28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Pamoja na majibu ya Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi aliyoyatoa tarehe 1 Julai,<br />

2011 wakati akijibu maswali Bungeni kuhusu hatua ambazo Serikali imechukua toka mamlaka<br />

husika zilipokabidhiwa ripoti husika, Kambi ya Upinzani inataka maelezo zaidi kutoka kwa Serikali<br />

kwa kuwa mwaka mmoja umepita toka uchunguzi huo ufanyike na sehemu kubwa ya viwanja<br />

bado vipo mikononi mwa wavamizi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali ieleze, ni viwanja vingapi<br />

vimerudishwa na vingapi bado vipo mikononi mwa wavamizi Ni lini Serikali itarejesha viwanja<br />

vyote vilivyobaki kwenye matumizi yake kwa mujibu wa sheria kwa kurejea mapendekezo ya<br />

Kamati Ni hatua gani zimechukuliwa kwa wahusika Wizarani na kwenye halmashauri walioshiriki<br />

kusababisha hali hiyo ukiondoa maafisa wachache ambao wamefikishwa mahakamani kutokana<br />

na kesi ya kiwanja kimoja hivi karibuni Kwa kuwa sasa Wizara ina kada ya askari (land rangers) ni<br />

lini askari hao watatembelea maeneo yote yaliyotajwa kuvamiwa kwa mujibu wa taarifa ya<br />

Kamati ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, athari za uvamizi wa viwanja vya wazi ni kubwa katika mipan<strong>go</strong> miji na<br />

maendeleo ya wananchi kwa ujumla. Mathalani katika Manispaa ya Kinondoni kwenye kiwanja<br />

Na. 856 Msasani beach ambacho kwa mujibu wa ramani ya upimaji iliyosajiliwa namba 29331<br />

ilikuwa ni kwa matumzi ya wazi, lakini baadae kilimilikishwa kwa mtu binafsi. Athari yake ni kuzibwa<br />

kwa njia ya mkondo kuelekea baharini yamezibwa na hivyo kuleta mafuriko katika barabara na<br />

makazi ya watu wa eneo husika, hali hiyo ipo pia katika majen<strong>go</strong> ya May Fair na Markham. Kambi<br />

ya Upinzani inataka Serikali ieleze hatua zipi itachukua ili kuepusha wananchi wa maeneo ya<br />

Msasani, Mikocheni na maeneo mengine katika Jiji la Dar es Salaam yaliyojengwa majen<strong>go</strong><br />

kinyume cha sheria na mipan<strong>go</strong> miji na hivyo kuleta athari kubwa kwa maisha ya wananchi.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu sekta ya nyumba, sekta hii ni sekta pekee inayoweza kuleta na<br />

kutekelezwa kwa dhana nzima ya maisha bora kwa kila Mtanzania. Nchi yetu na Watanzania kwa<br />

ujumla bado tuna matatizo makubwa ya nyumba bora na za bei nafuu kutokana na bei kubwa<br />

ya cement na bati bidhaa muhimu katika kutimiza azma ya ujenzi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, tulisema na tunasema kuwa bei ya simenti na bati inaweza kuwa chini<br />

ya shilingi 7,000/=, kama Serikali itakuwa na utashi wa kuwahudumia wananchi kwa dhati, wakati<br />

ukinunua simenti Uturuki na Pakistan ukinunua tani 600,000 bei ya tani moja ni dola za Marekani 70<br />

hadi bandarini. Guangzhou, China tani moja ni dola za Marekani 26. Kwa hesabu za kawaida kwa<br />

mfuko mmoja ni dola 3.5 sawa na shilingi 5,250 kama ukinunua Pakstan au Uturuki, ukinunua China<br />

bei itakuwa dola 1.3. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani bado inasisitiza kuwa kama Serikali inadhamira ya<br />

kweli mfuko wa simenti hauwezi kuuzwa zaidi ya shilingi 7,500. Hivyo basi tunaitaka Serikali itueleze<br />

kwa nini bei ya simenti inauzwa zaidi ya shilingi 14,000 kwa Dar es Salaam na kwa nje ya Dar es<br />

Salaam bei ni zaidi ya hapo, wakati malighafi zinapatikana hapa hapa nchini na kiwanda kikubwa<br />

cha simenti kinatumia gesi asili ili kupunguza gharama za umeme. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza gharama hizi na ni faida kiasi<br />

katika kodi tunayopata kwa kuwalangua Watanzania Serikali haioni kwamba ina wajibu wa<br />

kuondoa hizi kero wananchi wajenge nyumba bora na kwa bei nafuu (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lilipoanzishwa mwaka 1962, moja kati<br />

malen<strong>go</strong> yake ilikuwa ni kujenga nyumba za bei nafuu kwa ajili ya Watanzania wafanyao kazi<br />

mijini. Hata hivyo kwa kadri siku zilivyosonga mbele, shirika hili liligeuka kutoka kuwahudumia<br />

masikini na watu wenye kipato cha kati na badala yake kuwahudumia watu wa kipato cha juu.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Shirika la Nyumba la Taifa linahudumia asilimia 0.5 tu ya Watanzania<br />

wote wa nchi hii, swali la msingi ni je, Serikali imeweka mikakati gani ya kuhakikisha kuwa shirika hili<br />

linahudumia Watanzania wengi zaidi kwa kuwapatia nyumba za bei nafuu.<br />

52

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!