28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Com Paul: Asante kwa maoni yako, jiandikishe hapo tafadhali, halafu nitamuita Muhammed Abdul, Muhammed yuko,<br />

Muhammed yuko, Muhammed Bashuara, Muhammed Bashuara, tafadhali tumia dakika mbili tu uguzie yale muhimu.<br />

Muhammed Bashuara: Niongezee ya tatu maana ake mambo yangu ni matatu tu nayo ni mafupi mafupi sana, Asalamu<br />

waleykumu.<br />

Wananchi : Waleykumu salamu<br />

Com Salome: Sema jina lako.<br />

Muhammed Bashuara: Jina langu ni Muhammed Bue Bashuara, na sina mengi yangu sana ya kusema ni matatu paeke yake,<br />

langu la kwanza hasa kuhusu Katiba, ningependelea Katiba ya Kenya, inapomalizwa, lakini iwe ni mfumo wa elimu wa watoto<br />

kutoka darasa la kwanza mpaka kufikia darasa la mwisho, na nikishangia kwa sababu, ni kwamba Katiba inasema (inaudible)<br />

na Mwananchi wa kawainda wa Kenya hajui chochote kile, natunyanyazwa sana na mambo hayo ya Katiba kama vile hivi leo<br />

tunavyozungumza hapa, tuanapata ardhi ya ulongo na ni ardhi yako na unanyanyaswa nayo tena. Juu huna kibali na Katiba ya<br />

Kenya huijui Mwananchi, kwa hivyo mimi naonelea ifundushwe dani ya skuli kama kawaida ya masomo mengine yale yote ya<br />

Kenya.<br />

Ningependelea ardhi igawanywe kwa muafrika mwenyewe halisi ambaye kwamba ako na asili ya mahali alipotoka, tusikae tu<br />

kikoloni kutoka tulipoanza wakoloni mpaka hivi leo tuko chini ya ukoloni wakiarab, wakizungu na wakimatajiri na<br />

wakibebebari kama sisi hapa tulipo hapa afrika, tunanyanganya tena wafrika wenzetu, kwa hivyo jambo hili, katika Katiba ya<br />

Kenya itiliwe mkazo kwamba Mwananchi ambaye atapata ardhi , agawanyiwe na Wananchi wenyewe hasa wanaohusika<br />

katika makao au katika eneo hilo wanaloishi. Iandikishwe ama apewe Title Deed yakena hasa sehemu ambazo hazina title<br />

deeds watu wapewe titile deeds zao wanapo gawanyiwa mashamba yao kwa njia ya haki na ya ukweli.<br />

Nikimalizia sehemu yangu ya tatu, nitazungumzia kuhusu uislamu, nigependelea katika Katiba ya Kenya, isibadilishe tabia na<br />

mila na desturi za kislamu, kutokana na <strong>of</strong>fice ya Chief Kadhi, kuwe na mgawanyiko au na mpangilio kutoka juu ya kwa <strong>of</strong>fice<br />

ya Chief Kadhi mkuu wa Kenya itelemka kila sehemu mpaka wilaya, na watu hawa pia, walipwe malipo kulingana na sheria za<br />

kikadhi ama za kislamu kwasababu yeye ni mwisl;amu lakini mambo anay<strong>of</strong>anya ni ya sheria za hapa nchini kwetu Kenya kwa<br />

hivyo huyu mtu anastahili naye kupata chochote kutokana na uongozi wake ama na umutumishi wake wa umma anaotumikia<br />

Waislamu. Pia Katiba hii ibakishe haki ya muislamu hasa kuhusu kama mwanamke, mwanamke ni mtawala wa mwanamume<br />

kulingana na sheria za kislamu. Kwa hivyo Katiba ya Kenya iweke wazi kwamba muislamu ana Katiba yake maalumu ambayo<br />

inatoka katika kitabu tukufu cha Koran ambayo ana haki kuhusu uridhi, na ndoa na tarakakwa hivyo napenda sana kuchangia<br />

jambo hili la Waislamu saidi kwamba Katiba iangalie sana masilahi ya Waislamu hapa Nchini Kenya. (in venacular)<br />

86

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!