verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Irene Randu: Na ikiwa wataondoka katika hayo makao warudi mabarabarani wachukuliwe hatia. Sheria iruhusu wakina<br />
mama nafasi ya kuamua ni watoto wangapi wanataka kuwazaa kulingana na afya zao sio kushurutishwa ataje majina mbari<br />
nzima. Lazima waislamu wapewe wakina mama wakili wao ambaye atakaye simamia haki za watoto na wakina mama ambao<br />
wamemchagua wao wenyewe.<br />
Uandikishaji wa kupiga kura uwe ni wa kuendelea kwa sababu mda ya kujiandikisha kura hujulikani, kuwe na <strong>of</strong>isi maalum za<br />
kujiandikisha. Wananchi wana<strong>of</strong>ikisha umri wa kujiandikisha waweze kujiandikisha mahali popote wakati wowote. Kuwe na<br />
women desk katika ma-police station na hospitali zetu tumesema ziwe bure kwa sababu hali ya vifo na maradhi ni mengi sana,<br />
imeweza kutuadhiri sana ki uchumi. Uradhi, siku bwana akimwacha mkewe, mali yao yagawanywe nusu kwa nusu manake bibi<br />
pia amechangia katika kujenga hio nyumba. Mwanamume akinajisi mtoto mdogo, sehemu zake za siri ziweze kuwa castrated<br />
manake hukumu anayopewa ni ndogo sana ndio maana wanaendelea kila siku. Baba akimruka mama kuwa mtoto si wake,<br />
kuwe na sheria za kupimwa damu ili mzee huyo aweze kusimamia malezi ya huyo mtoto. Kuwe na koti ya uamuzi ya wakina<br />
mama, mila ya kuridhi mwanamke ikomeshwe, miji Kenda nao pia wanalia sana pamoja na mila zingine ambazo zinazidi kuleta<br />
mateso, mila ndogo ndogo za mama ameolewa, siku akiachwa anaambiwa arudishe mahari na yule bwana hawezi kumrudishia<br />
uzuri wake na usichana wake. Bibi na bwana wakiachana, mke na nume wakiachana, watoto wakiwa wako chini ya umri wa<br />
miaka kumi na nane waachiwe mama yao katika nyumba ile ile walio lelewa. Yule mume akiwa amepata mke mpya, aende<br />
akaanze boma jipya. Kuwe na tume speciali katika hospitali ambazo zitaangalia malalamiko ambayo tuko nayo, unaeza<br />
kwenda mama kuzaa hospitali na mtoto wako akadhuriwa kwa sababu ya ujeuri ulioko katika mahospitali, mtoto akaangushwa,<br />
akawa mlemavu na hakuna mahali tunaweza kupeleka hayo mashtaka. Na tabia ya wazazi, ikiwa ni baba au mama kuingilia<br />
ndoa za watoto wao zikomeshwe kwasababu hao ndio wanazidisha talaka na watoto wengi wanaadhirika kwa sababu ya ndoa<br />
kuvunjika ovyo ovyo.<br />
People: ....................................................(inaudible)<br />
Irene Randu: Na baba wa kambo na mama wa kambo pia waulizwe wazi wazi ikiwa hawawezi, mzazi wowote kulea<br />
mtoto wa mwenziwe aseme wazi wazi kuliko kumfanyia mateso. Tumesema natural resources ziweze kusaidia katika province<br />
zinakotoka kwa hivyo zitatusaidia kutokana kwa upande wa elimu, hospitali na mambo mengine. Ukatili katika majela hasa hizi<br />
juvenile courts za watoto wetu<br />
Com. Wambua: Summarize tafadhali, nimekupatia muda<br />
Irene Randu: sisi tumeketi kutoka asubuhi na kina mama tumedhulumiwa na mumetuonyesha wazi hapa. Ukatili<br />
undolewe katika jela za watoto wetu<br />
Com. Wambua: Mama................................(inaudible) tafadhali mama<br />
103