28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

tungeomba Serikali itie nguvu sheria ya Mwenyezi Mungu haifutiki lakini itie nguvu Serikali zile masharti zifuatwe za kuachwa na<br />

za kuoa.<br />

Jambo jingine, sisi kina mama ndio tuanaopata shia katika community yaani katika jamii. Mama mimi nitazaa, niwalee watoto<br />

wangu, wakue, bahati nzuri wapate kazi. Ikiwa ni mume aoe yule bibi hata sitaangaliwa, nimefika umri wa kizee lakini mtoto<br />

wangu yeye na bibi yake tu, hajui kama mama amezeeka anahitaji msaada.<br />

Ningeomba Serikali itoe jukumu ya kuwa kuwe na percentage fulani, mama wakifika awe kama watoto wake wanafanya kazi<br />

awe akipatiwa hizo pesa. Kwa maana, kina mama wengi wanapata shida na watoto wao wanafanya makazi makubwa,<br />

makubwa, wana magari lakini ukiangalia mamake na ile hali aliyo, imekuwa ya kusikitisha sana.<br />

Lingine sisi kina mama wa Mombasa hapa tunatumiwa kama vyombo vya kupiga kura, baada ya kura imekwisha. Hatupewi<br />

nafasi ya sisi kina mama kujiendeleza. Tukiwa na shida zetu tukiingia kwenya ma<strong>of</strong>isi ya Serikali, ikiwa huna kitu kidogo hutiliwi<br />

sign ujekupata kitambulisho, kwa chifu husikizwi kesi yako, kila kitu wewe mama ni lazima utoe kitu kidogo. Kwa hivyo sisi<br />

kina mama sasa tunataka haki utukike kutoka nyumbani kwa mzee aliyenioa mpaka kwa Serikali, itutambue.<br />

Jambo jingine ambalo sisi kina mama tunadhulumika, kwa wazazi wetu. Wanaamini kuwa mtoto wa kiume ndiye anaridhi mji,<br />

lakini mtoto wa kiume yule hawaangalii wazazi. Mimi ndiye ninaweza kumbuka babangu amezeeka nikampelekea shati,<br />

mamangu amezeeka nikampelekea rinda lakini mtoto wa kiume akioa ni yeye na kwa bibi peke yake. Kwa hivyo uradhi utiliwe<br />

Serikali maanani kuwa mtoto wa kike aweze kumiliki kwa wazazi wake.<br />

(Clapping from the audience)<br />

Na recruitment katika Serikali, ianze kuanza (?). Kama ni polisi, ianze pale pale. Kuna Nyali, kuna Bamburi,<br />

lakini wakati wa kuandikishwa kazi unakuta watu wanatoka mahali kwingine, wanaletwa tu, hao ndio wamechaguliwa.<br />

Tunataka kila police station ku-recruit watu kutoka area ile, (Clapping from the audience) watoto wetu wapate kazi.<br />

Sisi kina mama tusiwe tu ni bendera ya kuwa yafuata upepo. Saa hii tuanataka tuwe tumekita chini kabisa! Mume anaye piga<br />

bibi yake kupita kiasi si lazima ati kuwa maneno ya mume na mke hayaingiliwi, sheria itumike pale, yule mume aulizwe kwa nini<br />

amempiga bibi yake viel. Sio kusema ati umepigana na bwana yako wewe, hiyo ni shauri yako, hatutaki, tunataka tujue haki<br />

zetu.<br />

Na hapa Coast, hizi polytechnics, iwe nafasi za kwanza zinapewa watoto wa Coast ambao zile polytechnic ziko. Lakini utakuta<br />

watoto wa Coast waki-apply wanaambiwa nafasi hakuna ama amefeli ama hakupasi vizuri. Tatizo hilo tuachieni kila watu na<br />

sehemu zao wamiliki, wajisikie na hao ni raia wa nchi ile. Asante sana.<br />

27

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!