28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

na maombi ya kampuni hiyo kuwa katika hatua tofauti za kushughulikiwa katika Vijiji mbalimbali.<br />

Hivyo, ardhi iwe inatolewa kwa jinsi itakavyokuwa inapatikana baada ya kupanga mpan<strong>go</strong> mzuri<br />

wa matumizi ya ardhi”. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, huu ni ushauri na ni agizo kutoka kwa Katibu Mkuu, TAMISEMI<br />

akimuagiza Mkurugenzi wangu na anauelekeza uon<strong>go</strong>zi wa Mkoa wa Tanga. Wakati sisi<br />

tunajiandaa kutekeleza haya, tayari linakuja agizo hili kwamba wawekezaji hao wa Kampuni ya<br />

Arkadia wameshapewa ardhi hekta 25,000. Hatutakubaliana na hili! Hatusemi hivi kwa sababu<br />

hatutaki wawekezaji, la hasha!<br />

Mheshimiwa Spika, watu wa Mkinga tuna uzoefu wa kukaa na wawekezaji. Tunayo<br />

mashamba 10 ya wawekezaji mbalimbali. JKT Maramba wana hekta 2,416, Mwele Seed Farm<br />

wana hekta 954, Lu<strong>go</strong>n<strong>go</strong> Sisal Estate wana hekta 3,831, Mtapwa wana hekta 476, Kauzeni wana<br />

hekta 190, Mjesani wana hekta 9,081, Mavovo Farm wana hekta 1,503, Kwamtili wana hekta 700,<br />

Manza Estate wana hekta 386 na Mkomazi au Moa East wana hekta 6,292. Kwa hiyo, huu ni<br />

ushahidi tosha kwamba tunawapenda wawekezaji na tumekuwa tukiishi vizuri na wawekezaji<br />

hawa lakini sasa hili la mwekezaji mmoja kumpa hekta 25,000 bila maridhiano na wanavijiji husika<br />

na uon<strong>go</strong>zi wa Wilaya si sahihi hata kido<strong>go</strong>. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, lakini kinachouma zaidi, wapo wafugaji Wamasai ambao wamekuwa<br />

wakiomba maeneo waliyonyang’anywa yakaitwa ni maeneo ya hifadhi, wamewekeza kwenye<br />

maeneo yale, wamechimba visima na malambo kwa nguvu zao wenyewe, wamepoteza karibu<br />

shilingi milioni 10, suala lao ni la miaka mitano iliyopita. Yupo mwekezaji Ma<strong>go</strong>di ambaye ni<br />

Mmasai ameomba ekari 3,000 amenyimwa na kijiji kwa sababu kijiji hicho hakina ardhi lakini<br />

anapokuja mwekezaji Muitaliano anapewa ardhi ile bila ya Serikali ya Kijiji kushirikishwa. Hii si sahihi!<br />

Mheshimiwa Spika, hivi tunaitakia mema nchi yetu Vijiji viwili kati ya hivi vinavyotajwa viko<br />

kwenye mpaka na Kenya Hivi ni nani Serikalini asiyejua kwamba Wilaya ya Mkinga ina porous<br />

border kwamba tuna tatizo la watu kuingia hovyo kwenye nchi yetu katika ukanda ule Tuna<br />

tatizo la Wasomali na Waethiopia kwa kupitia maeneo ya Bahari na kupitia maeneo haya ya<br />

Kenya wanapita kila uchao bila matatizo Kama hiyo haitoshi leo tunakwenda kumpa mwekezaji<br />

maeneo hayo ya mpakani. Are we serious Watu wa Mkinga wameniambia nisiunge mkono hoja<br />

hii. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, mion<strong>go</strong>ni mwa maeneo tunayopigiwa kelele kwa njaa ndiyo maeneo<br />

haya leo ambayo watu hawa wanaporwa ardhi hii. Kichekesho zaidi ni kwamba wapo watu<br />

katika Wizara wanampotosha Mheshimiwa Rais. Wanataka kumfanya Mheshimiwa Rais achukiwe<br />

na watu wa Mkinga, watu wa Mkinga wanaipenda Serikali ya Chama cha Mapinduzi ndiyo<br />

maana siku zote tumekuwa tukiiunga mkono Serikali ya Chama cha Mapinduzi, hatutakuwa tayari<br />

kuona watu wachache wanavuruga sifa hii ya watu wa Mkinga. Tunaomba alishughulikie suala hili<br />

ili watu wale waendelee kuwa na imani na Serikali yao.<br />

Mheshimiwa Spika, sitaunga mkono hoja hii kwa sababu haya ndiyo matakwa ya<br />

wananchi wa Mkinga, wananchi wa Tarafa ya Maramba ambao leo hii ni mion<strong>go</strong>ni mwa watu<br />

ambao tunawaambia tunawapokonya ardhi, leo hii wanaishi kwa shida. Walikuwa wanalima<br />

kwenye mashamba ya JKT, tumewazuia. Serikali ya Wilaya inajipanga sasa kuwahamishia<br />

wananchi hawa na kuwawezesha walime katika maeneo ambayo leo yanachukuliwa anapewa<br />

mwekezaji, tunakwenda wapi Kwa nini Serikali haizungumzi kwa kauli moja Kwa nini Watendaji<br />

Wakuu wa Serikali hiyohiyo wanatofautiana Naomba mlishughulikie suala hili ili tusije tukaleta<br />

matatizo. Tunaomba uamuzi ule wa kwanza wa kusema kwamba matumizi bora ya ardhi<br />

yafanywe halafu Serikali ya Wilaya na Mkoa viangalie ni kwa jinsi gani inaweza kumgawia<br />

mwekezaji huyu ardhi yafuatwe. Hatutakuwa tayari kuona tunaendelea na maumivu ya<br />

kupokonywa ardhi wakati sisi wenyewe hatuna ardhi.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana Mheshimiwa Rais alipokuja katika Wilaya yetu alitoa<br />

agizo akasema, sasa watu wa Mkinga anzeni kuingia kwenye kuzalisha zao la Kakao. Maeneo<br />

ambayo tumeyapanga kwamba tuwashawishi watu wetu wawekeze katika kilimo cha Kakao<br />

ndiyo maeneo hayo ambayo Wizara yake wanayapora. Hivi ni nani huyu anayeweza kukinzana<br />

63

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!