verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
asubuhi. Kuja hapa usungumuze.<br />
Zainab Said: Asalamualekum.<br />
Audience: Aleikumsalam.<br />
Zainab Said: Mimi ninajulikana kama Zainab Said nimkaaji wa Kongowea lakini Kisauni Division.<br />
Neno la kwanza linalo niuma hapa kwetu ni mambo ya ardhi. Sisi tunalipia ardhi na tunaowalipa sio wa Kenya na isitoshe<br />
wengine hawaishi hata hapa Kenya, wako Canada, wengine wako America lakini anaokota pesa kutoka kwa wa Kenya. Sioni<br />
sababu tuendelee kuwalipa pesa watu hawa.<br />
Jambo la pili ni kuhusu kina mama. Kina mama tunaambiwa kuna fungu la pesa utengua na Serikali kwa maendeleo ya akina<br />
mama na shuhuli zote za akina mama. Lakini tuafanya kusikia kwa majina tu. Hatuzijui pesa hizi wala hatujui azipokeae ni nani<br />
wala zitamfaidi nani lakini tuajua budget yetu ikitengua kuna pesa ya akina mama. Shuhuli za maendeleo za akina mama Serikali<br />
aijisumbui nayo. Mukitengeze vikundi mtakuja muambiwe fanyeni vikundi, fanyeni nini, fanyeni nini, mtasaidiwa, lakini yale ua ni<br />
maoni pengine ni Mbunge ataka kura, pengine ni mkubua ataka sifa, lakini hakuna chochote tunacho fanyiwa. Hasa wale<br />
wamama walio chini kiwango cha chini. Na wakubua wanao shikilia vieo kule kwa maendeleo huwa ni wale, wale<br />
hawabadilishwi. Ninataka mkubua akishika cheo akae muda flani aondoke ashike mwingine. Sasa tutamjua kama alikua na<br />
makosa ama alikua ni mtu mzuri.<br />
Tatu, upande wa Kazi: Kina mama tunasumbuliwa kwa njia nyingi sana. Wewe ukiwa ni mrembe basi olewako. Ukienda<br />
kuandikiwa kazi, General Manager, iwakutaka Director, iwakutaka wewe Karani, iwakutaka wewe mpaka <strong>of</strong>is messenger pia,<br />
wakujitetea huna. Ukiwa wewe ni secretary, basi wewe u secretary wako wakalamu na u secretary mwingine juu. Vile boss<br />
anavyo taka ndivo utakovyo fanya. Hata ukiwa ni mku wa mtu. Na katika hali yetu tulionao kwa sasa hatuna pesa, hatuna nini<br />
pengine hata yule mume hana kazi wewe ndio waangalia kila mtu. Wengine wanalizimika kukubali, ili alishe familia yake. Laki<br />
ni njia mmoja ya kunyanyasa kina mama.<br />
Hawa rapists nao, wanawachua free. Mtu yule ati anapewa community services. Hataona msichana mdogo mwingine amrape?<br />
Ama hataona mama mwingine amrape? Rapist na mnyongaji wote hali mmoja. Waoze huko huko jela.<br />
La mwisho ni askari wetu. Askari wanatunyanyasa. Si askari pekee, ni wao na watu wajivitambulisho pamoja na watu wa<br />
jikaratasi za Passport. Kila mmoja ukimkuta tu tumbo li huko. Hapokei mshahara. Mshahara ni wewe. Ukienda wewe huna<br />
pesa, huna Passport na nafikiri Passport ni haki yangu. Birth Certificate, watoto wengine sio kina mama wote wana pesa<br />
kwenda kuzalia hospitali. Na saa zingine kuzaa ni kama kifo. Hakuagi. Unaweza kutoka hapa waenda pengine Utange,<br />
64