verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Na umri, awe na miaka arubaini na mitano mpaka sitini na mitano. Aki zidi hapo mara ingine akili zitarudi chini. Ijabo wale<br />
wazee walioko wasinielewe vibaya.<br />
Kwa hivyo nina mengine mengi. Tukiija kwa swala ya ardhi, tungeipendekeza kwamba tunasikia, hatuja jua vizuri kwamba<br />
mwananchi anapo pewa ardhi, zake ni futi tano kwenda chini. Huko chini ya futi tano si kwake. Swala ni kwa nani?<br />
Tungelipenda nikipewa kipande cha ardhi hata kama ni futi elefu saba chini, kuwe ni kwangu. Kama kuna madini, yawe ni<br />
yangu, si ya Serikali. Swaha hilo tukikosa kuna fujo kule Kwale kwa sababu madini yako kule chini hayako futi nne. Report za<br />
Satenium inaleta shida kule chini.<br />
Kwa mambo ya uhuru, uandishi, tungelipenda uandishi wapewe uhuru, lakini yale wanaandika wengine yaleta shida. Sipende<br />
kuona picha ya msichana akiwa nusu uchi, na ni gazeti ile. Jameni majimbo tuyapenda lakini haya nao tuiangalie. Angalao tuwe<br />
na mulekeo mzuri. Ningeungana na wale wengine wanataka mavazi yawe mazuri kwa sababu ukivaa nusu uchi unavyo sivyo<br />
mno, kwa hivyo jameni nina mengine mengi, lakini karatasi iko ilio andikua Kizungu. Asante.<br />
Com. Wambua: Asante sana Rev. kwa hivyo jiandikishe huko na utupatie hio memorandum, tutaisoma. Kwa hivyo tutamuita<br />
Juma Kumala. Yuko? Ako wapi? Athumani. Haya kuja hapa Mzee Athumani. Tunakupa dakika mbili umalizie, unalizie<br />
mzee yale ya muhimu.<br />
Athumani Mbwana Kumala: Jina langu ni Athumani Mbwana Kumala. Mimi sina zaidi ya maneno. Yatakuja mzemaji lakini<br />
mimi nitasema kama maili tu.<br />
Jambo la kwanza naiomba, Tume hii itukatie mpaka baina ya Fiji mpaka huko Kisauni. Upande ule uwe Mombasa. Na kwa<br />
sababu? Maanake huku kwetu waliletua kule Mombasa hawaoni kuwa sisi ni viongozi wala sisi tuataka kuongoza. Hawajui.<br />
Wajua huku ni mashamba, hakuna watu. Lakini ilikua ni mashamba zamani lakini sasa mashamba ina watu. Kwa hivyo ukatua<br />
mpaka uwe huku pekee yake. Ikiwa ni Mbunge, awe wa huku, Councillor awe wa huku, hata kama atawakilisha Mombasa,<br />
lakini awe amechanguliwe sehemu ya Kisauni.<br />
Na huku Kisauni kuna matatizo mengi ya ardhi kwa sababu wenye ardhi wote wako Mombasa. Sasa huona sisi huku ni kama<br />
Manyani tu. Wakiija, waja kututembelea, washika njia waende zao. Lakini sasa tuataka funga mpaka wawe hawaji tena huku.<br />
Sisi wenyewe tuchukue ardhi zetu, tujitawale wenyewe.<br />
Jambo la pili kwa kusemea hivo kuwa mpaka ukatue wale wa kule hawajui kama huko Kisauni kuna Waislamu, wafrica<br />
hawajui. Waona kule hakuna Muislamu hata mmoja. Na kosa hili inatokana na Serikali pia tukisema. Maanake Serikali<br />
aitambui mtu. Muisalim, Mafrica, yeye kila akiangalia aona Mwarabu ndio Muislamu. Hata kame ni myaudi, lakini mweupe ni<br />
66