Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
wananchi kwamba utaratibu tuliojiwekea wenyewe unakamilika lini Kwa sababu wameshasubiri<br />
mpaka wamechoka. Sasa wengine wanaweza wakaamua hata wakajenga na mkaona kwamba<br />
si watiifu lakini kumbe ni kule kusubiri watu wameshachoka. Wameshachoka kusubiri kwa hiyo<br />
wanaamua kuvunja Sheria. Niiombe Serikali iwaambie wananchi kwamba suala la Kigamboni<br />
mwisho wake ni lini. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la National Housing. Kwa wale ambao<br />
waliiona National Housing toka mwanzo inaanza na mpaka ikaendelea ikajenga nyumba katika<br />
Mikoa mingi mpaka sasa ilivyo, niwaombe sana na pengine nimwombe Mheshimiwa Waziri<br />
mhusika, labda ifike siku moja Wa<strong>bunge</strong> waandaliwe semina ili waelezwe jinsi National Housing<br />
sasa hivi inavyofanya kazi. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, National Housing iliyopo sasa, siyo ile ya siku zilizopita, ambayo<br />
ilikuwa hoi bin taaban. Ilishafika mahali haikuwa inaweza hata kukarabati nyumba. Lakini kwa sasa<br />
hivi National Housing iliyopo ni tofauti kabisa. Imekwishakarabati nyumba nyingi, imekwishajenga<br />
nyumba nyingi na kwa kweli inafanya kazi ambayo ni ya uhakika. Kwa mipan<strong>go</strong> waliyonayo kwa<br />
sisi wa Dodoma, kwa kweli tunashukuru Mungu. Tunashukuru sana kwa sababu zitajengwa<br />
nyumba 260 na nyumba 160 zitakuwa za kukodisha na nyumba 100 zitakuwa za kuuzia wananchi.<br />
Kwa kitendo hicho, nasema tunawashukuru sana vijana wetu wa National Housing na hasa<br />
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hili, kijana wetu Msechu amejitahidi kufanya kazi akishirikiana na<br />
wenzake na Wizara pamoja na Bodi inayohusika. Kwa hiyo, waendelee kuchapa kazi na wala<br />
wasirudi nyuma. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wa Dodoma tutakuwa tayari kununua hizo nyumba<br />
zitakazouzwa. Ila ninachokiomba, bahati nzuri jana walifanya uzinduzi wa ujenzi wa nyumba hizo<br />
na bahati nzuri maghorofa mawili tayari yamekwishajengwa. Sasa ninachowaomba au<br />
ninachoiomba Serikali, ambapo na Mheshimiwa Waziri alikisema mbele ya Waziri Mkuu kwamba,<br />
kuna gharama ambazo zinasababisha kupandisha bei ya nyumba, ni zile gharama za kupeleka<br />
maji na umeme. Niiombe sana Serikali na nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa sababu<br />
alikubali kukaa na watu wa maji na watu wa umeme. Sasa niombe basi, watakapokuwa tayari,<br />
basi ili kupunguza bei ya nyumba ambazo wananchi watauziwa, gharama hizo zigharamiwe na<br />
Serikali. Hata kama hizi zinazojengwa Dodoma ambazo tayari National Housing<br />
wamekwishapeleka umeme, watapeleka maji, basi hizo gharama zilipwe na Serikali ili nyumba<br />
zitakapokuwa tayari, zitakapouzwa, ile gharama ya umeme na maji iwe imekwishaondolewa pale<br />
ili bei kwa mnunuzi iwe rahisi. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niishukuru sana Serikali na nimshukuru sana sana<br />
Mheshimiwa Waziri kwa suala zima hili la kusimamia National Housing vizuri na mimi ni mjumbe wa<br />
Kamati ya Ardhi. Kwa hiyo tutashirikiana, tutasaidiana kuona kwamba nyumba nyingi zinajengwa<br />
kama walivyoahidi na kwa kutekeleza Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi. Kwa hiyo, tutashirikiana<br />
na tutasaidiana. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la mwisho ambalo ni kuhusu raia wa nchi za<br />
nje wanapoingia nchini kutafuta ardhi. Kuna maeneo ambayo wanapita na bahati nzuri<br />
wanajifunza nchi hii uendeshaji wake ukoje. Sisi Dodoma kuna hawa watu waliokuja kuchukua<br />
ardhi wakasingizia kwamba wanapanda Jatrofa. Kwa hiyo, wamechukua ardhi kubwa na Jatrofa<br />
hawapandi na mpaka sasa ardhi imekaa haina….<br />
(Hapa kengele Ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)<br />
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mfaki, kengele ya pili!<br />
MHE. MARIAM S. MFAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Ahsante<br />
sana na naunga mkono hoja! (Makofi)<br />
MWENYEKITI: Ahsante. Ujumbe wa Jatrofa umefika.<br />
75