verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Kazungu: Ndiye huyu mzee wangu<br />
Com. Wambua: Basi aketi hapo atoe maoni. Mzee nitakupatia dakika mbili tuu kwa kifupi utoe maoni yake halafu<br />
utupatie hiyo maandi, tutaenda kuyasoma halafu tu.................................(inaudible)<br />
Ali Hamisi: Kwa jina naitwa Ali Hamisi. Katika maoni ya watu wa Bombo Kassan, ambao wamenipa nije niwakilishe<br />
hapa Bombo Kassan, wamesema kuwa kuwe na serikali ya majimbo. Watu wa huko wamesisitiza sana serikali ya majimbo ili<br />
kila jimbo liweze kujitawala hilo lenyewe. Jambo la pili, kila mwana kenya aliyezaliwa jimbo hilo au ambaye anaishi katika<br />
jimbo hili au ambaye amezaliwa katika jimbo hili aishi jimbo hilo hilo kwa sheria ya jimbo. Jambo la tatu, zile manifesto ya<br />
viama vya kisiasa viwe na muongozo wa majimbo, ziwe na maongozo ya majimbo. Hivi ndivyo wato wa Kassani wamenieleza<br />
kuwa nije nitoe hayo manifesto, zile sheria za kisiasa, vile vitabu vyao waweke sheria za majimbo. Sikuwa yeye ana chama kina<br />
kile kitabu chao cha manifesto na hakina majimbo. Huyo asipatiwe licence ya kupigia kura katika Kenya. Lazima manifesto<br />
yake iwe ina mwongozo wa majimbo. Jambo la elimu, watu wa Bombo Kassani wamepitisha au wametoa mawazo yao kuwa<br />
elimu, kwa vile watu ni maskini zaidi na watoto wanaendelea kuzurura ovyo ovyo, iwe ya bure mpaka form four. Hapa ndio<br />
patakua hana uwezo wa kujitafutia kazi yeye mwenyewe hata kama hakuendelea. Kuhusu wabunge, mbunge kawaida zao ni<br />
kuwanyanyasa wananchi. yeye anasimamisha wananchi mlolongo kupigiwa kura halafu akisha pata basi, hawajui wananchi.<br />
kwa hivyo, mbunge kama huyo ambayo hashugulishani na wale matajiri wao waliowaandika, hawatizamiwa kiasi cha miaka<br />
miwili. Ikiwa hakutimiza masharti ya wananchi, atolewe, aje hapa nyumbani arudishwe mtu mwingine. Kuhusu waislamu,<br />
muislamu ana haki ya kupewa dhima yake na sheria zake na hukumu zake ziliko katika kitabu cha Koran tukufu. Muislamu<br />
kwa kifupi, katika sheria ya kislamu, mwizi akiiba hukatwa mkono. Tunaomba katiba nayo itupe uwezo huu ili tupunguze haya<br />
matatizo ya wizi. Katika muislamu, mtu katika sheria ya kislamu, mtu akishikwa na bibi ya mwenziwe ni apigwe mawe<br />
hadharani mpaka afe. Hii ni sheria iko katika kwa waislamu. Katika sheria za kislamu, zipewe uwezo wa kuweza<br />
ku........................(inaudible) kwa ufupi<br />
Com. Wambua: tafadhali, malizia tafadhali<br />
Speaker: Malizia<br />
Ali Hamisi: Kwa hivyo ninamalizia kwa kusema kuwa, katika sheria ya kislamu, mtu akiua mwenziwe ni auawe, akiuwa<br />
mwenziwe na auawe na akimjuruhu mwenziwe, akimkata kisu ipimwe kiasi cha vile alivyokatwa na yeye akatwe.<br />
Com. Wambua: Asante sana mzee, kwa hivyo jiandikishe hapo<br />
tafadhali....................................................................(inaudible<br />
101