verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Kenyan, must be allowed to do so as long as he fulfills the required conditions. The conditions should be reduced to the<br />
minimum in order to encourage as many immigrants or refugees or aliens who would like to become Kenyans. Once a person<br />
is married to a Kenyan, he or she should automatically become a Kenyan regardless <strong>of</strong> the sex. In this regard I am considering<br />
our immediate people <strong>of</strong> Somalia, Ethiopia, Sudan, Uganda, Tanzania and the Indian Ocean Island where there is a lot <strong>of</strong> cross<br />
border marriages. Every citizen is entitled to basic rights, food, clothes, health, shelter, education, life, livelihood or<br />
employment, freedom <strong>of</strong> association and <strong>of</strong> expression. A citizen must obey the Constitution and all other laws being enacted<br />
from time to time.<br />
Com. Pastor Zablon Ayonga: Hebu muulika maoni yale makubwa makubwa.<br />
James Olopono: Haya, asante. Maoni mengine yamo ndani ya karatasi ambayo nitapeana kwa hivyo nitafanya kwa ufupisho.<br />
Kuhusu uzalendo au citizenship, nimependekeza kila Mkenya awe Mkenya bila kuulizwa maswali mengi. Haya, kwa<br />
kuzaliwa, kwa ajili ya mzazi kuwa Mkenya na kwa ajili ya kupenda kuwa Mkenya. Unahamia kutoka nchi ingine, umependa<br />
kuishi Kenya na unataka kuwa Mkenya halisi, uruhusiwe, usizuiliwe kwa njia yeyote.<br />
Kuhusu mambo ya vitambulishe: Ingewezekana tunapendelea kila Mkenya amezaliwa Kenya apewe kitambulisho, apewe<br />
passport, apewe cardi ya kura mradi tu akigonga miaka kumi na nane, tangu siku yake ya kuzaliwa. Na hiyo yote inawezekana<br />
kwa ajili Kenya sasa ni computerized, watoto wakizaliwa majina yao na siku ya kuzaliwa iwekwe ndani ya computer. Miaka<br />
ya kumi na nane ikifika, apewe vitu hivyo bila kuulizwa maswali zaidi.<br />
Kuhusu defence and national security, usalama wa nchi: Rais haitajiki kuwa mkuu ya majeshi, haitajiki kusimamia kila sehemu,<br />
kila kituo, askari polisi, askari jeshi, hapana. Rais apeana vyeo vyingine kwa Wakenya na awaamini ya kuwa watasimamia<br />
jukumu yao bila wasiwasi. Kwa hivyo kuwezekane kuwe na Minister for Defence na aachwe afanye kazi yake kikamilifu.<br />
Kuwe na Commander <strong>of</strong> the Armed Forces t<strong>of</strong>auti na Rais na asimamie wanajeshi sawa sawa. Hapana changanya na si vizuri<br />
mtu mmoja kuwa na viti vyote ya Kenya. Igawanywe gawanywe, kila mwingine apewe.<br />
Kuhusu vyama vya kisiasa: Ninapendekeza vyama viwe vitatu. Chama kimoja ambacho kina majority, chama ya pili ambacho<br />
kina majority ya pili na chama cha tatu, kiitwe independent party. Chama ambacho kitasomba Wakenya wengine ambao<br />
hawataki chama ya kwanza, na hawataki chama cha pili. Lakini kuwa na mlolongo ya chama arubaini, sitini haifai. Zipunguzwe,<br />
zifanyiwe screening, uchuji, zichujwe kabisa zibaki tu tatu pekee yake. Halafu sisi tunajiandikisha kwa hivyo vitatu.<br />
Com. Pastor Zablon Ayonga: James saa yako imekwisha.<br />
James Olopono: Asante sana Bwana mwenye kiti. Kuna mengine mengi ningesema lakini kwa vile nitapeana ikiwa kwenye<br />
kitabu, ninaamini ma-commissioners watashughulikia vilivyo. Asante sana.<br />
5