Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
(c) Mheshimiwa Spika, mwaka 2008 mikataba ilifanyiwa durusu ili kuruhusu malipo ya<br />
mtaji wa mwekezaji na hivi sasa durusu inaendelea kuruhusu mradi wa Songas wa upanuzi wa<br />
miundombinu ya mradi wa Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong>. Aidha, bado Serikali na TPDC wako katika mazungumzo<br />
na Kampuni ya PAT kwa len<strong>go</strong> la kurekebisha maeneo kadhaa katika mkataba wa kugawana<br />
mapato ya mradi wa Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong>.<br />
MHE. YUSUPH A. NASSIR: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kumekuwa kuna mapungufu<br />
makubwa katika gharama zinazotolewa na Kampuni ya Songas pamoja na Pan Africa kwenye<br />
miradi mbalimbali. Je, nini kauli ya Serikali kuhusiana na kuhusisha Taasisi nyingine kama vile<br />
EWURA, Auditor General na hata PPRA kwa ajili ya kuhakiki na kutathmini gharama halisi za miradi<br />
hii<br />
Pili, kwa kuwa kumekuwa na mapungufu ya uadilifu wa kimkataba kati ya Pan Africa na<br />
TPDC kilichopelekea Serikali kupunjwa dola milioni 65 na hatimaye katika Mkutano uliofanyika<br />
mwezi Mei wakakubali kulipa dola milioni 28, ni lini fedha hizi zitarejeshwa Serikalini<br />
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, ni kweli, katika mfumo wa<br />
kufanya auditing ya gharama hizo, siyo kwa Songas na Pan Africa tumegundua kwamba kuna<br />
matatizo ambayo yametokea na kama unavyosema baada ya kufanyiwa auditing imegundulika<br />
na sisi katika upande wetu tumesema kwamba zilizopungua ni milioni 65 wao wamesema ni shilingi<br />
milioni 28, tumewaambia basi lipeni hizo kwanza. Lakini mkakati wa ku-involve hawa wote kwa<br />
maana ya CAG na nini, siyo tu kwa mkataba huu, lakini tunatarajia uwe ni utaratibu sasa wa<br />
kuwa, tuwe tuna macho zaidi katika mikataba yetu kwa sababu kwa namna hii tunaweza tukawa<br />
tunapoteza mapato mengi.<br />
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimekubali kwamba Taasisi nyingine ambazo zina uwezo wa<br />
kushiriki katika kubaini haya mapato ya Serikali yanayopotea yatashiriki katika kufuatilia mapato<br />
haya.<br />
SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, umeulizwa, ni lini shilingi milioni 28 zinalipwa<br />
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kama wiki mbili zilizopita<br />
tuliwaita Pan African na Songas na TPDC hapa Dodoma ili wakutane na Mheshimiwa Waziri wa<br />
Nishati na Madini pamoja na kubaini ile miradi mingine lakini pia kwa kujadiliana na hili. Kwa hiyo,<br />
kwa majadiliano ya malipo ya hii shilingi milioni 28 bado inaendelea, lakini tunawahimiza kwamba<br />
walipe haraka iwezekanavyo.<br />
MHE. SUSAN L. A. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa EWURA wametangaza asilimia<br />
tano ya ongezeko la bei ya mafuta na siku zilizopita walisema wana mafuta ya kutosha kwa siku<br />
48 mpaka 60 na kwa kisingizio kwamba shilingi imeporomoka. Je, hayo mafuta waliyoyapandisha<br />
ni haya yatakayokuja baadaye au haya yaliyoko ndani ya stock Kwa nini yamepandishwa<br />
SPIKA: Hili swali lilikuwa relevant kwa hili swali lililotoka. Hili swali la pili halikuwa relevant.<br />
Tusiulize maswali kwa sababu tunapenda, eeh! Mheshimiwa Waziri, tafadhali.<br />
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwa utaratibu wa kawaida wa<br />
kisheria, zoezi la kupitia bei ya bidhaa ya petroli nchini hufanyika kila baada ya wiki mbili, yaani siku<br />
14. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba kilichofanyika jana ni mwendelezo wa zoezi<br />
ambalo lilikuwa likifanyika kabla hata ya juzi formula ya kukokotoa bei kwenye bidhaa hizi<br />
kufanywa.<br />
Hili ni zoezi la kawaida. Wote tutakumbuka kwamba kuna kipindi ambapo kwa mfano<br />
kama hakuna ongezeko la bei ya mafuta katika soko la dunia ama hakuna mabadiliko katika<br />
exchange rate ya fedha yetu wakati fulani tumekuwa tukisikia bei za mafuta zinashuka. Kwa hili<br />
zoezi lililofanyika jana limezingatia hilo. Lakini kikubwa kilichosababisha jambo hilo ni mambo<br />
mawili. La kwanza, bei katika Soko la Dunia imeongezeka, lakini pia exchange rate ya fedha yetu<br />
imebadilika kido<strong>go</strong>.<br />
13