Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
MHE. EUGEN E. MWAIPOSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kipekee kwa kunipa<br />
nafasi ili niweze kuchangia hoja ambayo iko mbele yetu. Lakini pia, niungane na wenzangu<br />
ambao wamekwishatangulia kuchangia kumpongeza Waziri, Naibu Waziri, watendaji wa Serikali<br />
pamoja na Serikali kwa kuleta hoja hii ambayo imenipa fursa kuchangia mambo mbalimbali hasa<br />
yanayohusu Jimbo la Ukonga.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi zangu hizo, nianze kwa kusema kwamba<br />
sitaunga mkono hoja hii. Kwanza, naomba nianze kwa kuzungumzia matatizo ambayo yanahusu<br />
suala zima la kutathmini, suala la malipo ya fidia na suala la mahali wanapopelekwa watu hao<br />
ambao wanalipwa fidia na kuhamishwa katika maeneo yao.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kutathmini limekuwa linaleta m<strong>go</strong><strong>go</strong>ro mkubwa katika<br />
sehemu mbili. Sehemu ya kwanza, ni maeneo ambayo yanatathminiwa kutokupewa haki<br />
kufuatana na jinsi ambavyo Sheria ya Ardhi ya mwaka 1999 inavyosema kwamba,<br />
wanapotathmini wanatakiwa watathmini kwa hali halisi ya soko jinsi ilivyo (market value).<br />
Wananchi wamekuwa wakilalamika mara nyingi kwa sababu ya kupewa fedha kido<strong>go</strong><br />
kulinganisha na mali zao walizonazo katika eneo husika, lakini pia hata mazao waliyonayo mahali<br />
hapo wanapohamishwa.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika eneo la pili ni wananchi ambao wanafanyiwa<br />
tathmini na wanaachwa mahali pale kwa kipindi kirefu. Nitoe mfano halisi, wapo wananchi<br />
wanaoishi Kipunguni A. Wananchi wale walifanyiwa tathmini kuanzia mwaka 1977. Ni miaka<br />
takriban 34 sasa, ni miezi takribani 420 na kitu. Mpaka sasa wananchi wale wanaishi sehemu ile<br />
kama vile wafungwa, hawaruhusiwi kujenga, kuendeleza sehemu zile, hawaruhusiwi kwenda<br />
kuomba kibali cha ardhi ambacho kingewasaidia sana kwa ajili ya kutumika ili kukopea na<br />
kuendeleza maisha yao. Mpaka sasa miaka hiyo 34 wako kama vile wako kifun<strong>go</strong>ni. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka 34 ni mingi. Hata kama ni mtoto ni kwamba, amezaliwa na<br />
amezaa na akizaa kama mtoto wake ni mtundu, ana wajukuu tayari. Ni kipindi kirefu sana. Kwa<br />
hiyo, namwomba sana Mheshimiwa Waziri kwa kupitia wewe Mwenyekiti, aliangalie upya suala hili<br />
la kutathmini ili wananchi waweze kupata haki zao.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na hilo, liko suala zima la kulipwa fidia ambalo<br />
wananchi wengi wamelipwa kiwan<strong>go</strong> kido<strong>go</strong> na wameshindwa kulipwa kufuatana na Sheria ile<br />
kiasi kwamba kama wakija sasa Serikali kuja kulipa, wanalipa kwa value ya wakati ule ya mwaka<br />
1977 walipotathmini, wakati ambapo Sheria ya Ardhi inasema kwamba wanatakiwa waende<br />
wakatathmini na baada ya miezi sita wanatakiwa wawalipe wananchi hawa. Vinginevyo,<br />
wanatakiwa walipe asilimia sita kwa kila mwezi ambao unapita. Kwa hiyo, naomba sana kama<br />
zoezi hilo litafanyika, basi wananchi wale walipwe asilimia sita ya market value ya pale walipo kwa<br />
miezi hiyo 428.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la sehemu wanakopelekwa wananchi hao. Ni<br />
kawaida kabisa kwamba Serikali inahitaji maeneo ya wananchi walioko karibu na mjini kwa ajili ya<br />
maendeleo. Lakini cha kushangaza, hawaandai miundombinu mizuri ili wananchi wale wakaishi<br />
mahali ambapo angalau panafanana na mahali pale walipotoka. Kwa mfano, wapo wananchi<br />
ambao walihamishwa kutoka Kipawa, wengine Kigilagila, wananchi wale walikwenda kutupwa<br />
katika sehemu ya Pugu Kinyerezi. Kule hakuna maji, hakuna barabara, hakuna shule, hakuna afya<br />
na mambo kama hayo.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaambie kwamba niliwahi kutembelea shule moja ya Kimwani<br />
kule, shule ile ilikuwa na wanafunzi 900 lakini ina madawati 60 tu. Ni kwa sababu ya ongezeko la<br />
ghafla la wananchi waliohamia sehemu ile ambao walihama na watoto wao, kwa hiyo<br />
wakaenda kujijaza kwenye ile shule. Kwa hiyo, naomba sana Serikali iangalie ni namna gani<br />
inaweza ikaanza kutengeneza mazingira ya miundombinu kabla haijawahamishia wananchi<br />
wake.<br />
Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite sasa katika suala zima la mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya mipaka. Katika<br />
Wilaya ya Ilala tunayo mipaka ambayo imetuletea matatizo makubwa, lakini cha kushangaza ni<br />
kwamba Wizara ya Ardhi imekaa kimya. Upo m<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ambao ni wa miaka mingi sana ambao<br />
76