Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
MHE. YAHYA KASSIM ISSA: Mheshimiwa Spika, ya kwako. (Kicheko)<br />
SPIKA: Mheshimiwa M<strong>bunge</strong>, naomba ukae kwanza. Nimemjibu yule aliyeomba<br />
mwon<strong>go</strong>zo. Sasa haiwezi kuwa mwon<strong>go</strong>zo juu ya mwon<strong>go</strong>zo. Sasa tunaendelea.<br />
HOJA ZA SERIKALI<br />
Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi<br />
kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012<br />
WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba<br />
kutoa hoja kwamba kutokana na taarifa iliyowasilishwa leo ndani ya Bunge lako Tukufu na<br />
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, Bunge lako lipokee<br />
na kujadili makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya<br />
Makazi kwa mwaka 2011/2012.<br />
Mheshimiwa Spika, awali ya yote namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha sisi sote<br />
kuwa Wa<strong>bunge</strong> wa Bunge lako Tukufu. Naomba nichukue fursa hii kumpongeza Rais - Mheshimiwa<br />
Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania<br />
kwa kipindi chake cha pili na Mheshimiwa Dkt. Mohammed Gharib Bilal kuwa Makamu wa Rais;<br />
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohammed Shein kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa<br />
Baraza la Mapinduzi; na Mheshimiwa Mizen<strong>go</strong> Kayanza Peter Pinda - M<strong>bunge</strong> wa Katavi, kwa<br />
kuteuliwa na Mheshimiwa Rais na kupitishwa na Bunge kuwa Waziri Mkuu.<br />
Aidha, ninamshukuru Mheshimiwa Rais kwa dhamana kubwa aliyonipa kwa kuniteua kuwa<br />
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Sekta ambayo nilibahatika kuishughulikia kwa<br />
miaka ipatayo kumi nikiwa Katibu Msaidizi Mkuu (UN Under-Secretary General) na Mkurugenzi<br />
Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Makazi (UN-Habitat). Namshukuru Mheshimiwa Rais<br />
kwa kunipa nafasi ya kutumia uzoefu nilioupata huko kutumikia nchi yangu. Naahidi kwamba kwa<br />
baraka za Mwenyenzi Mungu nitafanya kila linalowezekana kufikia matarajio yake na ya<br />
wananchi wote kwa ujumla. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kwa mara nyingine tena nakupongeza sana kwa kujenga historia ya<br />
nchi yetu kwa kuwa Spika wa kwanza mwanamke wa Bunge hili Tukufu. Nakupongeza kwa<br />
umahiri na umakini ambao tayari umeonyesha katika kuon<strong>go</strong>za shughuli za Bunge. Hongera sana,<br />
na Mwenyezi Mungu aendelee kukuon<strong>go</strong>za na kukupa hekima. Aidha, nampongeza Mheshimiwa<br />
Job Yustino Ndugai - M<strong>bunge</strong> wa Kongwa, kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika. Pia<br />
nawapongeza Waheshimiwa Jenista Joakim Mhagama - M<strong>bunge</strong> wa Peramiho, Sylivester Massele<br />
Mabumba - M<strong>bunge</strong> wa Dole, na George Boniface Simbachawene - M<strong>bunge</strong> wa Kibakwe kwa<br />
kuchaguliwa kuwa Wenyeviti wa Bunge.<br />
Mheshimiwa Spika, napenda nitumie fursa hii kuwashukuru kwa dhati wananchi wa Jimbo<br />
la Muleba Kusini kwa kunichagua bila kupingwa kuwa M<strong>bunge</strong> wao katika uchaguzi wa mkuu wa<br />
mwaka 2010 na kuniwezesha kutekeleza majukumu yangu. Aidha, nawashukuru ndugu, jamaa na<br />
marafiki walioshiriki katika kuniwezesha kurejea nyumbani kutoka Umoja wa Mataifa. Kipindi cha<br />
mpito kilikuwa kigumu kwangu na chenye hekaheka nyingi, lakini kwa msaada, imani na mapenzi<br />
waliyonipa mambo yamekwenda vizuri.<br />
Nawashukuru wananchi na ninawahakikishia popote pale mlipo, iwe Tarafa ya Nshamba,<br />
Kimwani au Muleba yenyewe, kwamba tutajifunga kibwebwe kuliendeleza Jimbo la Muleba Kusini<br />
na Wilaya ya Muleba kwa ujumla kwa ari, nguvu na kasi zaidi. Pia, napenda kutoa salamu zangu<br />
kwa Watanzania wote na kuwashukuru kwa moyo wao wa kulinda amani na utulivu katika<br />
kuendeleza demokrasia. Ni sifa ambayo imeleta heshima kubwa kwa Taifa letu. Asiwadanganye<br />
mtu, kwani kote nilikopita duniani wakati nikitumikia Umoja wa Mataifa tulitambuliwa kwa sifa hiyo.<br />
Namwomba Mwenyezi Mungu amwezeshe kila mwananchi kulitambua hili na kuchangia katika<br />
nafasi yake na kadri ya uwezo wake ili hali hiyo iendelee. (Makofi)<br />
18