28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

kujua raisi wake aliyetu kombolea nchi hii ni nani kuliko kuingia kwa hasara ya kutengeza pesa sijui Kibaki pesa zake, kijana<br />

pesa zake, hii ni kuharibu mali ya uma sana. Halafu mishahara, kazi zote, kazi zote zifikiriwe mishahara maalum, wabunge<br />

mishahara yao ipunguzwe na hata ma-commssioners pia mishahara yao tunaona ni mingi sana. Ikiwa sisi hapa tumeshinda<br />

kutoka asubuhi hatujakula, na tumefanya kazi hii kuhakikisha kwamba nini, hiyo ni haki gani? Asanteni kwa hayo machache,<br />

asante.<br />

Com. Wambua: Asante sana, jiandikishe hapo, tume sikia maneno yako kwa hivyo wamepokelewa. Sasa, tutawauliza tu<br />

watu wengine wawili watu hivi halafu tutafunga kikao. Wale ambao wamebakia, bila kutoa maoni ni watu wengi na ni arobaini<br />

na watano, nimewahesabu tayari. Kwa hivyo inaonekana lazma tutafanya mpango turudi hapa ndio maoni ya wale ambao<br />

wamebaki yatapokelewa. Hata tukiketi hapa mpaka kesho asubuhi, pengine hatutamaliza kwa hivyo lazima tutamaliza.<br />

Tutawapatia nafasi mzee tu hapa aliyefika hapa wakati huu na wawili wao ndio wataongea peke yao. Tutamwita mmoja, Peter<br />

Musiko<br />

Peter Msiko: Peter Umano<br />

Com. Wambua: Sasa wewe tutakupatia nafasi dakika mbili utupatie maoni yako halafu yule atakayefuata ni John<br />

Nyangate, ndiye atakaye fuata halafu kumalizia kabisa baada ya hawa wawili kutoa maoni yao, tutamwita huyu Bwana<br />

Khumala, nilimtaja, ako wapi halafu wewe ndiyo sasa utamalizia. Halafu tufunge kikao. Endela hapo Peter Musiko<br />

Peter Msiko: Mimi naitwa Peter Msiko na sioni, jambo la kwanza. Ningependa kuzungumza kuhusu hasa sisi watu<br />

ambao kwa jumla walemavu na vip<strong>of</strong>u kwa sababu sisi huwa tunapata shida sana katika hii serikali yetu ya wakati huu. Kwa<br />

sababu sisi bado hatujajulikana ama sisi tuko watu. Ingawaje sisi tunajiona tuko watu, bado hatujatambulika kama sisi tu watu.<br />

Nikasema hivyo kwa nini, sababu utakuja ona hata kama kwenye parliament, wakati inasemekana parliament inafanya vikao<br />

vyao, hutasikia habari wa walemavu ikigusiwa, wala eti walemavu wafanyiwe hivi, hiyo ni kitu tunafaa kuzungumza just verbally.<br />

Na inafaa kusemekana tu basi, walemavu watapata kitu fulani na hio kitu inaishia pale pale hata hiyo kitu hatutaiona, inaisha vile<br />

vile. Na jambo lingine, watoto walemavu hata sisi walemavu, elimu yetu kama tungepewa elimu ya bure, kidogo ingesaidia<br />

walemavu kwa njia nyingine. Kwa sababu sasa ikiwa mzazi wa mlemavu anaambia atoe shilling elfu ishirini ama thelathini alipie<br />

mtoto wake mlemavu, na zile pesa hana, atafanya nini? Yule mlemavu itabidi akae nyumbani bila kusoma na utakuja kuona pia<br />

katika hivyo pia, mtu ambaye haoni shida ni hio hio. Kwa sababu utakuja kuona kama wewe huoni na kama haukusoma, uko<br />

hali yako pengine na mwenzako. Na utakuja ukipita mbele ya watu wengine pia wanauliza, ‘eh, na huyu mtu, namna gani huyu<br />

mtu, ana tembea ki vipi huyu mtu?’ kuna wale wana roho ya imani, watakushika mkono akuambie, ‘ eh, mzee ama mama, hapa<br />

utagongwa na kitu, pita hapa hivi’. Lakini kuna wale wanakuangalia tu, wewe unapita lakini kama una elimu kidogo na uko na<br />

idea ya kutembea, unatembea. Tatu, sisi walemavu tunataka wakati tumeajiriwa, tupate kuajiriwa na ma kampuni, tusifanyiwe<br />

ubaguzi. Katika ma kampuni mengi utakuta walemavu hatupendwi sana kwa sababu wanafikiria pengine huyu hata akiandikwa,<br />

atafanya kazi gani huyu? Pengine huyu mlemavu hata akiwekwa hapa, atafanya kazi gani huyu? Hakuna kazi yoyote atafanya.<br />

107

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!