Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
hawakushirikishwa hata kido<strong>go</strong>. Maafisa wa Mipan<strong>go</strong> Miji walichofanya walikwenda katika<br />
maeneo ambayo kwa wanakijiji wale ni maeneo muhimu sana kwao kwa sababu walikuwa<br />
wakilima mazao ya kudumu, kulikuwa na minazi, miembe, na mazao ya muda mfupi, kulikuwa na<br />
makaburi, walikuwa na eneo la kuweza kuchungia wanyama wao kama ng’ombe, kondoo na<br />
mbuzi.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, walichofanya ni kwamba walipima kwa ujanja ujanja ambalo ni<br />
kosa la kwanza walilolifanya. Pili, hawakuwapa fomu namba 69, ambayo ni muhimu sana kwani<br />
ndiyo inayoonesha vitu vyote vitakavyofanyiwa tathmini. Wanakijiji walipohoji siku hizi wanakijiji<br />
wote siyo kama hawaelewi, afadhali kido<strong>go</strong> shule za Kata zimesaidia, kuna vijana wana uelewa<br />
mzuri. Walipohoji mbona hatukupewa fomu namba 69, Afisa Mipan<strong>go</strong> Miji Ndugu Mapunda<br />
akawajibu kuwa kama mnaona mnadhulumiwa nendeni Mahakamani. Kwa hiyo amewadhalilisha<br />
kwanza, amewadharau wanakijiji wale, ndivyo ambavyo walijisikia.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni ya Tanga Cement, baada ya kufanya tathmini na<br />
kutokuwapa kila mmoja kujua ana ekari ngapi, kampuni ya Tanga cement ikalipa, ikatoa pesa zile<br />
kwa Halmashauri, awamu ya kwanza walilipa milioni 345, pesa hizo ziligawanywa kwa Serikali ya<br />
Kijiji ilipata milioni 26 kwa wakati huo, sijui ni kweli, zipo kwenye akaunti au nazo zimeliwa. Kwa<br />
baadhi ya wanakijiji waliobahatika kupata fidia hiyo ambao ni wachache tena waliwalipa kwa<br />
kuwalaghai kwa sababu ilikuwa ni mwezi wa Ramadhani na sikukuu inakaribia, wakawaita,<br />
wakaona hawana jinsi kwa sababu ni maskini bila kuambiwa una heka ngapi. Aliyelipwa laki saba,<br />
aliyelipwa milioni mbili, ambapo kwa jumla haifiki hata milioni hamsini kwa wale baadhi waliolipwa,<br />
wengine wali<strong>go</strong>ma.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ukiangalia pesa zote zilizobakia milioni takriban mia<br />
mbili na zaidi hazijulikani zilikokwenda. Hii inaonesha kuwa, pesa zote hizo wamezitafuna bila ya<br />
imani, bila ya huruma, bila ya hofu hata ya kumuo<strong>go</strong>pa Mwenyezi Mungu. Hapa kuna tatizo<br />
kubwa sana katika kijiji hiki na uon<strong>go</strong>zi wa Mipan<strong>go</strong> Miji. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya Wanakijiji ambao walikuwa wanadai walikuwa ni 30 katika<br />
orodha, lakini watu wa Mipan<strong>go</strong> Miji kwa kushirikiana na Serikali ya Kijiji ambao nao waliwaingiza<br />
katika mte<strong>go</strong> waliongeza watu hewa 36, kwa hiyo jumla wakawa watu 66. Wanakijiji wale<br />
hawakukubali saruji kuchimbwa katika eneo lao, wali<strong>go</strong>ma na walikaa kikao wakaunda Kamati<br />
Ndo<strong>go</strong> ya kwenda kushughulikia tatizo lao hilo. Walikwenda kwa Mkurugenzi na wengine<br />
walijigawa kwenda kwa mwakilishi wa saruji. Saruji alipoona matatizo yanaongezeka akaongeza<br />
milioni 70 ili walipwe wale wanakijiji ambao wana malalamiko. Kwa taarifa nilizonazo, hiyo milioni<br />
70 mpaka sasa hivi iko Halmashauri haijagawiwa kwa sababu kila leo wanaongezeka watu, au<br />
yanaongezeka madai mapya, ndio sababu walizozitoa.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ujumla fedha zote zilizolipwa na mwekezaji huyu saruji milioni<br />
415. Kwa haraka haraka ukiangalia zoezi zima la uthamini mpaka ulipaji fidia lilikuwa na kasoro<br />
nyingi pamoja na usiri mkubwa na limegubikwa na mazingira ya rushwa tena ya hali ya juu.<br />
Mkurugenzi akaona njia pekee ya kuwatuliza wanakijiji ni kuunda Tume, Tume ikaundwa ya<br />
kuchunguza, Tume ile imechukua takriban miezi mitatu bila kutoa taarifa yoyote. Mkuu wa Wilaya<br />
hali kadhalika alikuwa na Tume yake lakini hakuna ambacho wamekuja nacho.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wale wanacheleweshwa kila leo wanapewa taarifa<br />
mpya na huku mwekezaji cha kushangaza sasa tarehe 13 Juni, 2011 saruji walipata ruhusa kutoka<br />
kwa Mkuu wa Wilaya na kwenda kuchimba tani 5000 za majaribio kwa malighafi hiyo. Ni udon<strong>go</strong><br />
ambao unachanganywa na material nyingine kutengeneza saruji. Wanakijiji wale walistuka sana<br />
na hawakukubaliana na hilo lakini alichofanya Mkuu wa Wilaya aliwashirikisha baadhi ya Vion<strong>go</strong>zi<br />
wa Kijiji na Kata ambao wamepata marupurupu haya, wakaenda kwa nguvu katika eneo hilo<br />
wakasafisha eneo wakaweka ulinzi mkubwa ili mwekezaji yule achimbe. Sisi tunasema kuwa<br />
Tanzania tuna amani kama kweli, wanakijiji wale wameridhia Mtendaji yule kwa nini kumewekwa<br />
ulinzi mkubwa wa mgambo na marungu na mapanga ili mwekezaji yule aweze kuchimba<br />
(Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.<br />
82