28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

la malighafi! Kwa ujumla eneo lote lina ukubwa wa hekta 922.22, eneo linalohusika na uzalishaji<br />

na malighafi lina ukubwa wa hekta 685. Eneo ambalo halitumiki na mwekezaji ni hekta 236.63. Ni<br />

eneo hili ambalo ndilo lina makazi ya wananchi ambao wengi wao walidhulumiwa kwa<br />

kulazimishwa kumpisha mwekezaji pasipo utaratibu wa kisheria kufuatwa! (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, tumekuwa tunaishauri Serikali ambayo inataka kuwaondoa wananchi<br />

kwa nguvu kuliangalia suala hili kwa busara ya hali ya juu. Tofauti na maeneo mengine ambayo<br />

kuna uvamizi wa maeneo ya watu, wananchi eneo hili, wengi wao ni watu wazima ambao wana<br />

kila ushahidi wa kuonyesha kwamba pale ni asili yao na kilichofanyika ni dhuluma dhidi yao<br />

kupisha wenye fedha na hawapo tayari kuacha makazi yao, wakiungwa mkono na M<strong>bunge</strong> wao<br />

na Madiwani wao wa Kata za Wazo na Bunju (CCM)! Tumeweka itikadi pembeni! (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, ufisadi wa ardhi na mustakabali wa Mtanzania maskini mkoa wa<br />

Mbeya, katika Wilaya ya Mbarali, shamba la mpunga la Mbarali (Mbarali Rice Farm - ekari 14437)<br />

na shamba la mpunga la Kapunga (ukubwa ekari 18425) yalikuwa ndio chanzo cha mapato<br />

cha wananchi wa eneo husika. Mashamba haya yalikuwa yanahudumia watu zaidi ya 30,000 na<br />

vijiji kumi. Ardhi hiyo pia ilikuwa inahudumia watu wa Iringa na Wilaya nyingine za Mbeya. Mipan<strong>go</strong><br />

ya awali ya Serikali, mwaka 2003/2004 kama ilivyobainishwa na aliyekuwa Waziri wa Kilimo ilikuwa<br />

ni kuyabinafsisha mashamba hayo kwa wakulima wado<strong>go</strong> wado<strong>go</strong>, mpan<strong>go</strong> ambao<br />

ungejumuisha mashamba ya Ruvu na Dakawa. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kutokana na nguvu ya mafisadi kuizidi hekima ya Serikali na licha ya<br />

kilio cha aliyekuwa M<strong>bunge</strong> wa Mbarali kipindi hicho Mheshimiwa Esterina Kilasi, Serikali iliamua<br />

kuuza eneo husika kwa Kampuni ya Highland Estates Ltd. Mmiliki wa sasa Bwana Nawab Mulla ni<br />

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Mbeya. Wananchi wamegeuka wapangaji kwa<br />

kukodisha maeneo ili waweze kulima na kujipatia kipato! (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, wakati Shamba la Mbarali akipewa kwa bei ya kutupa Mwenyekiti wa<br />

CCM, shamba la Kapunga lilibinafsishwa na kukabidhiwa kwa Kampuni ya Export Co. Ltd. kwa bei<br />

ya kutupa ya shilingi bilioni 2.3, mmiliki akiwa bwana Jeetu Patel (Jina halisi Jayantkumar<br />

Chandubhai Patel). (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, hii ndio Tanzania ambayo wazawa wananyang’anywa ardhi, maeneo<br />

yote muhimu na ya kimkakati na kukabidhiwa wageni au watu wenye mamlaka na fedha huku<br />

ikiwaacha wazawa kubaki vibarua au wakulima wado<strong>go</strong> wanaotegemea hisani ya mabeberu!<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, bado mustakabali wa shamba la mahindi Mbozi haujajulikana, serikali<br />

inataka kumpa mwekezaji, wakati wananchi wana uhaba wa ardhi kwa matumizi yao! Kambi ya<br />

Upinzani inaitaka Serikali itoe majibu kuhusiana na hatma ya shamba la mahindi mbozi.<br />

Halikadhalika, Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali iliambie Bunge hili Tukufu, ni vigezo gani<br />

vilivyotumika kupata wanunuzi wa shamba la mpunga la Mbarali, shamba la Kapunga na<br />

mashamba husika yaligawiwa kwa maslahi ya nani (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Mara, Musoma Mjini kumekuwa na mtafaruku mkubwa kati<br />

Jeshi la Wananchi (JWTZ) na wananchi wa Bukanga na Buhare (Mgaranjabo) kutokana na jeshi<br />

kujimilikisha maeneo yao ya asili, waliyokuwa wakitumia kwa ajili ya matambiko kwa kabila ya<br />

Wakwaya. Hivi sasa wananchi hao hawaruhusiwi kuingia katika eneo hilo, jambo hilo limezusha<br />

chuki kubwa sana kati ya Jeshi na jamii ya Wakwaya wakazi wa Musoma Mjini. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Moro<strong>go</strong>ro na matatizo ya ardhi, kwa wakubwa<br />

kunyang’anya wanyonge ardhi imeikumba pia Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero. M<strong>go</strong><strong>go</strong>ro huu<br />

unahusu shamba namba 299 (iliyokuwa NARCO Ranches),lenye ukubwa wa hekta 49,981.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, katika shamba hili taarifa zinaonyesha kwamba hekta 30,007<br />

walipewa Mtibwa Sugar licha ya malalamiko kutoka kwa wananchi kwamba eneo walilopewa ni<br />

46

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!