Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Read - bunge .parliament.go. tz
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
mbalimbali, kwa mfano maonesho, maadhimisho ya Kkitaifa na mitandao ya jamii (social media).<br />
(Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kuhusu huduma za utawala na rasilimali watu, utendaji kazi katika<br />
Wizara uliendelea kuboreshwa kwa kusimamia rasilimali zilizopo. Kwa kutambua umuhimu wa<br />
rasilimali watu, Wizara iliendelea kutoa mafunzo, kuboresha mazingira ya kazi, kuwapatia<br />
watumishi stahili zinazoendana na ajira zao na kusisitiza utawala bora, kusimamia nidhamu ya<br />
watumishi na kupiga vita rushwa. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2010/2011 Wizara yangu iliendelea kutekeleza mpan<strong>go</strong><br />
wa uendelezaji rasilimali watu kwa kubaini mahitaji halisi ya watumishi na sifa wanazotakiwa kuwa<br />
nazo katika kutekeleza majukumu mbalimbali ya Wizara. Wizara iliwapandisha vyeo watumishi 262<br />
na kuwathibitisha kazini watumishi 76. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, watumishi wa Wizara waliendelea kupata mafunzo ya aina<br />
mbalimbali. Katika mwaka 2010/2011 jumla ya watumishi 100 walihudhuria mafunzo ya muda<br />
mrefu na mfupi ndani na nje ya nchi. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara yangu inatarajia kuwapatia<br />
mafunzo watumishi wapatao 110. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza azma ya kutoa huduma bora kwa mteja, Wizara<br />
yangu iliendelea kutoa mafunzo mahususi kwa watumishi. Katika mwaka 2010/2011 waajiriwa<br />
wapya 84 walipata mafunzo ya awali kuhusu majukumu yao. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara<br />
itaendelea kuboresha huduma kwa wateja kwa kuanzisha kituo maalum cha kuwahudumia<br />
(Customer Service Centre) kwenye makao makuu yake. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu iliendelea kuelimisha watumishi juu ya namna ya<br />
kujihadhari na UKIMWI. Watumishi 19 waliopima na kutoa taarifa kwa uon<strong>go</strong>zi juu ya hali ya afya<br />
zao waliendelea kupatiwa huduma za dawa na lishe kila mwezi. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara<br />
itaendelea kuhamasisha upimaji wa afya kwa hiari na kutoa huduma kwa watumishi wanaoishi na<br />
virusi vya UKIMWI. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kuhusu Vyuo vya Ardhi, Wizara yangu inasimamia Vyuo vya Ardhi vya<br />
Tabora na Moro<strong>go</strong>ro ambavyo vinatoa mafunzo ya stashahada (Ordinary Diploma) katika fani za<br />
urasimu ramani na upimaji ardhi na Cheti katika fani za umiliki ardhi, uthamini na uchapaji ramani.<br />
Wataalam wanaosomea fani hizi wanahitajika kwa wingi katika Serikali Kuu, Taasisi za Umma na<br />
Serikali za Mitaa. Katika mwaka 2010/2011 walihitimu wanafunzi 130. Kati yao 50 walitoka Chuo<br />
cha Ardhi Moro<strong>go</strong>ro na 80 walitoka Chuo cha Ardhi Tabora. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2010/2011 Wizara yangu iliendelea kutekeleza mradi wa<br />
upanuzi wa Chuo cha Ardhi Tabora kwa kujenga mabweni, madarasa na maktaba ili kuongeza<br />
udahili wa wanafunzi. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa mradi huo unaendelea. Ujenzi wa<br />
bweni unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2011. Kwa mwaka 2011/2012 Wizara itaendelea<br />
na ujenzi wa maktaba na ukarabati wa madarasa. (Makofi)<br />
Mheshimiwa Spika, shukrani, katika muda mfupi niliotekeleza majukumu yangu katika Wizara<br />
ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, nimeona jinsi Wizara ilivyo na majukumu mazito<br />
yanayogusa nyanja zote za kiuchumi, kijamii na kisiasa za nchi yetu. Ni mategemeo yangu<br />
kwamba Bunge litaendelea kuwa na mtizamo chanya na kuipa kipaumbele Wizara hii na sekta ya<br />
ardhi kwa ujumla kulingana na mchan<strong>go</strong> wake katika kufanikisha juhudi za kuleta maendeleo ya<br />
haraka katika nchi yetu. (Makofi)<br />
Mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya ardhi katika mwaka 2010/2011 ni matokeo ya<br />
ushirikiano na misaada ya kifedha na kitaalam kutoka kwa nchi wahisani, taasisi zisizokuwa za<br />
Kiserikali, Mashirika ya Kidini na taasisi za fedha za Kimataifa. Wadau hao ni pamoja na Shirika la<br />
Maendeleo la Ujerumani (GIZ); Benki ya Dunia na Serikali za Denmark, Sweden, Uholanzi na<br />
Uingereza kupitia Mradi wa Kuboresha Mazingira ya Biashara (Business Environment Strengthening<br />
for Tanzania); Serikali za Finland na Norway na Shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa (UN-<br />
HABITAT). (Makofi)<br />
35