28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

sehemu ambayo inaishi familia moja kwa sasa, ikiendelezwa vizuri zinaweza kuishi familia kati ya<br />

100 hadi 150. Kamati inapenda kusisitiza kuwa baada ya maeneo hayo kuendelezwa, ni vyema<br />

kipaumbele cha kuuziwa au kupangishwa kikatolewa kwanza kwa watu/familia zilizokuwa zinaishi<br />

katika maeneo hayo. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, mwisho katika shukrani zangu, lakini kwa umuhimu mkubwa,<br />

nakushukuru wewe Mheshimiwa Spika, Naibu Spika na Wenyeviti wote wa Bunge kwa kazi kubwa<br />

mnayoifanya ya kulion<strong>go</strong>za Bunge hili. Mungu awajalie afya njema, hekima na busara katika<br />

kutekeleza wajibu huu mkubwa mliokabidhiwa na Watanzania. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya wanakamati wenzangu napenda kuchukua nafasi hii<br />

kumshukuru Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mheshimiwa Profesa Anna<br />

Tibaijuka, Naibu Waziri Mheshimiwa Goodluck Ole-Medeye, Katibu Mkuu Ndugu Patrick<br />

Rutabanzibwa pamoja na wataalam wote wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya<br />

Makazi pamoja na Taasisi na Mashirika yanayofanya kazi chini ya Wizara hii kwa maelezo ya<br />

ufafanuzi walioutoa mbele ya Kamati wakati wa kuchambua Bajeti ya Wizara. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, naomba pia niwashukuru Wajumbe wenzangu wa Kamati kwa<br />

ushirikiano wao walionipa wakati wa kuchambua Mpan<strong>go</strong> na Makadirio ya Bajeti ya Wizara hii na<br />

hivyo kufanikisha taarifa hii ambayo kwa niaba yao naiwasilisha leo katika Bunge lako. Naomba<br />

niwatambue kwa kuwataja majina kama ifuatavyo:-<br />

Mheshimiwa James Lembeli, Mwenyekiti, Mheshimiwa Abdulkarim Shah, Makamu<br />

Mwenyekiti na wajumbe ambao ni Mheshimiwa Zakia Meghji, Mheshimiwa Saleh Pamba,<br />

Mheshimiwa Philemon Ndesamburo, Mheshimiwa Kheri Khatib Ameir, Mheshimiwa Benardetha<br />

Mushashu, Mheshimiwa Mariam Mfaki, Mheshimiwa Ali khamis Seif, Mheshimiwa Susan Lyimo,<br />

Mheshimiwa Jaku Hashim Ayoub, Mheshimiwa Mariam Kasembe, Mheshimiwa Silvestry Koka,<br />

Mheshimiwa Josephat Kandege, Mheshimiwa Magdalena Sakaya, Mheshimiwa Dkt. Charles<br />

Tizeba, Mheshimiwa Amina Andrew Clement, Mheshimiwa Michael Laizer, Mheshimiwa Kaika<br />

Telele, Mheshimiwa Lediana Mng’ong’o, Mheshimiwa Meshack Opulukwa, Mheshimiwa Mchungaji<br />

Peter Msigwa, Mheshimiwa Mwanakhamis Kassim Said, Mheshimiwa Engineer Hamad Yussuf<br />

Masauni, Mheshimiwa Al-Shymaa Kwegyir, Mheshimiwa Elizabeth Batenga, Mheshimiwa Abdalla<br />

Haji Ali na mimi mwenyewe Dkt. Mary Mwanjelwa. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii pia kumshukuru Katibu wa Bunge Dkt. Thomas<br />

Didimu Kashilillah, Katibu wa Kamati Ndugu Rachel Nyega kwa kuihudumia Kamati ipasavyo na<br />

kufanikisha maandalizi ya taarifa hii kwa wakati. Aidha, nawashukuru watendaji wote wa Ofisi ya<br />

Bunge kwa ushirikiano wao mzuri wa kuiwezesha Kamati kutekeleza majukumu yake kwa ukamilifu.<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na<br />

Mazingira naomba kuwasilisha na ninaunga mkono hoja. (Makofi)<br />

MHE. HALIMA J. MDEE – MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI KWA WIZARA YA ARDHI,<br />

NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, napenda kuchukua nafasi hii<br />

kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuwepo hapa leo kuwasilisha maoni ya Kambi ya<br />

Upinzani kuhusu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, pia nikushukuru wewe kwa kuniruhusu kutoa maoni ya Kambi ya<br />

Upinzani kuhusu Wizara hii kwa mujibu wa Kanuni ya 99(7) Kanuni za Bunge Toleo la mwaka<br />

2007. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, pili ningependa kutoa shukrani zangu za dhati kwa Chama cha<br />

Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na wananchi wa Jimbo la Kawe kwa imani yao kwangu,<br />

makamanda wote (vijana, wazee na akina mama wa vyama vyote) walioshiriki katika harakati<br />

zangu zote za Kampeni na hatimaye kukesha na m<strong>go</strong>mbea wao, Shule ya Msingi Oysterbay<br />

kulinda ushindi wetu. Mungu pekee ndiye anayejua shukrani yangu kwao! Ahadi yangu kwao ni<br />

kuwatumikia kwa uwezo wangu wote kwa kadri Mwenyezi Mungu atakavyoniwezesha! (Makofi)<br />

42

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!