28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

MHE. EUGEN E. MWAIPOSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kipekee kwa kunipa<br />

nafasi ili niweze kuchangia hoja ambayo iko mbele yetu. Lakini pia, niungane na wenzangu<br />

ambao wamekwishatangulia kuchangia kumpongeza Waziri, Naibu Waziri, watendaji wa Serikali<br />

pamoja na Serikali kwa kuleta hoja hii ambayo imenipa fursa kuchangia mambo mbalimbali hasa<br />

yanayohusu Jimbo la Ukonga.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi zangu hizo, nianze kwa kusema kwamba<br />

sitaunga mkono hoja hii. Kwanza, naomba nianze kwa kuzungumzia matatizo ambayo yanahusu<br />

suala zima la kutathmini, suala la malipo ya fidia na suala la mahali wanapopelekwa watu hao<br />

ambao wanalipwa fidia na kuhamishwa katika maeneo yao.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kutathmini limekuwa linaleta m<strong>go</strong><strong>go</strong>ro mkubwa katika<br />

sehemu mbili. Sehemu ya kwanza, ni maeneo ambayo yanatathminiwa kutokupewa haki<br />

kufuatana na jinsi ambavyo Sheria ya Ardhi ya mwaka 1999 inavyosema kwamba,<br />

wanapotathmini wanatakiwa watathmini kwa hali halisi ya soko jinsi ilivyo (market value).<br />

Wananchi wamekuwa wakilalamika mara nyingi kwa sababu ya kupewa fedha kido<strong>go</strong><br />

kulinganisha na mali zao walizonazo katika eneo husika, lakini pia hata mazao waliyonayo mahali<br />

hapo wanapohamishwa.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika eneo la pili ni wananchi ambao wanafanyiwa<br />

tathmini na wanaachwa mahali pale kwa kipindi kirefu. Nitoe mfano halisi, wapo wananchi<br />

wanaoishi Kipunguni A. Wananchi wale walifanyiwa tathmini kuanzia mwaka 1977. Ni miaka<br />

takriban 34 sasa, ni miezi takribani 420 na kitu. Mpaka sasa wananchi wale wanaishi sehemu ile<br />

kama vile wafungwa, hawaruhusiwi kujenga, kuendeleza sehemu zile, hawaruhusiwi kwenda<br />

kuomba kibali cha ardhi ambacho kingewasaidia sana kwa ajili ya kutumika ili kukopea na<br />

kuendeleza maisha yao. Mpaka sasa miaka hiyo 34 wako kama vile wako kifun<strong>go</strong>ni. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka 34 ni mingi. Hata kama ni mtoto ni kwamba, amezaliwa na<br />

amezaa na akizaa kama mtoto wake ni mtundu, ana wajukuu tayari. Ni kipindi kirefu sana. Kwa<br />

hiyo, namwomba sana Mheshimiwa Waziri kwa kupitia wewe Mwenyekiti, aliangalie upya suala hili<br />

la kutathmini ili wananchi waweze kupata haki zao.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamoja na hilo, liko suala zima la kulipwa fidia ambalo<br />

wananchi wengi wamelipwa kiwan<strong>go</strong> kido<strong>go</strong> na wameshindwa kulipwa kufuatana na Sheria ile<br />

kiasi kwamba kama wakija sasa Serikali kuja kulipa, wanalipa kwa value ya wakati ule ya mwaka<br />

1977 walipotathmini, wakati ambapo Sheria ya Ardhi inasema kwamba wanatakiwa waende<br />

wakatathmini na baada ya miezi sita wanatakiwa wawalipe wananchi hawa. Vinginevyo,<br />

wanatakiwa walipe asilimia sita kwa kila mwezi ambao unapita. Kwa hiyo, naomba sana kama<br />

zoezi hilo litafanyika, basi wananchi wale walipwe asilimia sita ya market value ya pale walipo kwa<br />

miezi hiyo 428.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la sehemu wanakopelekwa wananchi hao. Ni<br />

kawaida kabisa kwamba Serikali inahitaji maeneo ya wananchi walioko karibu na mjini kwa ajili ya<br />

maendeleo. Lakini cha kushangaza, hawaandai miundombinu mizuri ili wananchi wale wakaishi<br />

mahali ambapo angalau panafanana na mahali pale walipotoka. Kwa mfano, wapo wananchi<br />

ambao walihamishwa kutoka Kipawa, wengine Kigilagila, wananchi wale walikwenda kutupwa<br />

katika sehemu ya Pugu Kinyerezi. Kule hakuna maji, hakuna barabara, hakuna shule, hakuna afya<br />

na mambo kama hayo.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaambie kwamba niliwahi kutembelea shule moja ya Kimwani<br />

kule, shule ile ilikuwa na wanafunzi 900 lakini ina madawati 60 tu. Ni kwa sababu ya ongezeko la<br />

ghafla la wananchi waliohamia sehemu ile ambao walihama na watoto wao, kwa hiyo<br />

wakaenda kujijaza kwenye ile shule. Kwa hiyo, naomba sana Serikali iangalie ni namna gani<br />

inaweza ikaanza kutengeneza mazingira ya miundombinu kabla haijawahamishia wananchi<br />

wake.<br />

Mheshimiwa Mwenyekiti, nijikite sasa katika suala zima la mi<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ya mipaka. Katika<br />

Wilaya ya Ilala tunayo mipaka ambayo imetuletea matatizo makubwa, lakini cha kushangaza ni<br />

kwamba Wizara ya Ardhi imekaa kimya. Upo m<strong>go</strong><strong>go</strong>ro ambao ni wa miaka mingi sana ambao<br />

76

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!