28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

wapo, Majeshi yapo, bunduki zipo lakini watu wamezikimbia bunduki, wakakimbia Ikulu<br />

wakaondoka. Tafadhalini kaeni na watu vizuri, jaribuni kuwaridhisha watu na waone kuwa<br />

mnawahurumia. Msiwafikishe watu mahali wakalalamika sana mpaka ikapita kiasi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Ardhi. Sheria ya Ardhi ina matatizo. Ni nchi chache<br />

sana duniani leo ambazo anakwenda mtu mgeni kwa kisingizio cha uwekezaji akapewa ardhi<br />

anayokata, akafanya anavyotaka kama wanavyofanya hapa Tanzania. Lazima Sheria ibadilishwe<br />

ili mwekezaji aweze kuwekeza au awe partnership na Mtanzania na hiyo ndiyo namna ya<br />

kuwawezesha watu wetu. Kama tunataka kuwawezesha, tufanye hivyo. Si geni hili, leo huwezi<br />

kwenda nchi za Uarabuni pamoja na utajiri wao ukaweza hata siku moja kufanya biashara yoyote<br />

kama huna ubia na mzalendo wa pale. Maana yake ni nini Hutaweza kuhamisha mali<br />

kiujanjaujanja ukifika mahali umeshindwa unaambiwa ondoka, biashara na mali inabaki ndani ya<br />

nchi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa imekuwa ile lugha waliyosema, yupo mtu mmoja<br />

mashuhuru sana ndani ya nchi alifananisha timu yetu ya Taifa na Kichwa cha Mwendawazimu kila<br />

mtu anayekuja ananyoa anavyotaka. Haiwezekani, ardhi ni kitu muhimu sana, ndiyo rasilimali ya<br />

Watanzania halafu tunaiachia hivihivi tu, watu wanakuja wanapewa wanavyotaka, wanafanya<br />

wanavyotaka ilhali wanyonge hawana wanachoambulia.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naiomba Serikali, hebu tufikie mahali suala hili la mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro<br />

baina ya wafugaji na wakulima limalizwe. Mheshimiwa Waziri Mkuu aliulizwa humu ikaundwa<br />

Tume. Maswali yanayokuja, yanaulizia masuala haya na kila leo linaendelea. Tutafika wapi Hivi ni<br />

suluhisho unaondoa wafugaji katika eneo fulani unawapeleka kwenye eneo ambalo watu wa<br />

eneo hilo hukuwauliza kwa sababu tu ni raia wako Haiwezekani! Kama wewe unaona wafugaji ni<br />

kero upande wako basi na wale ambao walikuwa hawajazoea kuwaona wafugaji vilevile<br />

wanaona ni kero. Kuna rafiki yangu M<strong>bunge</strong> mmoja wa Mikoa ya Kusini aliwahi kusema hapa<br />

kwamba wao wakiona ng’ombe wanashtuka sana kwa sababu hawakuzoea kuwaona ng’ombe.<br />

Sasa kama mtu hakuwahi kuona ng’ombe, akiona ng’ombe mmoja anao<strong>go</strong>pa, unampelekeaje<br />

ng’ombe 3,000 Baya si hilo, watu wana<strong>go</strong>mbana. Hivi kweli Serikali iko tayari ione watu<br />

wanauana kwa sababu hii ya ku<strong>go</strong>mbania ardhi Kwa nini hampimi, mkasema eneo hili la<br />

wafugaji, eneo hili la wakulima, eneo hili la watu fulani, kila mtu akajua eneo lake. Yule anayevuka<br />

mipaka yake ni rahisi kumhukumu kwa sababu umeshamwekea mipaka yake lakini mnaacha hali<br />

mpaka iwe mbaya ndiyo mnapeleka Polisi wakapige watu, mnapeleka Majeshi wapige watu bure<br />

tu kumbe mngeweza kuondoa tatizo hilo kwa kutumia maarifa, kwa kutumia busara. Nguvu<br />

hazijengi kila wakati. Mara nyingi unapoamua kufanya kitu kwa kutumia nguvu unaharibu, fanya<br />

kitu kwa kutumia akili, akili itakuon<strong>go</strong>za vizuri. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)<br />

MHE. MARIAM S. MFAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili na<br />

mimi niweze kuchangia kuhusu Wizara yetu hii ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaanza kuchangia, nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu<br />

kwa kutujalia sisi sote afya njema na kuwepo katika Ukumbi huu wa Bunge jioni hii. Vilevile<br />

niwapongeze ndugu zangu Waislam kwa mfun<strong>go</strong> mzuri wa mwezi wa Ramadhan. Nawatakia kila<br />

la kheri lakini na ninyi ndugu zetu tuwe pamoja na tushirikiane maana mfun<strong>go</strong> huu ndiyo ni kwa<br />

Waislam lakini vilevile na nyie mko ndani yake. Kwa hiyo, kwa pamoja nasema Mungu atujalie kila<br />

la kheri tuendelee kumaliza shughuli hii ya kufunga. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu<br />

Mkuu pamoja na Watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kusukuma<br />

maendeleo ya wananchi kupitia Wizara yao. Niwapongeze sana na nimpongeze sana<br />

Mheshimiwa Waziri yeye ni mgeni katika Wizara lakini kwa jinsi alivyokuja na kuelewa na kuisoma<br />

na jinsi alivyowasilisha hotuba yake, nina uhakika ataendelea kuisimamia vizuri. Nakutakia kila la<br />

kheri Mama Tibaijuka.<br />

73

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!