28.01.2015 Views

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

Read - bunge .parliament.go. tz

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

mbalimbali, kwa mfano maonesho, maadhimisho ya Kkitaifa na mitandao ya jamii (social media).<br />

(Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu huduma za utawala na rasilimali watu, utendaji kazi katika<br />

Wizara uliendelea kuboreshwa kwa kusimamia rasilimali zilizopo. Kwa kutambua umuhimu wa<br />

rasilimali watu, Wizara iliendelea kutoa mafunzo, kuboresha mazingira ya kazi, kuwapatia<br />

watumishi stahili zinazoendana na ajira zao na kusisitiza utawala bora, kusimamia nidhamu ya<br />

watumishi na kupiga vita rushwa. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Wizara yangu iliendelea kutekeleza mpan<strong>go</strong><br />

wa uendelezaji rasilimali watu kwa kubaini mahitaji halisi ya watumishi na sifa wanazotakiwa kuwa<br />

nazo katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya Wizara. Wizara iliwapandisha vyeo watumishi 262<br />

na kuwathibitisha kazini watumishi 76. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, watumishi wa Wizara waliendelea kupata mafunzo ya aina<br />

mbalimbali. Katika mwaka 2010/2011 jumla ya watumishi 100 walihudhuria mafunzo ya muda<br />

mrefu na mfupi ndani na nje ya nchi. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu inatarajia kuwapatia<br />

mafunzo watumishi wapatao 110. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza azma ya kutoa huduma bora kwa mteja, Wizara<br />

yangu iliendelea kutoa mafunzo mahususi kwa watumishi. Katika mwaka 2010/2011 waajiriwa<br />

wapya 84 walipata mafunzo ya awali kuhusu majukumu yao. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara<br />

itaendelea kuboresha huduma kwa wateja kwa kuanzisha kituo maalum cha kuwahudumia<br />

(Customer Service Centre) kwenye makao makuu yake. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu iliendelea kuelimisha watumishi juu ya namna ya<br />

kujihadhari na UKIMWI. Watumishi 19 waliopima na kutoa taarifa kwa uon<strong>go</strong>zi juu ya hali ya afya<br />

zao waliendelea kupatiwa huduma za dawa na lishe kila mwezi. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara<br />

itaendelea kuhamasisha upimaji wa afya kwa hiari na kutoa huduma kwa watumishi wanaoishi na<br />

virusi vya UKIMWI. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kuhusu Vyuo vya Ardhi, Wizara yangu inasimamia Vyuo vya Ardhi vya<br />

Tabora na Moro<strong>go</strong>ro ambavyo vinatoa mafunzo ya stashahada (Ordinary Diploma) katika fani za<br />

urasimu ramani na upimaji ardhi na Cheti katika fani za umiliki ardhi, uthamini na uchapaji ramani.<br />

Wataalam wanaosomea fani hizi wanahitajika kwa wingi katika Serikali Kuu, Taasisi za Umma na<br />

Serikali za Mitaa. Katika mwaka 2010/2011 walihitimu wanafunzi 130. Kati yao 50 walitoka Chuo<br />

cha Ardhi Moro<strong>go</strong>ro na 80 walitoka Chuo cha Ardhi Tabora. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2010/2011 Wizara yangu iliendelea kutekeleza mradi wa<br />

upanuzi wa Chuo cha Ardhi Tabora kwa kujenga mabweni, madarasa na maktaba ili kuongeza<br />

udahili wa wanafunzi. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa mradi huo unaendelea. Ujenzi wa<br />

bweni unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2011. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara itaendelea<br />

na ujenzi wa maktaba na ukarabati wa madarasa. (Makofi)<br />

Mheshimiwa Spika, shukrani, katika muda mfupi niliotekeleza majukumu yangu katika Wizara<br />

ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, nimeona jinsi Wizara ilivyo na majukumu mazito<br />

yanayogusa nyanja zote za kiuchumi, kijamii na kisiasa za nchi yetu. Ni mategemeo yangu<br />

kwamba Bunge litaendelea kuwa na mtizamo chanya na kuipa kipaumbele Wizara hii na sekta ya<br />

ardhi kwa ujumla kulingana na mchan<strong>go</strong> wake katika kufanikisha juhudi za kuleta maendeleo ya<br />

haraka katika nchi yetu. (Makofi)<br />

Mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya ardhi katika mwaka 2010/2011 ni matokeo ya<br />

ushirikiano na misaada ya kifedha na kitaalam kutoka kwa nchi wahisani, taasisi zisizokuwa za<br />

Kiserikali, Mashirika ya Kidini na taasisi za fedha za Kimataifa. Wadau hao ni pamoja na Shirika la<br />

Maendeleo la Ujerumani (GIZ); Benki ya Dunia na Serikali za Denmark, Sweden, Uholanzi na<br />

Uingereza kupitia Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (Business Environment Strengthening<br />

for Tanzania); Serikali za Finland na Norway na Shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa (UN-<br />

HABITAT). (Makofi)<br />

35

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!