28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Mheshimiwa Spika, tulikwenda na Waziri Mkuu tarehe 14/3/2009, Waziri Mkuu akaagiza na<br />

anayo haki ya kuagiza kwamba jamani eeh, walipeni hawa wananchi haraka na jamaa wa<br />

Mabwawani pale ambao mwanzo walilipwa ukiondoa hawa ambao hawajalipwa kabisa lakini<br />

ukiambiwa malipo yenyewe ni vichekesho kwani mtu mwenye msingi kalipwa shilingi 300,000/=,<br />

mwenye nyumba kalipwa shilingi 1,800,000/= mpaka shilingi 4,000,000/= ambayo kwa kweli siyo<br />

haki, hazitoshi. Rais aliagiza tarehe 27/10/2010 kwamba walipeni wananchi wa Kurasini lakini<br />

mpaka leo wananchi wale hawajalipwa. Waziri mhusika alikwenda akakutana na wananchi na<br />

akasikitika sana na akawaambia anaharakisha kuwalipa lakini mimi nataka kusema ukweli kabisa<br />

kwamba Waziri hana tatizo wala Naibu Waziri hana tatizo lakini kilio cha wananchi wa Kurasini ni<br />

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, hata lile eneo la mradi hajafika, tofauti na Mama Salome<br />

Sijaona. Ni tatizo kwelikweli, si vema kusema watu lakini niseme ukweli Katibu Mkuu, huyu Bwana<br />

Mkubwa kama ataendelea na Mama Tibaijuka kazi yote nzuri anayofanya Mama Tibaijuka<br />

itakuwa ni bure.<br />

Mheshimiwa Spika, tumeambiwa mpan<strong>go</strong> mzuri wa National Housing, kwanza nipongeze<br />

uon<strong>go</strong>zi wa National Housing. Vijana wana uwezo na ni wachapakazi ukiondoa wale wazee wa<br />

zamani akina Komba, Malisa na Zedieli, lakini ndiyo waliofanya mambo yote makubwa. Yale<br />

maghorofa mazuri tunayoona Dar es Salaam, walikuwa wazee hawa nao walikuwa wachapakazi,<br />

wana nguvu na uwezo kwa hiyo wanashindana.<br />

Mheshimiwa Spika, nachosema ni lazima maamuzi ya Bunge yaheshimike, tuliamua<br />

kwenye Bunge hilihili mwaka 2009/2010 na mwaka 2010/2011 na kitabu kiko hapa kwamba baadhi<br />

ya nyumba za National Housing mfano nyumba za Keko, Chang’ombe mafleti na mimi ni mkazi<br />

wa pale, Block No.1, niseme mapema Mheshimiwa Spika usikie, Tandika Maghorofani, Ilala Kota,<br />

Mafleti ya Breweries, Flats za Ubun<strong>go</strong> na nyingine nyingi Tanzania tulisema tutawauzia wananchi<br />

walioishi mle kwa muda mrefu ili na wao waweze kujikimu. Mambo ya kushangaza leo mpan<strong>go</strong> ule<br />

umekufa kabisa lakini sasa sijui kama Mheshimiwa Waziri wamepitia vitabu vya nyuma wakaona<br />

maamuzi ya Bunge au wameisikiliza tu Management na Board ya National Housing Mimi<br />

nawaomba sana wapitie vitabu vya nyuma waangalie maamuzi ya Bunge, leo tulikuwa<br />

tunatarajia nyumba zile tutakuwa tumeshawakabidhi wananchi.<br />

Mheshimiwa Spika, kengele ya pili inaweza ikanililia basi niseme tu mapema bajeti hii mimi<br />

siiungi mkono mpaka niambiwe wananchi wa Kurasini wanalipwa lini na wananchi wa<br />

Maghorofani na nyumba zote za National Tanzania tulizosema na tusione haya katika hili, mbona<br />

yale majumba mazuri tuliuziana Kuwauzia hawa wananchi tunasita nini<br />

Mheshimiwa Spika, naamini leo nimeongea sauti ya chini na Mama mahali alipo moyo<br />

hautakwenda juu, siungi mkono hoja hii mpaka nipate majibu ya watu wa Kurasini na watu wa<br />

Maghorofa na wale wengine wenye nyumba ndo<strong>go</strong>ndo<strong>go</strong>. Haiwezekani Mheshimiwa Waziri,<br />

akisimama hapa atamke kwamba mradi huu hauwezekani, wananchi waendelee kujenga<br />

nyumba zao. Hata wale watu walionunua vile viwanja wako akina Camel Oil na Oil Com, vile<br />

viwanja vya mwanzo hamjawapa hati zao wala hamjawakabidhi mali yao, sasa sijui vipi. Hawa<br />

waliouza hamjawapa pesa zao wale walionunua hamjawapa hati zao, sasa sijui tunakwendaje<br />

Mheshimiwa Spika, leo mmeleta bajeti nzuri, kitabu hiki kido<strong>go</strong>, tulikuwa tunauliza kitabu<br />

kido<strong>go</strong>do<strong>go</strong> hiki ndiyo kimejaa mambo yote ya shida za ardhi ya nchi hii Tunasema<br />

kinatosheleza, kina maneno mazuri lakini hofu yangu pamoja na kwamba asili yangu ni Temeke<br />

lakini asili yangu ni Ilala pia Kigamboni kunanihusu. Yule Bi. Siti, Baba yake Chekimea alipotoka<br />

Tunduru alifikia Tuan<strong>go</strong>ma ndipo alipomkuta yule Mama wa Kizaramo, Mama yao Bi. Siti. Kwa hiyo,<br />

napata hofu sana na huu mradi wa Kigamboni kama utafanikiwa. Kama hawawezi tusiwasumbue<br />

wananchi tena. Hofu yangu tunaweza sasa hivi tukauchangamkia ikiisha Awamu ya Nne na mradi<br />

huu umeondoka. Kwa hiyo, tuwaambie wananchi ukweli.<br />

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, nisije nikapigiwa kengele ya pili lakini siungi mkono<br />

mpaka nipate majibu. (Makofi)<br />

61

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!