28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

MHE. YAHYA KASSIM ISSA: Mheshimiwa Spika, ya kwako. (Kicheko)<br />

SPIKA: Mheshimiwa M<strong>bunge</strong>, naomba ukae kwanza. Nimemjibu yule aliyeomba<br />

mwon<strong>go</strong>zo. Sasa haiwezi kuwa mwon<strong>go</strong>zo juu ya mwon<strong>go</strong>zo. Sasa tunaendelea.<br />

HOJA ZA SERIKALI<br />

Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi<br />

kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012<br />

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba<br />

kutoa hoja kwamba kutokana na taarifa iliyowasilishwa leo ndani ya Bunge lako Tukufu na<br />

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, Bunge lako lipokee<br />

na kujadili makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya<br />

Makazi kwa mwaka 2011/2012.<br />

Mheshimiwa Spika, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha sisi sote<br />

kuwa Wa<strong>bunge</strong> wa Bunge lako Tukufu. Naomba nichukue fursa hii kumpongeza Rais - Mheshimiwa<br />

Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania<br />

kwa kipindi chake cha pili na Mheshimiwa Dkt. Mohammed Gharib Bilal kuwa Makamu wa Rais;<br />

Mheshimiwa Dkt. Ali Mohammed Shein kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa<br />

Baraza la Mapinduzi; na Mheshimiwa Mizen<strong>go</strong> Kayanza Peter Pinda - M<strong>bunge</strong> wa Katavi, kwa<br />

kuteuliwa na Mheshimiwa Rais na kupitishwa na Bunge kuwa Waziri Mkuu.<br />

Aidha, ninamshukuru Mheshimiwa Rais kwa dhamana kubwa aliyonipa kwa kuniteua kuwa<br />

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Sekta ambayo nilibahatika kuishughulikia kwa<br />

miaka ipatayo kumi nikiwa Katibu Msaidizi Mkuu (UN Under-Secretary General) na Mkurugenzi<br />

Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi (UN-Habitat). Namshukuru Mheshimiwa Rais<br />

kwa kunipa nafasi ya kutumia uzoefu nilioupata huko kutumikia nchi yangu. Naahidi kwamba kwa<br />

baraka za Mwenyenzi Mungu nitafanya kila linalowezekana kufikia matarajio yake na ya<br />

wananchi wote kwa ujumla. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa mara nyingine tena nakupongeza sana kwa kujenga historia ya<br />

nchi yetu kwa kuwa Spika wa kwanza mwanamke wa Bunge hili Tukufu. Nakupongeza kwa<br />

umahiri na umakini ambao tayari umeonyesha katika kuon<strong>go</strong>za shughuli za Bunge. Hongera sana,<br />

na Mwenyezi Mungu aendelee kukuon<strong>go</strong>za na kukupa hekima. Aidha, nampongeza Mheshimiwa<br />

Job Yustino Ndugai - M<strong>bunge</strong> wa Kongwa, kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika. Pia<br />

nawapongeza Waheshimiwa Jenista Joakim Mhagama - M<strong>bunge</strong> wa Peramiho, Sylivester Massele<br />

Mabumba - M<strong>bunge</strong> wa Dole, na George Boniface Simbachawene - M<strong>bunge</strong> wa Kibakwe kwa<br />

kuchaguliwa kuwa Wenyeviti wa Bunge.<br />

Mheshimiwa Spika, napenda nitumie fursa hii kuwashukuru kwa dhati wananchi wa Jimbo<br />

la Muleba Kusini kwa kunichagua bila kupingwa kuwa M<strong>bunge</strong> wao katika uchaguzi wa mkuu wa<br />

mwaka 2010 na kuniwezesha kutekeleza majukumu yangu. Aidha, nawashukuru ndugu, jamaa na<br />

marafiki walioshiriki katika kuniwezesha kurejea nyumbani kutoka Umoja wa Mataifa. Kipindi cha<br />

mpito kilikuwa kigumu kwangu na chenye hekaheka nyingi, lakini kwa msaada, imani na mapenzi<br />

waliyonipa mambo yamekwenda vizuri.<br />

Nawashukuru wananchi na ninawahakikishia popote pale mlipo, iwe Tarafa ya Nshamba,<br />

Kimwani au Muleba yenyewe, kwamba tutajifunga kibwebwe kuliendeleza Jimbo la Muleba Kusini<br />

na Wilaya ya Muleba kwa ujumla kwa ari, nguvu na kasi zaidi. Pia, napenda kutoa salamu zangu<br />

kwa Watanzania wote na kuwashukuru kwa moyo wao wa kulinda amani na utulivu katika<br />

kuendeleza demokrasia. Ni sifa ambayo imeleta heshima kubwa kwa Taifa letu. Asiwadanganye<br />

mtu, kwani kote nilikopita duniani wakati nikitumikia Umoja wa Mataifa tulitambuliwa kwa sifa hiyo.<br />

Namwomba Mwenyezi Mungu amwezeshe kila mwananchi kulitambua hili na kuchangia katika<br />

nafasi yake na kadri ya uwezo wake ili hali hiyo iendelee. (Makofi)<br />

18

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!