Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
ya mafuta hasa kwa sababu bei yenyewe ni elekezi kwa kila sehemu ya Tanzania. Bei elekezi ni<br />
tofauti kwa Mwanza na ni tofauti kwa Dar es Salaam. Kwa hiyo, naomba ...<br />
WABUNGE FULANI: Aaah!<br />
SPIKA: Hamna. Hilo ni jibu. Kwa nini nyie mnabisha<br />
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa<br />
M<strong>bunge</strong> atuletee baadaye, tumpe bei elekezi kwa maeneo yote ya Tanzania.<br />
SPIKA: Sawa. Ni jibu sahihi kabisa.<br />
Na. 422<br />
Umuhimu wa Nishati ya Gesi Asilia Katika Kuzalisha Umeme<br />
MHE. YUSUPH A. NASSIR aliuliza:-<br />
Raslimali ya nishati ya gesi asilia ni chanzo muhimu na mahsusi cha kuzalisha umeme,<br />
ikiwemo ile ya Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong> na Mnazibay:-<br />
(a)<br />
(b)<br />
(c)<br />
Je, ni lini vyanzo vingine vilivyopo vitatumika ili kuongeza uzalishaji umeme kwenye<br />
gridi ya Taifa<br />
Je, Serikali haioni umuhimu wa kujihusisha moja kwa moja na ujenzi wa miradi hiyo<br />
ili mapungufu yaliyotokea katika ujenzi wa mradi wa Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong> yasije kujirudia<br />
Je, ni lini Mikataba ya Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong> na uhalali wa uwepo wa PAE kwenye sekta<br />
ya gesi asilia utaangaliwa upya ukizingatia hali halisi ya yaliyojitokeza<br />
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-<br />
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, napenda kujibu swali la<br />
Mheshimiwa Yusuph Abdallah Nassir, M<strong>bunge</strong> wa Korogwe Mjini, lenye vipengele (a), (b) na (c)<br />
kama ifuatavyo:-<br />
(a) Mheshimiwa Spika, kwa sasa jumla ya umeme unaotokana na raslimali yetu ya<br />
Gesi Asilia ni MW 400 zinazozalishwa Dar es Salaam kutokea kwenye chanzo cha Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong><br />
Kilwa, MW 7.5 zinazozalishwa kwenye Kituo cha Somanga Fungu, Kilwa kwa gesi inayotoka kwa ajili<br />
ya Son<strong>go</strong> Son<strong>go</strong>, na MW 18 zinazozalishwa kwenye kituo cha umeme Mtwara, kwa gesi<br />
inayotokana Mnazibay kufanya jumla ya MW 425.5 zinazoingia katika mfumo wa umeme wa Taifa.<br />
Mheshimiwa Spika, ili vyanzo hivi vipya vya gesi asili viweze kutumika kukidhi mahitaji ya<br />
gesi asilia yanayozidi kuongezeka TPDC kwa kushirikiana na Makampuni yanayohusika (Maurel<br />
and Prom, Ndovu Resources, na BG) yamejipanga kuchimba visima zaidi ili kubaini kiasi cha gesi<br />
kilichopo. Kazi hii itafuatiwa na shughuli za kuendeleza vyanzo hivyo kwa ajili ya matumizi<br />
mbalimbali zikiwemo kukamilisha bomba la gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es Salaam ifikapo<br />
Desemba, 2013, kuzalisha umeme, matumizi ya gesi viwandani, na pia katika sekta nyingine za<br />
uchumi. Aidha, miradi mbalimbali ya kuzalisha umeme kutokana na vyanzo vingine kama vile<br />
makaa ya mawe, maji na upepo vinaendelezwa.<br />
(b) Mheshimiwa Spika, hivi sasa Serikali kwa kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli<br />
TPDC iko katika mchakato wa maandalizi ya ujenzi wa awamu ya kwanza ya bomba la kusafirisha<br />
gesi asili kutoka Mnazi Bay hadi Dar es Salaam kupitia Somanga Fungu – Kilwa. Maoni ya<br />
Mheshimiwa M<strong>bunge</strong> ndiyo msimamo wa sasa kwenda mbele, wa Serikali kuhusiana na miradi hii<br />
nyeti ya miundombinu. Uwekezaji na umiliki wa miundombinu hii ya gesi asili itakuwa chini ya<br />
Serikali ili kupunguza ukiritimba unaoweza kutokea kwa miundombinu kama hii kumilikiwa na<br />
makampuni binafsi.<br />
12