28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Kuhusu msaada wa UN-HABITAT, sina budi kuchukua fursa hii kumshukuru Katibu Mkuu<br />

Mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Mheshimiwa Kofi Annan, kwa kunipendekeza na nikachaguliwa<br />

na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuwa Katibu Mkuu Msaidizi wa Umoja wa Mataifa na<br />

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Makazi Duniani (UN-HABITAT) kwa miaka kumi (Septemba, 2000<br />

hadi A<strong>go</strong>sti, 2010). (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, katika kipindi hicho nilifanikiwa kujenga ushirikiano wa karibu na Serikali<br />

ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwezesha miradi kadhaa nchini kutekelezwa ambayo<br />

Shirika hilo linaendelea kuifadhili. Ushirikiano huo umezaa matunda mengi katika sekta mbalimbali.<br />

Kwa mfano, mchakato wa kuandaa Sheria ya Mikopo ya Nyumba na Sheria ya Umiliki wa Sehemu<br />

ya Jen<strong>go</strong> ambazo zilipitishwa na Bunge lako Tukufu mwaka 2008, ulitokana na ushauri wa UN-<br />

HABITAT. Sina budi kutambua ushirikiano mkubwa nilioupata katika kutekeleza majukumu yangu<br />

kama Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo kutoka kwa Mawaziri walionitangulia ambao walikuwa<br />

ni vion<strong>go</strong>zi wa ujumbe wa Tanzania katika Baraza la UN-HABITAT. (Makofi)<br />

Shukrani za kipekee nazitoa kwa Mheshimiwa John Pombe Magufuli, Waziri wa Ujenzi na<br />

M<strong>bunge</strong> wa Chato ambaye mwaka 2006 akiwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya<br />

Makazi alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kongamano la Maendeleo ya Miji la Umoja wa Mataifa<br />

(World Urban Forum II) lililofanyika Vancouver, Canada ambalo nililiandaa. Vilevile namshukuru<br />

Mheshimiwa John Chiligati, Naibu Katibu Mkuu, Tanzania Bara wa Chama cha Mapinduzi na<br />

M<strong>bunge</strong> wa Manyoni ambaye alinisaidia sana kutekeleza majukumu yangu ya Kimataifa.<br />

Namshukuru kwa jinsi alivyonikaribisha, niliporejea nyumbani, kwa upendo na akanikabidhi Wizara<br />

na kwa jinsi anavyoendelea kunishauri katika utekelezaji wa majukumu yangu. Hakika aliniachia<br />

msingi mzuri ambao nitauendeleza. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa mara nyingine napenda kumshukuru Naibu Waziri wa Wizara ya<br />

Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Goodluck Ole-Medeye, kwa kunisaidia<br />

katika kutekeleza majukumu yangu. Pia napenda kumshukuru Katibu Mkuu Bwana Patrick<br />

Rutabanzibwa na Naibu Katibu Mkuu Bibi Maria Bilia kwa ushirikiano mkubwa walionipa kwa kipindi<br />

kifupi tangu niteuliwe kuwa Waziri wa Wizara hii. (Makofi)<br />

Nawashukuru vilevile Wakuu wa Idara na Viten<strong>go</strong> katika Wizara, vion<strong>go</strong>zi wa taasisi zilizo<br />

chini ya Wizara, watumishi na wataalamu wote wa sekta ya ardhi kwa kunisaidia katika kutimiza<br />

majukumu yangu. Naomba waendelee kutekeleza majukumu yetu kwa kujielekeza katika<br />

kuchangia ipasavyo kuboresha mazingira ya kuondoa umaskini na kuendeleza biashara na<br />

uwekezaji. (Makofi)<br />

Natambua kuwa Wizara yangu haina nyenzo na rasilimali zote tunazohitaji, lakini hata kwa<br />

rasilimali tulizonazo, zikisimamiwa kwa uangalifu tukapata thamani inayowiana na rasilimali hizo<br />

(value for money), zitazaa matunda makubwa. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, hitimisho, kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu imeazimia kutekeleza<br />

mipan<strong>go</strong> ya kuendeleza ardhi, nyumba na makazi ili kukabiliana na changamoto zilizoainishwa<br />

katika hotuba hii. Aidha, itahakikisha kuwa upangaji na ugawaji wa ardhi, upangaji wa miji<br />

unaendelea kwa kuzingatia sheria zilizopo kwa usimamizi wa karibu. Vilevile Wizara kwa<br />

kushirikiana na Halmashauri tutawezesha upatikanaji wa ardhi kwa ajili ya wawekezaji kwa<br />

utaratibu mpya wa wananchi kutumia ardhi kama mtaji (land for equity). Hali kadhalika kwa<br />

kushirikiana na Halmashauri na wadau wengine Wizara itaendelea kutafuta ufumbuzi wa<br />

mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro sugu ya ardhi na tutajielekeza katika kuziba mianya inayosababisha mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro hiyo ili<br />

isiendelee kutokea.<br />

Mheshimiwa Spika, kwa hali hiyo Wizara yangu imejipanga kuhakiki, kupanga matumizi ya<br />

ardhi, kupima, kusajili na kutoa hati katika maeneo hayo ili kuwezesha kuwepo kwa usalama wa<br />

milki na hivyo kuondoa mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro kati ya watumiaji mbalimbali wa ardhi. Natoa rai kwa mamlaka<br />

na asasi mbalimbali kutoa ushirikiano unaotakiwa kuhakikisha kuwa ardhi inaziwezesha sekta zote<br />

kwa len<strong>go</strong> la kuwaondolea wananchi umaskini. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, maombi ya fedha kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu imejipanga<br />

kutekeleza majukumu yake iliyojiwekea ili kufikia malen<strong>go</strong> ya MKUKUTA II, Dira ya Taifa ya 2025 na<br />

36

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!