28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

wananchi kwamba utaratibu tuliojiwekea wenyewe unakamilika lini Kwa sababu wameshasubiri<br />

mpaka wamechoka. Sasa wengine wanaweza wakaamua hata wakajenga na mkaona kwamba<br />

si watiifu lakini kumbe ni kule kusubiri watu wameshachoka. Wameshachoka kusubiri kwa hiyo<br />

wanaamua kuvunja Sheria. Niiombe Serikali iwaambie wananchi kwamba suala la Kigamboni<br />

mwisho wake ni lini. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la National Housing. Kwa wale ambao<br />

waliiona National Housing toka mwanzo inaanza na mpaka ikaendelea ikajenga nyumba katika<br />

Mikoa mingi mpaka sasa ilivyo, niwaombe sana na pengine nimwombe Mheshimiwa Waziri<br />

mhusika, labda ifike siku moja Wa<strong>bunge</strong> waandaliwe semina ili waelezwe jinsi National Housing<br />

sasa hivi inavyofanya kazi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, National Housing iliyopo sasa, siyo ile ya siku zilizopita, ambayo<br />

ilikuwa hoi bin taaban. Ilishafika mahali haikuwa inaweza hata kukarabati nyumba. Lakini kwa sasa<br />

hivi National Housing iliyopo ni tofauti kabisa. Imekwishakarabati nyumba nyingi, imekwishajenga<br />

nyumba nyingi na kwa kweli inafanya kazi ambayo ni ya uhakika. Kwa mipan<strong>go</strong> waliyonayo kwa<br />

sisi wa Dodoma, kwa kweli tunashukuru Mungu. Tunashukuru sana kwa sababu zitajengwa<br />

nyumba 260 na nyumba 160 zitakuwa za kukodisha na nyumba 100 zitakuwa za kuuzia wananchi.<br />

Kwa kitendo hicho, nasema tunawashukuru sana vijana wetu wa National Housing na hasa<br />

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hili, kijana wetu Msechu amejitahidi kufanya kazi akishirikiana na<br />

wenzake na Wizara pamoja na Bodi inayohusika. Kwa hiyo, waendelee kuchapa kazi na wala<br />

wasirudi nyuma. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wa Dodoma tutakuwa tayari kununua hizo nyumba<br />

zitakazouzwa. Ila ninachokiomba, bahati nzuri jana walifanya uzinduzi wa ujenzi wa nyumba hizo<br />

na bahati nzuri maghorofa mawili tayari yamekwishajengwa. Sasa ninachowaomba au<br />

ninachoiomba Serikali, ambapo na Mheshimiwa Waziri alikisema mbele ya Waziri Mkuu kwamba,<br />

kuna gharama ambazo zinasababisha kupandisha bei ya nyumba, ni zile gharama za kupeleka<br />

maji na umeme. Niiombe sana Serikali na nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa sababu<br />

alikubali kukaa na watu wa maji na watu wa umeme. Sasa niombe basi, watakapokuwa tayari,<br />

basi ili kupunguza bei ya nyumba ambazo wananchi watauziwa, gharama hizo zigharamiwe na<br />

Serikali. Hata kama hizi zinazojengwa Dodoma ambazo tayari National Housing<br />

wamekwishapeleka umeme, watapeleka maji, basi hizo gharama zilipwe na Serikali ili nyumba<br />

zitakapokuwa tayari, zitakapouzwa, ile gharama ya umeme na maji iwe imekwishaondolewa pale<br />

ili bei kwa mnunuzi iwe rahisi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niishukuru sana Serikali na nimshukuru sana sana<br />

Mheshimiwa Waziri kwa suala zima hili la kusimamia National Housing vizuri na mimi ni mjumbe wa<br />

Kamati ya Ardhi. Kwa hiyo tutashirikiana, tutasaidiana kuona kwamba nyumba nyingi zinajengwa<br />

kama walivyoahidi na kwa kutekeleza Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi. Kwa hiyo, tutashirikiana<br />

na tutasaidiana. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la mwisho ambalo ni kuhusu raia wa nchi za<br />

nje wanapoingia nchini kutafuta ardhi. Kuna maeneo ambayo wanapita na bahati nzuri<br />

wanajifunza nchi hii uendeshaji wake ukoje. Sisi Dodoma kuna hawa watu waliokuja kuchukua<br />

ardhi wakasingizia kwamba wanapanda Jatrofa. Kwa hiyo, wamechukua ardhi kubwa na Jatrofa<br />

hawapandi na mpaka sasa ardhi imekaa haina….<br />

(Hapa kengele Ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)<br />

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mfaki, kengele ya pili!<br />

MHE. MARIAM S. MFAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Ahsante<br />

sana na naunga mkono hoja! (Makofi)<br />

MWENYEKITI: Ahsante. Ujumbe wa Jatrofa umefika.<br />

75

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!