verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
alternative government for the people <strong>of</strong> Kenya when the government <strong>of</strong> the ruling party looses the legitimacy. Mwisho kabisa,<br />
viama vya upinzani vinapaswa kupewa haki zifuatazo za katiba ili viweze kufanya kazi yake vizuri; kwanza wawe na radio yao<br />
na television yao ili kuendeleza sera zao. Pili, wawe wanaweza kufanya mikutano ya kisiasa katika sehemu yoyote ya Kenya<br />
bila kutatizwa na polisi na kunyanyaswa kwa njia yoyote. Asanteni sana.<br />
Com. Wambua: Asante, tupatie memorandum na ujiandikishe pande hio. Sasa tutampatia nafasi.....................(inaudible)<br />
jina lakini ungojee tu. nitamwita mama mmoja Nuru Said. Huko wapi Nuru, kuja hapa mama tafadhali, chukua muda wa<br />
dakika mbili tu utupatie maoni yako halafu tuendele<br />
Nuru Said: Hamjambo nyote, mimi Nuru Said natoko Kongoea. Maoni yangu kuhusu kina mama wapewe haki zao.<br />
Kina mama sisi twanyanyaswa sana kuhusu pahali popote tunapokwenda kuwa hatuna uwezo wa kuzungumza jambo lolote na<br />
kuhusu kama polisi pale, lazima tuwe na meza yetu kina mama. Jambo jingine ni kuhusu hapa pwana; pwani sisi watu wa pwani<br />
twanyanyaswa ingawa pwani ni yetu, lakini twanyanyaswa sana. tukitaka kwenda maskuli kama hii polytechnic, mimi nina<br />
watoto wangu wengi karibu watatu, tungienda kwenye polytechnic twambia tungojee advertisement. Na wengi sana ni watu wa<br />
kutoka juu. Twataka sisi, 90% kutoka hapa pwani wachukuliwe na hilo ilobakia 10% wachukuliwe watu wa kwengine. Na<br />
kuhusu port pia, sisi leo watoto wetu wanakaa vikundi vikundi, hakuna watoto wanaokwenda kule port kupata kazi kwa<br />
sababu watu wa bara ndio wao wakubwa kule. Watu wa bara ndio wachukuliwe, mtu yuko bara kule atakaa miaka yote, akija<br />
akimaliza skuli moja kwa moja yuangia wapi, kazini. Sisi watoto wetu wakaa magarden halafu ambao watoto wa pwani<br />
wavivu, watoto wetu hawasomi, hawaendi university. Hawana nafasi university kabisa, pwani hii yetu haina university hata moja<br />
na ambayo ni city sasa. Kuna city itakosa university? Kwani watoto wetu hawasomi? Watoto wetu wasoma sana, tena<br />
werevu sana lakini sasa kuanzia sasa, mimi maoni yangu nataka watoto wetu, mitihani yao zifanyiwe hapa hapa, zisiende juu.<br />
Kwa sababu kule kule juu ndiko wanakoangushwa. Wakija hapa, watoto wetu ambao waseja hawana university. Kuna<br />
watoto hawapata grade za A wakienda kule wa pewa business. Mtoto anasoma hapa anapata grade A halafu aende university<br />
bara, apewe business tena si kwa kutaka yeye mwenyewe, yeye ataka kama doctor, nini lakini akifika hapa, akifika kule<br />
abadilishiwa moja kwa moja. Na hio iko, nishaona hapa hapa ambapo ni mtoto wetu, ni mmoja katika.. Mimi kila<br />
ninalozungumza ananipata mimi mwenyewe. Kuhusu COast General, Coast General hapa, watoto wetu wakiandikisha form,<br />
wasichana wetu wawe ma-nurse, wakienda kule wabaguliwa, zao zawekwa kando, ishajulikana Mariamu, Fatuma wao, sisi<br />
twataka hapa hapa mkoa wetu uwe hapa hapa, majina ya watoto wetu yachaguliwe hapa hapa. Na kuhusu hizi beach, beach<br />
hizi zote wafanyikazi wote ni watu wa bara. Wote kwanzia Manager mpaka wa chini, mpake watchmen wa nje mlangoni ni<br />
watu kutoka juu. Utakuta Mohamad na Salim wawili. Mimi leo nitazungumza mambo mengi manake yaniumiza roho yangu.<br />
Na kuhusu polisi kushika shika watu ovyo ovyo, pia hatutaki<br />
Com. Wambua: Tafadhalini tufanye heshima kwa mama, tumpatie nafasi atoe maoni yake<br />
Nuru Said: Kuhusu mapolisi, mtu mama kama mimi mtu mzima nikiota, pengine natoka harusini au natoka kwa watoto<br />
98