28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Na swala lingine ambalo ningependekeza ni kwamba hao wanao gombea ubunge. Lau mtu amepata term yake ya kwanza a<br />

serve term mbili pekee yake. Yaani kipindi cha miaka kumi. Baada ya miaka kumi ile, haruhusiwi tena kugombea ule ubunge<br />

kwa sababu atakuwa akili yake sasa imesha zorota kimaendeleo. Atakuwa sasa ni mtu wakujinufaisha matumbo yake na<br />

kugandamiza wananchi. Hakuna mmoja atakal<strong>of</strong>anyia. Mfano mzuri twaona Mvita huko.<br />

Na swala lingine ambalo ningependa kuzungumzia ni ile wazungu wasema “justice delayed, is justice denied”. Serikali yetu<br />

kwa hakika ina senti za kutosha. Na hapa kutokana na kwamba ina senti za kutosha, ingeongeza idadi ya mahakimu, hawa<br />

magistrates, wangeongezwa wakawa wengi, na kukawa na transparency ya zile kesi. Sio mtu yule askari anashika, amemuona<br />

kabisa akitoka dukani amuuliza watoka wapi na waenda wapi. Si unaona mimi natoka dukani naenda nyumbani. Swala kama<br />

lile lirekebishwe kwamba yule mtu akishikwa akipelekwa kotini, atakuwa ni mtu (inaudible)<br />

wanakwenda pale, wanazungumza kesi yao, kama ni mashahidi anawaita, siku ile ile mashaidi wao wanazungumza kesi ile.<br />

Ikifika kwamba amehukumiwa kufungwa, anakwenda kutumika kisawa. Sio kwamba anakwenda kuhukumiwa kwa kwamba<br />

amegandamizwa. Tunaona sera hii inatumika Uganda, na sera hii pia inatumika Tanzania. Kwa nini Kenya tusiitumie?<br />

Na swala lingine ni hili swala la mapolisi. Watu wengi wamelizungumzia swala la mapolisi na kama kila mtu anavyojua, sisi sote<br />

tukimwona polisi hata akiingia hapa kila mtu ataingiwa na baridi. Kwa sababu gani? Wamewekwa katika hali ya kuwa wao<br />

wana nguvu zaidi kutushinda sisi raia tunaowalipa. Maana yake wao hawajui mishahara yao inatoka kwa kodi zetu tunazolipa<br />

sisi, lakini imekuwa sasa wao ndio wanatugandamiza. Wanatugandamiza hali ya kuwa ukimwona askari yule askari anakuwa<br />

akikushika, ashakuhukumu maana anakupiga, anakuadhibu haraka upesi. Inakuwa wewe hakuna cha kujitetea wewe uko chini<br />

ya ulinzi, na anakwambia chochote utakachosema kitatumika kukuhumu koti, na hakuna koti utakayo fikishwa. Kwa hiyo<br />

lazima kuwekwe kipengele cha kwamba maaskari wafundiswe sheria. Wafundishwe transparency, kusaidia raia na kuwaokoa<br />

maisha yao, isiwe tu wanatuumiza.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Asante, asante.<br />

Salimi Mwambala: Haya, shukurani.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Unaweza kutoa hayo maandishi?<br />

Salim Mwambala: Ah Ah. Ilikuwa bado moja tu ningelizungumzia basi.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Ukizungumzia moja utatuachia?<br />

Salim Mwambala: Ah si waachii, nafikiri mshaandika nyinyi wenyewe. Hize ni points zangu ndogo ndogo tu nimeaandika.<br />

21

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!