Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Kuhusu msaada wa UN-HABITAT, sina budi kuchukua fursa hii kumshukuru Katibu Mkuu<br />
Mstaafu wa Umoja wa Mataifa, Mheshimiwa Kofi Annan, kwa kunipendekeza na nikachaguliwa<br />
na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuwa Katibu Mkuu Msaidizi wa Umoja wa Mataifa na<br />
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Makazi Duniani (UN-HABITAT) kwa miaka kumi (Septemba, 2000<br />
hadi A<strong>go</strong>sti, 2010). (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, katika kipindi hicho nilifanikiwa kujenga ushirikiano wa karibu na Serikali<br />
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwezesha miradi kadhaa nchini kutekelezwa ambayo<br />
Shirika hilo linaendelea kuifadhili. Ushirikiano huo umezaa matunda mengi katika sekta mbalimbali.<br />
Kwa mfano, mchakato wa kuandaa Sheria ya Mikopo ya Nyumba na Sheria ya Umiliki wa Sehemu<br />
ya Jen<strong>go</strong> ambazo zilipitishwa na Bunge lako Tukufu mwaka 2008, ulitokana na ushauri wa UN-<br />
HABITAT. Sina budi kutambua ushirikiano mkubwa nilioupata katika kutekeleza majukumu yangu<br />
kama Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo kutoka kwa Mawaziri walionitangulia ambao walikuwa<br />
ni vion<strong>go</strong>zi wa ujumbe wa Tanzania katika Baraza la UN-HABITAT. (Makofi)<br />
Shukrani za kipekee nazitoa kwa Mheshimiwa John Pombe Magufuli, Waziri wa Ujenzi na<br />
M<strong>bunge</strong> wa Chato ambaye mwaka 2006 akiwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya<br />
Makazi alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kongamano la Maendeleo ya Miji la Umoja wa Mataifa<br />
(World Urban Forum II) lililofanyika Vancouver, Canada ambalo nililiandaa. Vilevile namshukuru<br />
Mheshimiwa John Chiligati, Naibu Katibu Mkuu, Tanzania Bara wa Chama cha Mapinduzi na<br />
M<strong>bunge</strong> wa Manyoni ambaye alinisaidia sana kutekeleza majukumu yangu ya Kimataifa.<br />
Namshukuru kwa jinsi alivyonikaribisha, niliporejea nyumbani, kwa upendo na akanikabidhi Wizara<br />
na kwa jinsi anavyoendelea kunishauri katika utekelezaji wa majukumu yangu. Hakika aliniachia<br />
msingi mzuri ambao nitauendeleza. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kwa mara nyingine napenda kumshukuru Naibu Waziri wa Wizara ya<br />
Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Goodluck Ole-Medeye, kwa kunisaidia<br />
katika kutekeleza majukumu yangu. Pia napenda kumshukuru Katibu Mkuu Bwana Patrick<br />
Rutabanzibwa na Naibu Katibu Mkuu Bibi Maria Bilia kwa ushirikiano mkubwa walionipa kwa kipindi<br />
kifupi tangu niteuliwe kuwa Waziri wa Wizara hii. (Makofi)<br />
Nawashukuru vilevile Wakuu wa Idara na Viten<strong>go</strong> katika Wizara, vion<strong>go</strong>zi wa taasisi zilizo<br />
chini ya Wizara, watumishi na wataalamu wote wa sekta ya ardhi kwa kunisaidia katika kutimiza<br />
majukumu yangu. Naomba waendelee kutekeleza majukumu yetu kwa kujielekeza katika<br />
kuchangia ipasavyo kuboresha mazingira ya kuondoa umaskini na kuendeleza biashara na<br />
uwekezaji. (Makofi)<br />
Natambua kuwa Wizara yangu haina nyenzo na rasilimali zote tunazohitaji, lakini hata kwa<br />
rasilimali tulizonazo, zikisimamiwa kwa uangalifu tukapata thamani inayowiana na rasilimali hizo<br />
(value for money), zitazaa matunda makubwa. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, hitimisho, kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu imeazimia kutekeleza<br />
mipan<strong>go</strong> ya kuendeleza ardhi, nyumba na makazi ili kukabiliana na changamoto zilizoainishwa<br />
katika hotuba hii. Aidha, itahakikisha kuwa upangaji na ugawaji wa ardhi, upangaji wa miji<br />
unaendelea kwa kuzingatia sheria zilizopo kwa usimamizi wa karibu. Vilevile Wizara kwa<br />
kushirikiana na Halmashauri tutawezesha upatikanaji wa ardhi kwa ajili ya wawekezaji kwa<br />
utaratibu mpya wa wananchi kutumia ardhi kama mtaji (land for equity). Hali kadhalika kwa<br />
kushirikiana na Halmashauri na wadau wengine Wizara itaendelea kutafuta ufumbuzi wa<br />
mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro sugu ya ardhi na tutajielekeza katika kuziba mianya inayosababisha mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro hiyo ili<br />
isiendelee kutokea.<br />
Mheshimiwa Spika, kwa hali hiyo Wizara yangu imejipanga kuhakiki, kupanga matumizi ya<br />
ardhi, kupima, kusajili na kutoa hati katika maeneo hayo ili kuwezesha kuwepo kwa usalama wa<br />
milki na hivyo kuondoa mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro kati ya watumiaji mbalimbali wa ardhi. Natoa rai kwa mamlaka<br />
na asasi mbalimbali kutoa ushirikiano unaotakiwa kuhakikisha kuwa ardhi inaziwezesha sekta zote<br />
kwa len<strong>go</strong> la kuwaondolea wananchi umaskini. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, maombi ya fedha kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu imejipanga<br />
kutekeleza majukumu yake iliyojiwekea ili kufikia malen<strong>go</strong> ya MKUKUTA II, Dira ya Taifa ya 2025 na<br />
36