28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

unaumua njiani, unamzaa yule mtoto. Kuna Midwife pale ambae ataandika kila kitu. Utakapo kwenda hospitali hakuna<br />

anaekusikiza. Ukienda kwa Birth Certicate, hoo, nilizalia nyumbani, ndio balaa kabisa. Sasa watoto kama hawa tuafanyie nini?<br />

Na watoto walemavu, ukienda nae hospitali akiwa bahati mbaya ametiliwa mimba ni wakike, ukisema niacheni nimzungumuzie,<br />

hakuna anaekusikiza ‘mama kaa nje hii ni labour’. Mimi ni mama, sistahili kufukuzua kutoka kwenya labour. Nataka kumsaidia<br />

huyu, lugha yake nailewa mimi. Nyinyi hamuielewi na hamna watu special ambao mume waweka kwa kuhudumia. Sasa<br />

mlemavu yule atakua kuambiwa ‘sukuma wee, yuaruka’. Kisha wanampiga.<br />

Com. Wambua: Mama tumeyasikia hayo yote kwa hivyo asante sana na ujiandikishe pande huu.<br />

Maua Said: Na mimi nashukuru.<br />

Com. Wambua: Mama jiandikishe hapa tafadhali. Tuna Amina. Amina. Yuko? Rev. Joseph Kashuru? Rev. uko na<br />

maandishi umeitengeneza? Basi tutakupa dakika tatu tu tafadhali. Watu ni wengi. Mulika tu yale yalio muhimu na utupe haya<br />

maandishi. Tutaenda kuyasoma yote.<br />

Rev. Joseph Mangaro Kashuru: Kuma ungenipa tano --- haya. Mimi ni Rev. Joseph Mangaro Kashuru na ninawakilisha<br />

Kanisa la Ki Anglicana, Mombasa. Tuliandika mambo haya kwa ki lugha ya kimombo lakini tuko Mombasa, nitaongea tu<br />

Kiswahili halafu mwingine atasema Kizungu huko mbele.<br />

Katiba tulionayo haituambii sisi wa Kenya tumetoka wapi. Kwa hivyo hakuna ajuae ni Mkenya kivipi? So, tungependa Katiba<br />

iwe na ile inaitua kwa Kizungu Preamble ili ittujulishe sisi wa Kenya tulitokezea wapi, na tulitoka Shungwaya au tulitokea<br />

Matondo? Hilo ni la kwanza.<br />

Jambo la pili, tungelipenda Serikali iwe ya Majimbo. Hilo hatuwezi kuli -----(clapping)<br />

Na huyu ambae atakua kiongozi wa kule juu, angalau aweze ku serve kwa terms mbili za miaka mitano, mitano. Akimaliza<br />

miaka yake kumi, hata kama ni mzuri sana aachue. Twende kwa jimbo lingine nalo lionje hio cake kubua.<br />

Tungelipenda tuwe na Regional Assemblies ambao ziko chini ya ma Governor ambao watakua wakifanya kazi na dhani mna<br />

elewa nyinyi Serikali ya Majimbo inakaa je kuliko sisi. Kwa hivyo ninadhani mnaelewa ninasema nini? Huyu kiongozi kwanza<br />

awe mwananchi, huyo President.<br />

Pili, kama ni kusoma, angalawo awe amefika Unversity na kiuwezi au kifedha awe ni, anaitua kwa Kizungu Economically stable<br />

asije apewe u President halafu akaanza kuinufakia pekee yake halafu, mengine akaharibika.<br />

65

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!