yanayosemwa ndiyo<br />

yatakayotekelezwa au yanatekelezwa (Makofi)<br />

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA (k.n.y WAZIRI WA KILIMO,<br />

CHAKULA NA USHIRIKA): Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> kwamba Serikali<br />

iko makini na inachosema ndicho inachotekeleza. Namwomba tu Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> tarehe 20<br />

A<strong>go</strong>sti, 2011 ahudhurie kikao hiki cha wadau na aweze kutoa madukuduku yake na yatajadiliwa<br />

na kukubaliwa na watu wote katika kikao hicho.<br />

MHE. HAMAD RASHID MOHAMED: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Sababu moja ya<br />

wakulima wetu katika kipindi chote cha miaka 50 ya kuendelea kuwa maskini ni kwa sababu<br />

bado hatujawa na viwanda vya kutosha vya kuweza kuongeza thamani ya mazao tunayozalisha.<br />

Kwa mfano, bado tunasafirisha asilimia tano tu ya pamba ambayo imekuwa processed, Korosho<br />

kwa asilimia 30 tu, karafuu kwa asilimia 15 tu na kadhalika.<br />

Je, Serikali ina utaratibu na mpan<strong>go</strong> gani wa kuhakikisha angalau hili zao moja la korosho<br />

ambalo tayari lina viwanda ambavyo kama vikisaidiwa tunaweza tukasafirisha zaidi ya asilimia 70<br />

ya korosho iliyosafishwa ili wakulima wetu waondokane na umasikini (Makofi)<br />

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA (k.n.y WAZIRI WA KILIMO,<br />

CHAKULA NA USHIRIKA): Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> anatambua na aliona hivi<br />

karibuni Serikali imeleta mpan<strong>go</strong> wake wa miaka mitano hapa Bungeni, na katika mambo muhimu<br />

yaliyowekewa kipaumbele ni kuhakikisha kwamba tunaendeleza viwanda na kuhakikisha<br />

kwamba tunakuwa na viwanda ambavyo vitaongeza thamani ya mazao yetu ili tuweze kupata<br />

bei nzuri zaidi katika Soko la Dunia. Kwa hiyo, nimhakikishie tu Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> kwamba,<br />

Serikali itaendelea na mpan<strong>go</strong> wake huu wa miaka mitano na itatoa kipaumbele katika maeneo<br />

ambayo vilevile Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> ameyataja.<br />

MHE. MESHACK J. OPULUKWA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Sambamba na<br />

zao la korosho, napenda kumwuliza Mheshimiwa Waziri swali do<strong>go</strong> la nyongeza. Ni lini sasa Serikali<br />

itaacha kuweka zuio kwa wakulima wa Mikoa ya Shinyanga hususan Wilaya ya Meatu la kuwazuia<br />

kuchanganya pamba pamoja na mahindi<br />

Mheshimiwa Spika, ahsante.<br />

SPIKA: Mheshimiwa M<strong>bunge</strong>, nasikitika sana sio swali lenyewe. Nasikitika sana! Mheshimiwa<br />

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Mahusiano na Uratibu) unataka kujibu, lakini swali siyo lenyewe<br />

kabisa!<br />

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MAHUSIANO NA URATIBU): Mheshimiwa Spika, pamoja na<br />

kwamba swali lililoulizwa ni tofauti na swali la msingi, lakini kwa manufaa ya wakulima wa pamba<br />

katika Mkoa wa Shinyanga ambao wamekuwa wakichanganya pamba na mahindi, ningependa<br />

kusema kwamba kiutaalam na kwa mujibu wa matokeo ya utafiti, mazao ya mahindi kwa<br />

7

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!