Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
wapo, Majeshi yapo, bunduki zipo lakini watu wamezikimbia bunduki, wakakimbia Ikulu<br />
wakaondoka. Tafadhalini kaeni na watu vizuri, jaribuni kuwaridhisha watu na waone kuwa<br />
mnawahurumia. Msiwafikishe watu mahali wakalalamika sana mpaka ikapita kiasi. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Ardhi. Sheria ya Ardhi ina matatizo. Ni nchi chache<br />
sana duniani leo ambazo anakwenda mtu mgeni kwa kisingizio cha uwekezaji akapewa ardhi<br />
anayokata, akafanya anavyotaka kama wanavyofanya hapa Tanzania. Lazima Sheria ibadilishwe<br />
ili mwekezaji aweze kuwekeza au awe partnership na Mtanzania na hiyo ndiyo namna ya<br />
kuwawezesha watu wetu. Kama tunataka kuwawezesha, tufanye hivyo. Si geni hili, leo huwezi<br />
kwenda nchi za Uarabuni pamoja na utajiri wao ukaweza hata siku moja kufanya biashara yoyote<br />
kama huna ubia na mzalendo wa pale. Maana yake ni nini Hutaweza kuhamisha mali<br />
kiujanjaujanja ukifika mahali umeshindwa unaambiwa ondoka, biashara na mali inabaki ndani ya<br />
nchi. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa imekuwa ile lugha waliyosema, yupo mtu mmoja<br />
mashuhuru sana ndani ya nchi alifananisha timu yetu ya Taifa na Kichwa cha Mwendawazimu kila<br />
mtu anayekuja ananyoa anavyotaka. Haiwezekani, ardhi ni kitu muhimu sana, ndiyo rasilimali ya<br />
Watanzania halafu tunaiachia hivihivi tu, watu wanakuja wanapewa wanavyotaka, wanafanya<br />
wanavyotaka ilhali wanyonge hawana wanachoambulia.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naiomba Serikali, hebu tufikie mahali suala hili la mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro<br />
baina ya wafugaji na wakulima limalizwe. Mheshimiwa Waziri Mkuu aliulizwa humu ikaundwa<br />
Tume. Maswali yanayokuja, yanaulizia masuala haya na kila leo linaendelea. Tutafika wapi Hivi ni<br />
suluhisho unaondoa wafugaji katika eneo fulani unawapeleka kwenye eneo ambalo watu wa<br />
eneo hilo hukuwauliza kwa sababu tu ni raia wako Haiwezekani! Kama wewe unaona wafugaji ni<br />
kero upande wako basi na wale ambao walikuwa hawajazoea kuwaona wafugaji vilevile<br />
wanaona ni kero. Kuna rafiki yangu M<strong>bunge</strong> mmoja wa Mikoa ya Kusini aliwahi kusema hapa<br />
kwamba wao wakiona ng’ombe wanashtuka sana kwa sababu hawakuzoea kuwaona ng’ombe.<br />
Sasa kama mtu hakuwahi kuona ng’ombe, akiona ng’ombe mmoja anao<strong>go</strong>pa, unampelekeaje<br />
ng’ombe 3,000 Baya si hilo, watu wana<strong>go</strong>mbana. Hivi kweli Serikali iko tayari ione watu<br />
wanauana kwa sababu hii ya ku<strong>go</strong>mbania ardhi Kwa nini hampimi, mkasema eneo hili la<br />
wafugaji, eneo hili la wakulima, eneo hili la watu fulani, kila mtu akajua eneo lake. Yule anayevuka<br />
mipaka yake ni rahisi kumhukumu kwa sababu umeshamwekea mipaka yake lakini mnaacha hali<br />
mpaka iwe mbaya ndiyo mnapeleka Polisi wakapige watu, mnapeleka Majeshi wapige watu bure<br />
tu kumbe mngeweza kuondoa tatizo hilo kwa kutumia maarifa, kwa kutumia busara. Nguvu<br />
hazijengi kila wakati. Mara nyingi unapoamua kufanya kitu kwa kutumia nguvu unaharibu, fanya<br />
kitu kwa kutumia akili, akili itakuon<strong>go</strong>za vizuri. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)<br />
MHE. MARIAM S. MFAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili na<br />
mimi niweze kuchangia kuhusu Wizara yetu hii ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaanza kuchangia, nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu<br />
kwa kutujalia sisi sote afya njema na kuwepo katika Ukumbi huu wa Bunge jioni hii. Vilevile<br />
niwapongeze ndugu zangu Waislam kwa mfun<strong>go</strong> mzuri wa mwezi wa Ramadhan. Nawatakia kila<br />
la kheri lakini na ninyi ndugu zetu tuwe pamoja na tushirikiane maana mfun<strong>go</strong> huu ndiyo ni kwa<br />
Waislam lakini vilevile na nyie mko ndani yake. Kwa hiyo, kwa pamoja nasema Mungu atujalie kila<br />
la kheri tuendelee kumaliza shughuli hii ya kufunga. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu<br />
Mkuu pamoja na Watendaji wote wa Wizara kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kusukuma<br />
maendeleo ya wananchi kupitia Wizara yao. Niwapongeze sana na nimpongeze sana<br />
Mheshimiwa Waziri yeye ni mgeni katika Wizara lakini kwa jinsi alivyokuja na kuelewa na kuisoma<br />
na jinsi alivyowasilisha hotuba yake, nina uhakika ataendelea kuisimamia vizuri. Nakutakia kila la<br />
kheri Mama Tibaijuka.<br />
73