28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika,<br />

makubaliano kati ya Kampuni ya Mawasiliano na mwenye ardhi ni mkataba wa watu wawili na<br />

wanapoingia wote wanasaini mbele ya watu ambao wanashuhuidia. Kwa hiyo, namwomba tu<br />

Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> pamoja na Watanzania kwamba wawe makini sana wanapoingia mikataba<br />

na makampuni hayo ili kuhakikisha kwamba pale ambapo malipo yanachelewa, basi kuwe na<br />

close ya penalty kama mtu atachelewa kulipa aweze kulipa na riba kido<strong>go</strong>.<br />

Na. 418<br />

Mashamba ya NAFCO Mbarali na NAFCO Kapunga<br />

MHE. MODESTUS D. KILUFI aliuliza:-<br />

Mashamba ya NAFCO Mbarali na NAFCO Kapunga yamepewa wawekezaji: Je, Serikali<br />

itawasaidiaje wakulima wado<strong>go</strong> wado<strong>go</strong> wanaozunguka mashamba hayo ambao awali waliishi<br />

ndani ya mashamba hayo na kuwasaidia na wale wa nje<br />

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu:-<br />

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, napenda kujibu<br />

swali la Mheshimiwa Modestus D. Kilufi, M<strong>bunge</strong> wa Mbarali, kama ifuatavyo:-<br />

Mheshimiwa Spika, shamba la Mpunga la Mbarali lililokuwa la NAFCO lilibinafsishwa kwa<br />

Kampuni ya Highland Estate Ltd, tarehe 18 A<strong>go</strong>sti, 2006. Shamba la Mpunga la Kapunga<br />

lilibinafsishwa kwa kampuni ya Export Trading Company Ltd, tarehe 13 Septemba, 2006. Tangu<br />

kubinafsishwa kwa mashamba hayo, kumekuwa na mi<strong>go</strong>ngano kati ya wawekezaji na wakulima<br />

wado<strong>go</strong> ambao kabla mashamba hayajabinafsishwa walikuwa wanalima kwa kujikimu maeneo<br />

ambayo NAFCO haikuweza kuyalima. Mi<strong>go</strong>ngano inayojitokeza mara kwa mara katika matumizi<br />

ya maji ya kumwagilia mashamba na maeneo ya kulima (Mashamba) ni kwa sababu ya matatizo<br />

ya uhusiano.<br />

Mheshimiwa Spika, wananchi wanaoishi katika maeneo yanayozunguka mashamba<br />

yaliyobinafsishwa wana mchan<strong>go</strong> mkubwa katika kusaidiana na mwekezaji kuhakikisha kwamba<br />

mashamba yote yanalimwa na kuzalisha chakula kama ilivyopangwa. Aidha, wananchi hao pia<br />

wanayo nafasi ya kupata ajira au hata kuzalisha mpunga kwa mkataba maalum.<br />

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha kwamba wananchi wanamiliki mashamba yao nje ya<br />

mashamba yaliyobinafsishwa, Serikali inaendelea kuchukua hatua za kuboresha miundombinu ya<br />

umwagiliaji katika maeneo yanayozunguka mashamba yaliyobinafsishwa. Kwa mfano, katika<br />

mwaka 2011/2012, Serikali imetenga Shilingi milioni 500 ili kujenga banio la umwagiliaji katika Kijiji<br />

cha Mwendamtitu huko Mbarali. Aidha, tarehe 4 A<strong>go</strong>sti, 2011, Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na<br />

Ushirika alifanya ziara katika mashamba ya Kapunga na Mbarali na kumwagiza Mhandisi wa<br />

Umwagiliaji wa Kanda ya Mbeya kukagua maeneo yaliyopendekezwa na wananchi kuendelezwa<br />

kwa kilimo cha umwagiliaji huko Kapunga ili Serikali itafute fedha za kuyaendeleza. Mhandisi<br />

anaendelea kufanya uchunguzi wa kitaalamu.<br />

Namwomba Mheshimiwa Kilufi na wananchi wa Mbarali na Kapunga kuwa na subira<br />

wakati Serikali inaandaa miradi ya kuwasaidia wakulima.<br />

MHE. MODESTUS D. KILUFI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa<br />

Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwa vile wananchi wa Kapunga ambao sasa<br />

hivi ni Kata mbili, Chimala na Kitamboleo walikuwa wanategemea sana eneo hilo na sasa tayari<br />

liko chini ya mwekezaji, na eneo ambalo wanaliomba liendelezwe ni eneo la Mpunga Mmoja<br />

ambalo lina hekta zaidi ya 4,000 pamoja na eneo la Mwashikamile na Iyala:-<br />

(i) Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kuona kwamba wananchi hawa wanaondokana<br />

na adha hiyo, na hivyo maeneo yanaboreshwa ili yaweze kulimwa na wananchi hao<br />

5

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!