28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

kuhakikisha kwamba wanaochezea chezea pamba anawafukuza kazi. Wanaochezea chezea<br />

pamba kama Bodi, anaifukuza Bodi. Wanaochezea chezea pamba kama vile Mkurugenzi,<br />

anamfukuza ili kuhakikisha kwamba kweli yupo makini katika kuhakikisha kwamba anawasaidia<br />

watu hao. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, lakini niendelee, utawala huu wa ardhi bado haujatumalizia mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro,<br />

mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ipo kibao. Na siku hizi kwa sababu ardhi watu wengi wanakimbilia kutafuta maeneo<br />

ambayo sasa hivi yamekuwa haba na maeneo yamekuwa haba kwa sababu watu<br />

tumeongezeka. Tulipoanza Taifa hili tulikuwa watu 8,000,000 leo akinamama, akina baba<br />

wamefanya kazi nzuri, tuna zaidi ya watu 40,000,000 sasa hivi. Lakini kila wakati Serikali,<br />

inawanyang’anya watu ardhi yao! Aidha, inafanya mapori, au inafanya hifadhi, sasa hivi<br />

tumeelezwa na Kambi ya Upinzani, uwekezaji mkubwa wa ardhi kubwa na mambo kama hayo.<br />

Sasa sisi hatuna mahali pa kwenda! Sisi kule Sukuma land sasa hivi watu tumebanana hivi!<br />

Tunatafuta twende tukalime wapi Na Serikali hii inatuhimiza Kilimo Kwanza, tulime wapi Ukienda<br />

kugusa hapa, mwekezaji! Ukienda ukigusa hapa, mhifadhi! Ukienda ukigusa hapa, hujapata kibali!<br />

Twende wapi Tanzania hii ndio tumepewa na Mwenyezi Mungu tuitumie sisi kwanza. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mimi nimefurahishwa na dhana moja ambayo Waziri<br />

amesema, Land Bank (Hazina ya Ardhi), labda sasa wakati umefika, tupime ardhi yetu, tupime vijiji<br />

vipya na tumwambie kwamba wewe ukienda kijiji hiki maalum utapata heka kumi, utapata heka<br />

20 na tuziweke ambazo hizi ni za Watanzania tu na tuweke mahali kwamba kama ni mwekezaji<br />

aje hapa lakini usimpe bure! Hii biashara ya kumpa bure mtu anayetoka nje, imetoka wapi<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, leo ardhi kijijini, nina hakika thamani yake siyo chini ya shilingi 5,000 kwa<br />

kile eka. Sasa mtu unampa eka 40,000, umempa mtaji wa bure. Huyo mtu akichukua ile hati ya 99<br />

years anaingia ndani ya Benki, yule Mzungu anakuja hapa na ndala, unampa hiyo hati, anaingia<br />

pale ana mtaji wake wa kuanzia, tuuze! Mimi nilipokuwa mwekezaji Swaziland, nilinunua ardhi na<br />

nikaweka kiwanda, kwa nini mtu aje hapa apewe tu, hii kupewa tu imetoka wapi Hii ndiyo inaleta<br />

ufisadi na rushwa. Mimi naona imefika wakati sasa tuiangalie ardhi kama mali ili iweze kutusaidia.<br />

Mheshimiwa Spika, ni lazima tuiangalie Sheria upya, Sheria ya sasa ya kutenganisha kati ya<br />

Sheria ya general land yaani Sheria Na.4 na Sheria Na.5, mimi naona hii inaleta mchanganyiko<br />

mkubwa sana. Siku moja nilikuwa nazungumza na Jaji wa Mahakama wa Ardhi, nikamuuliza hivi<br />

tatizo ni nini, mbona mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro imejaa kila mahali. Akasema mojawapo ya tatizo ni Sheria. Nafikiri<br />

kuna haja ya kuangalia Sheria hii. Mimi sasa hivi nina mfano mkubwa sana wa ndugu yangu<br />

mmoja anaitwa Mwanachene Ikanda, ambaye mtu mmoja alikuwa nje ya kijiji cha Lagangabidili,<br />

huyu bwana kuna baba yake alifia pale, kaja kajenga kaburi, kesho yake yuko Mahakamani<br />

anasema hapa ni ardhi yangu na maskini huyu sasa amekaa pale miaka na miaka, ana zaidi ya<br />

wajukuu 30 lakini kwa kutumia Sheria tuliyonayo sasa anafukuzwa na leo kama Mungu<br />

asiponisaidia kumsaidia, nyumba zake zote zinavunjwa, kwa sababu mtu ametumia Sheria<br />

tulizonazo ambazo hazikidhi mahitaji ya Taifa letu. Nafikiri kuna haja kubwa sana ya kuangalia hizi<br />

Sheria zetu upya na kwa huyu mwananchi Mheshimiwa Waziri kama anaweza kunisaidia akaweza<br />

kunihakikisha kwamba atasaidiwa angalau familia yake pale, naomba ndugu yangu afanye hivyo<br />

kwa sababu anapenda watu. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, la mwisho nataka kuzungumzia juu ya Shirika la Nyumba. Shirika la<br />

Nyumba kwa maoni yangu kama kuna kitu ambacho Mwalimu alikabidhi nchi hii ni utajiri mkubwa<br />

wa nyumba, pamoja na kwamba Serikali ya Awamu nyingine ilianza kuuza nyumba za Serikali,<br />

hiyo tutaishia hapo. Mimi sijaona Shirika ukiliangalia kithamani lililo na pesa nyingi kama Shirika la<br />

Nyumba, labda tuliangalie kwa mtazamo huo tusiliangalie kama Shirika ambalo linatoa service tu,<br />

mambo ya kutoa huduma dunia hii yamekwisha, Mr. Bure alishakufa siku nyingi, siku hizi lazima<br />

tuangalie kilicho na thamani lazima ukinunue na ukinunue kwa bei ya soko. Kwa hiyo, mimi naona<br />

mtazamo wake lazima sasa hivi tuanze kuufikiria upya. Mimi nafikiri kama Shirika la Nyumba<br />

linataka kutujengea nyumba, lina uwezo huo, lina uwezo wa kukopa kwa sababu dhamana ipo.<br />

Ukiangalia Upanga yote hiyo ni mabilioni ya shilingi, ni benki gani itakayoifungia mlan<strong>go</strong> Shirika la<br />

Nyumba Kwa hiyo, likielekezwa katika mtazamo huo, nafikiri litaweza kutujengea nyumba nyingi<br />

na iuze kwa bei ya soko, mambo ya burebure haya yameshapitwa na wakati. (Makofi)<br />

57

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!