28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

ya mafuta hasa kwa sababu bei yenyewe ni elekezi kwa kila sehemu ya Tanzania. Bei elekezi ni<br />

tofauti kwa Mwanza na ni tofauti kwa Dar es Salaam. Kwa hiyo, naomba ...<br />

WABUNGE FULANI: Aaah!<br />

SPIKA: Hamna. Hilo ni jibu. Kwa nini nyie mnabisha<br />

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa<br />

M<strong>bunge</strong> atuletee baadaye, tumpe bei elekezi kwa maeneo yote ya Tanzania.<br />

SPIKA: Sawa. Ni jibu sahihi kabisa.<br />

Na. 422<br />

Umuhimu wa Nishati ya Gesi Asilia Katika Kuzalisha Umeme<br />

MHE. YUSUPH A. NASSIR aliuliza:-<br />

Raslimali ya nishati ya gesi asilia ni chanzo muhimu na mahsusi cha kuzalisha umeme,<br />

ikiwemo ile ya Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong> na Mnazibay:-<br />

(a)<br />

(b)<br />

(c)<br />

Je, ni lini vyanzo vingine vilivyopo vitatumika ili kuongeza uzalishaji umeme kwenye<br />

gridi ya Taifa<br />

Je, Serikali haioni umuhimu wa kujihusisha moja kwa moja na ujenzi wa miradi hiyo<br />

ili mapungufu yaliyotokea katika ujenzi wa mradi wa Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong> yasije kujirudia<br />

Je, ni lini Mikataba ya Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong> na uhalali wa uwepo wa PAE kwenye sekta<br />

ya gesi asilia utaangaliwa upya ukizingatia hali halisi ya yaliyojitokeza<br />

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-<br />

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la<br />

Mheshimiwa Yusuph Abdallah Nassir, M<strong>bunge</strong> wa Korogwe Mjini, lenye vipengele (a), (b) na (c)<br />

kama ifuatavyo:-<br />

(a) Mheshimiwa Spika, kwa sasa jumla ya umeme unaotokana na raslimali yetu ya<br />

Gesi Asilia ni MW 400 zinazozalishwa Dar es Salaam kutokea kwenye chanzo cha Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong><br />

Kilwa, MW 7.5 zinazozalishwa kwenye Kituo cha Somanga Fungu, Kilwa kwa gesi inayotoka kwa ajili<br />

ya Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong>, na MW 18 zinazozalishwa kwenye kituo cha umeme Mtwara, kwa gesi<br />

inayotokana Mnazibay kufanya jumla ya MW 425.5 zinazoingia katika mfumo wa umeme wa Taifa.<br />

Mheshimiwa Spika, ili vyanzo hivi vipya vya gesi asili viweze kutumika kukidhi mahitaji ya<br />

gesi asilia yanayozidi kuongezeka TPDC kwa kushirikiana na Makampuni yanayohusika (Maurel<br />

and Prom, Ndovu Resources, na BG) yamejipanga kuchimba visima zaidi ili kubaini kiasi cha gesi<br />

kilichopo. Kazi hii itafuatiwa na shughuli za kuendeleza vyanzo hivyo kwa ajili ya matumizi<br />

mbalimbali zikiwemo kukamilisha bomba la gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es Salaam ifikapo<br />

Desemba, 2013, kuzalisha umeme, matumizi ya gesi viwandani, na pia katika sekta nyingine za<br />

uchumi. Aidha, miradi mbalimbali ya kuzalisha umeme kutokana na vyanzo vingine kama vile<br />

makaa ya mawe, maji na upepo vinaendelezwa.<br />

(b) Mheshimiwa Spika, hivi sasa Serikali kwa kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli<br />

TPDC iko katika mchakato wa maandalizi ya ujenzi wa awamu ya kwanza ya bomba la kusafirisha<br />

gesi asili kutoka Mnazi Bay hadi Dar es Salaam kupitia Somanga Fungu – Kilwa. Maoni ya<br />

Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> ndiyo msimamo wa sasa kwenda mbele, wa Serikali kuhusiana na miradi hii<br />

nyeti ya miundombinu. Uwekezaji na umiliki wa miundombinu hii ya gesi asili itakuwa chini ya<br />

Serikali ili kupunguza ukiritimba unaoweza kutokea kwa miundombinu kama hii kumilikiwa na<br />

makampuni binafsi.<br />

12

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!