28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Irene Randu: Na ikiwa wataondoka katika hayo makao warudi mabarabarani wachukuliwe hatia. Sheria iruhusu wakina<br />

mama nafasi ya kuamua ni watoto wangapi wanataka kuwazaa kulingana na afya zao sio kushurutishwa ataje majina mbari<br />

nzima. Lazima waislamu wapewe wakina mama wakili wao ambaye atakaye simamia haki za watoto na wakina mama ambao<br />

wamemchagua wao wenyewe.<br />

Uandikishaji wa kupiga kura uwe ni wa kuendelea kwa sababu mda ya kujiandikisha kura hujulikani, kuwe na <strong>of</strong>isi maalum za<br />

kujiandikisha. Wananchi wana<strong>of</strong>ikisha umri wa kujiandikisha waweze kujiandikisha mahali popote wakati wowote. Kuwe na<br />

women desk katika ma-police station na hospitali zetu tumesema ziwe bure kwa sababu hali ya vifo na maradhi ni mengi sana,<br />

imeweza kutuadhiri sana ki uchumi. Uradhi, siku bwana akimwacha mkewe, mali yao yagawanywe nusu kwa nusu manake bibi<br />

pia amechangia katika kujenga hio nyumba. Mwanamume akinajisi mtoto mdogo, sehemu zake za siri ziweze kuwa castrated<br />

manake hukumu anayopewa ni ndogo sana ndio maana wanaendelea kila siku. Baba akimruka mama kuwa mtoto si wake,<br />

kuwe na sheria za kupimwa damu ili mzee huyo aweze kusimamia malezi ya huyo mtoto. Kuwe na koti ya uamuzi ya wakina<br />

mama, mila ya kuridhi mwanamke ikomeshwe, miji Kenda nao pia wanalia sana pamoja na mila zingine ambazo zinazidi kuleta<br />

mateso, mila ndogo ndogo za mama ameolewa, siku akiachwa anaambiwa arudishe mahari na yule bwana hawezi kumrudishia<br />

uzuri wake na usichana wake. Bibi na bwana wakiachana, mke na nume wakiachana, watoto wakiwa wako chini ya umri wa<br />

miaka kumi na nane waachiwe mama yao katika nyumba ile ile walio lelewa. Yule mume akiwa amepata mke mpya, aende<br />

akaanze boma jipya. Kuwe na tume speciali katika hospitali ambazo zitaangalia malalamiko ambayo tuko nayo, unaeza<br />

kwenda mama kuzaa hospitali na mtoto wako akadhuriwa kwa sababu ya ujeuri ulioko katika mahospitali, mtoto akaangushwa,<br />

akawa mlemavu na hakuna mahali tunaweza kupeleka hayo mashtaka. Na tabia ya wazazi, ikiwa ni baba au mama kuingilia<br />

ndoa za watoto wao zikomeshwe kwasababu hao ndio wanazidisha talaka na watoto wengi wanaadhirika kwa sababu ya ndoa<br />

kuvunjika ovyo ovyo.<br />

People: ....................................................(inaudible)<br />

Irene Randu: Na baba wa kambo na mama wa kambo pia waulizwe wazi wazi ikiwa hawawezi, mzazi wowote kulea<br />

mtoto wa mwenziwe aseme wazi wazi kuliko kumfanyia mateso. Tumesema natural resources ziweze kusaidia katika province<br />

zinakotoka kwa hivyo zitatusaidia kutokana kwa upande wa elimu, hospitali na mambo mengine. Ukatili katika majela hasa hizi<br />

juvenile courts za watoto wetu<br />

Com. Wambua: Summarize tafadhali, nimekupatia muda<br />

Irene Randu: sisi tumeketi kutoka asubuhi na kina mama tumedhulumiwa na mumetuonyesha wazi hapa. Ukatili<br />

undolewe katika jela za watoto wetu<br />

Com. Wambua: Mama................................(inaudible) tafadhali mama<br />

103

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!