28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

MHE. MODESTUS D. KILUFI: Basi Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani ujumbe umefika,<br />

nashukuru sana. (Makofi)<br />

MWENYEKITI: Haya bwana ujumbe umefika.<br />

Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> tunaendelea nilisema atakayefuata ni Mheshimiwa Zarina,<br />

atafuatiwa na Mheshimiwa Rebecca Mn<strong>go</strong>do.<br />

MHE. ZARINA S. MADABIDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kupata nafasi hii.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimshukuru Mwenyezi Mungu halafu niwatakie<br />

Ramadhani Karim ndugu zangu wote waliofunga na nawatakia rehema na amani Watanzania<br />

wote. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kusema siungi mkono hoja na nitawaomba<br />

Waheshimiwa Wa<strong>bunge</strong> wanisaidie kutokuunga mkono hoja, kwa sababu gani Kuna mradi<br />

mkubwa wa upanuzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi ambao unataka kuruka wakati<br />

wowote. Mradi wa dola milioni 76.5 takribani ni shilingi bilioni 115. Ninasema siungi mkono hoja<br />

kwa sababu sioni utashi kwa upande wa Wizara ya Ardhi kutaka mradi huu kweli uendelee,<br />

nitatoa sababu.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chuo Kikuu cha Afya, MUHAS waliomba ardhi mwaka 2004 na<br />

wakapewa mwaka 2006 katika maeneo ya Kwembe na Mloganzila. Ardhi hii ilikuwa ni ardhi<br />

ambayo inamilikiwa huko nyuma na mpaka sasa hivi title ndio inavyosema ni ya KABIMITA na<br />

Tanganyika Packers. Wamepewa ardhi ile na Mheshimiwa Rais alikwenda kuomba mkopo Korea<br />

ya Kusini akapata fedha hizo dola milioni 76.5 kuja kujenga Chuo Kikuu hiki. Hiki Chuo Kikuu<br />

ambacho ndio tunatarajia kipanue nyanja zote za afya, kiweze kuwafunza wataalam wa afya,<br />

kiweze ku-save fedha za Serikali za kupeleka watu nje kwa sababu wengi watakuwa wanatibiwa<br />

hapa, lakini kumekuwa na dillydally isiyoeleweka.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Rais alipokwenda Korea amepata mwekezaji, mikataba<br />

imesainiwa, mwekezaji amekuja, sio mwekezaji huyu anayetoa mkopo, tumekopa. Masharti ya ule<br />

mkopo unasema riba yake ni asilimia 0.01, ndo<strong>go</strong> sana. Muda wa kun<strong>go</strong>jea miaka 15, malipo<br />

miaka 45, tunataka nini kingine Ukiangalia bajeti ya Wizara ni shilingi bilioni 22 huyu anatupa<br />

mkopo wa shilingi bilioni 115. Sasa wataalam wako hapa tokea mwezi Juni hawajaweza kuaccess<br />

kule kwenda kuchukua hata udon<strong>go</strong>. Wizara inalijua hilo, Wizara ya Elimu imeandika<br />

barua nyingi, MUHAS imeandika barua nyingi na naomba kwanza ni-declare interest kwamba<br />

mimi ni Makamu Mwenyekiti wa Council ya MUHAS, kwa hiyo ninalijua vizuri sana suala hili.<br />

Mkataba umeshasainiwa na consultant ameshateuliwa. Consultant amekuja hapa akiamini kabisa<br />

kwamba anakuja kuanza kazi. Amekuja hapa hakuna kitu kinaendelea tokea mwezi Juni. Juni<br />

imemalizika, Julai imemalizika na A<strong>go</strong>sti kesho kutwa inakwisha hivi kweli sisi tunataka Chuo hicho<br />

kijengwe. Nasema hatuko serious kwa sababu kuna wakati Wizara ya Ardhi iliomba kwamba<br />

imege kipande cha ardhi ya pale Mloganzila ili wagawanye kwa watu wengine wakisema<br />

kwamba ni kubwa. Kama isingekuwa Mheshimiwa Rais kuingilia kati wangeshakata. Sasa kweli<br />

walikuwa wanataka huu mradi uendelee<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, wamekwenda watu wa ardhi wamefukuzwa lakini Serikali<br />

ilikwishatoa fidia ya shilingi bilioni nane tokea mwaka jana na shilingi bilioni nane hiyo ni watu 1,917.<br />

Wakatokeza watu wengine wakasema sisi bado, lakini malipo kesho, kesho kutwa watu 303 na leo<br />

wanatokea watu wengine wanasema hawajalipwa sasa wako 617. Nasema huu mradi ni wa<br />

maslahi ya wananchi wa Tanzania wote milioni 40, ndio tutategemea pale. Sasa hivi pale<br />

Mutumbili hao Wakorea wamejifinya wanajenga Chuo pamoja na hospitali kubwa, hivi nani<br />

ambaye haitamfaa<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeongea na Diwani wa Kwembe, nikawauliza, kwa nini<br />

mnakataa hawa consultant hata wasije kuchukua udon<strong>go</strong> Wakasema ndio tumekataa kwa<br />

sababu tuliambiwa tutalipwa fidia na sasa hivi hatujui Wizara ya Ardhi inasema nini. Mpaka leo<br />

69

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!