verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Com. Pastor Zablon Ayonga: Okay. Mambo yako yote yameingia katika (inaudible)<br />
Salim Mwambala: Yameingia hapo, asante.<br />
Com. Pastor Zablon Ayonga: Njoo ujiandikishe. Bwana Aggrey Kilo. Aggrey Kilo unamaandishi?<br />
Aggrey Kilo: Ndio ninamaandishi.<br />
Com. Pastor Zablon Ayonga: Kwa hiyo mulika tu juu ya maandishi yako.<br />
Aggrey Kilo: Nashukuru macommissioner na wananchi waliojitokesha hapa. Kwa majina mimi naitwa Aggrey Kilo vile<br />
Bwana Chairman alikuwa amesema na mimi nina vidokezo tatu tu ambavyo nitazungumzia. Kwanza kabisa ni kuhusu nyumba,<br />
nyumba za upangizaji. Unakuta ya kuwa Kenya sasa serikali ama munispaa, si kama mukoloni, mukoloni alikuwa anajenga<br />
nyumba za wapangizaji lakini serikali ya sasa ama munispaa ya Kenya saa hii, hawafanyi hivi. Na hatuelewi ni kwanini. Ile pesa<br />
mkoloni alikuwa anaokota ndio ile serikali ya sasa inarokota, na unakuta serikali ama munispa, hawatujengei nyumba za<br />
kupangisha. Sasa hio imeleta jambo ambapo sasa ni wafanyi biashara fulani wanajenga nyumba, (inaudible) kuna kuwa<br />
na wapagizaji. Sasa wale watu wanaweka sheria fulani. Anasema ukiingia kwa hii nyumba yangu, utalipa deposit ya miezi tatu<br />
ama mieze miwili. Sasa vile unataka kuingia kwa nyumba na una haraka unampa ile pesa. Ukisha mpa ile pesa pengine<br />
unapigwa transfer kwa haraka. Unamwambia ile pesa yangu nikupa ya deposit, si unipe. Inakuwa ni mkutano, ile pesa hupati.<br />
Kwa hivyo tungelipenda serikali iangalie hili jambo. Juu ukienda kwa watu wa lands tribunal wanakuambia ya kuwa hiyo sheria<br />
hakuna. Wanatambua wewe ulipe nyumba, hawatambui deposit. Hiyo pesa yako itakuwa nikuvutana ama pengine hata<br />
uwachane nayo. Umechukua transfer mbali kwa hivyo lazima Constitution yenye itakuja lazima iangalie hili jambo, tuweze<br />
kulindwa kwa hii mambo ya kulipa deposit.<br />
Jambo la pili ni kuhusu elimu. Unakuta ya kuwa tumekuwa na (inaudible) <strong>of</strong>fice ama divisional <strong>of</strong>fice. Hawa watu<br />
wanatengeneza bairo zao. Unakuta wana either ma-head teachers wanawaambia, tumepitisha hili. Na juu sasa ma-head<br />
teachers wako chini yao, akikataa kufuata, atapigwa transfer mahali penye hataki, inabidi afuate. Wanakuja na sheria<br />
wanasema, ni lazima watoto wafanye common exam division mzima. Ambapo kila shule itarokota pesa ipeleke kwa division.<br />
Ile ni pesa nyingi sana ukichukua shule zote karibu (inaudible). Ile pesa haujui inaenda wapi na wale watu<br />
wamelazimishwa, akikataa, transfer. Na ukienda kwa ministry wanasema hatutambui hio. Hamtambui lakini iko (inaudible)<br />
Sasa tufanye vipi? Lazima Katiba mpya iangalie hao watu wasi (inaudible) na divisional <strong>of</strong>ficers mambo ile<br />
wanafanya na ikuwe legalized na serikali ijue ile pesa inarokotwa inatembea kivipi.<br />
Jambo langu la mwisho ni kuhusu wanabiashara ambao wanajulikana kama jua kali. Jua kali wa sasa Kenya unakuta<br />
umepelekea mtu fulani vile mzee alikuwa ameongea. Umepelekea mtu vitu. Atatafuta kakosa kadogo, anakuruka kukulipa.<br />
Akisha ruka kukulipa, yeye anapesa ya kwenda kuchukua advocate vile yule mzee alivyokuwa ameongea tu. Ni wewe hauna<br />
22