verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Com. Pr. Ayonga: Unafikiri utaongea dakika ngapi?<br />
Ali Asaa: Zile utakazo ni ruhusu wewe, lakini ningependa…..<br />
Com. Pr. Ayonga: Lakini unapoona wengi, wewe unaona aje? Wewe ni mzee mwenzangu.<br />
Ali Asaa: Ni mzee mwenzangu kweli, lakini, nipe kidogo leo, maanake siku ile tuli…..<br />
Com. Pr. Ayonga: Leo?<br />
Ali Asaa: Siku ile tuliwachana kati kati. Kama wataka kuniweka mwisho, pia ni sawa.<br />
Com. Pr. Ayonga: Tafadhali, ni mimi ninaongea naye. Mzee!<br />
Ali Asaa: Ndio.<br />
Com. Pr. Ayonga: Tafadhali ……………………. (inaudible) tafadhali.<br />
Ali Asaa: Asante sana. Asante. Kwanza, napiga shkurani kwa Mwenyezi Mungu kwa kunipa wafsi kama huu, kuja<br />
kuhudhuria kikao kama hichi. “…………….. (inaudible)”, sisi Waislamu kabla ya kuanza jambo lolote, Mwenyezi Mungu<br />
ametuamulisha tumutangulishe yeye. Mawazo yangu na maoni yangu ni haya:-<br />
Jina langu kwa kikamilivu ni Ali Taabu Asaa.<br />
Ninalopendelea mimi kwanza, linalouma watu wa Kisauni pamoja na mimi mwenyewe, na Waislamu wote, na wakaaji, hata<br />
Wakristo – ndugu zote, ni squatters wa Coast, hasa hii Mombasa, Kisauni, umeishi muda mrefu sana. Kwa hivyo,<br />
tungependelea, na kuiomba Serikali yetu tukufu, iondoe kabisa, marufuku kabisa, hapa mwaka ujao, tukute sisi si ma-squatters<br />
tena.<br />
Jambo la pili, tungependelea, Rais akiwa ni Mkristo, makamu wake awe ni Muislamu ……………….. (inaudible). Na mvumu<br />
wa Serikali hiyo yote tunayozungumzia, iwe ni ya Majimbo.<br />
Na tungependa Waislamu wenyewe, wawajiwe mambo yao wajiamulie kulingana na …………………………. (inaudible).<br />
Na Kadhi wetu apewe mamlaka sawa na ma-Judge wale walioko kortini, maanake wote wako katika nyuma ya Serikali.<br />
Chief Kadhi apewe gari, apewe na driver, na wale ma-Kadhi wadogo pia kadhalika, wafanyiwe usawa na wale ma-Judge<br />
51