28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Na umri, awe na miaka arubaini na mitano mpaka sitini na mitano. Aki zidi hapo mara ingine akili zitarudi chini. Ijabo wale<br />

wazee walioko wasinielewe vibaya.<br />

Kwa hivyo nina mengine mengi. Tukiija kwa swala ya ardhi, tungeipendekeza kwamba tunasikia, hatuja jua vizuri kwamba<br />

mwananchi anapo pewa ardhi, zake ni futi tano kwenda chini. Huko chini ya futi tano si kwake. Swala ni kwa nani?<br />

Tungelipenda nikipewa kipande cha ardhi hata kama ni futi elefu saba chini, kuwe ni kwangu. Kama kuna madini, yawe ni<br />

yangu, si ya Serikali. Swaha hilo tukikosa kuna fujo kule Kwale kwa sababu madini yako kule chini hayako futi nne. Report za<br />

Satenium inaleta shida kule chini.<br />

Kwa mambo ya uhuru, uandishi, tungelipenda uandishi wapewe uhuru, lakini yale wanaandika wengine yaleta shida. Sipende<br />

kuona picha ya msichana akiwa nusu uchi, na ni gazeti ile. Jameni majimbo tuyapenda lakini haya nao tuiangalie. Angalao tuwe<br />

na mulekeo mzuri. Ningeungana na wale wengine wanataka mavazi yawe mazuri kwa sababu ukivaa nusu uchi unavyo sivyo<br />

mno, kwa hivyo jameni nina mengine mengi, lakini karatasi iko ilio andikua Kizungu. Asante.<br />

Com. Wambua: Asante sana Rev. kwa hivyo jiandikishe huko na utupatie hio memorandum, tutaisoma. Kwa hivyo tutamuita<br />

Juma Kumala. Yuko? Ako wapi? Athumani. Haya kuja hapa Mzee Athumani. Tunakupa dakika mbili umalizie, unalizie<br />

mzee yale ya muhimu.<br />

Athumani Mbwana Kumala: Jina langu ni Athumani Mbwana Kumala. Mimi sina zaidi ya maneno. Yatakuja mzemaji lakini<br />

mimi nitasema kama maili tu.<br />

Jambo la kwanza naiomba, Tume hii itukatie mpaka baina ya Fiji mpaka huko Kisauni. Upande ule uwe Mombasa. Na kwa<br />

sababu? Maanake huku kwetu waliletua kule Mombasa hawaoni kuwa sisi ni viongozi wala sisi tuataka kuongoza. Hawajui.<br />

Wajua huku ni mashamba, hakuna watu. Lakini ilikua ni mashamba zamani lakini sasa mashamba ina watu. Kwa hivyo ukatua<br />

mpaka uwe huku pekee yake. Ikiwa ni Mbunge, awe wa huku, Councillor awe wa huku, hata kama atawakilisha Mombasa,<br />

lakini awe amechanguliwe sehemu ya Kisauni.<br />

Na huku Kisauni kuna matatizo mengi ya ardhi kwa sababu wenye ardhi wote wako Mombasa. Sasa huona sisi huku ni kama<br />

Manyani tu. Wakiija, waja kututembelea, washika njia waende zao. Lakini sasa tuataka funga mpaka wawe hawaji tena huku.<br />

Sisi wenyewe tuchukue ardhi zetu, tujitawale wenyewe.<br />

Jambo la pili kwa kusemea hivo kuwa mpaka ukatue wale wa kule hawajui kama huko Kisauni kuna Waislamu, wafrica<br />

hawajui. Waona kule hakuna Muislamu hata mmoja. Na kosa hili inatokana na Serikali pia tukisema. Maanake Serikali<br />

aitambui mtu. Muisalim, Mafrica, yeye kila akiangalia aona Mwarabu ndio Muislamu. Hata kame ni myaudi, lakini mweupe ni<br />

66

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!