28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

pesa. Sasa ile process ya kuenda kushtaki yule mtu ni ghali na wewe yule mtu mwenye jua kali hana hiyo pesa. Sasa unakuta<br />

yule mtu amedhulumiwa na yule tajiri. Kwa hivyo tena hiyo sheria lazima iangaliwe ikiwa hawa watu watawekewa sheria<br />

ambayo itawasaidia. Ikiwa hana pesa, atasaidiwa vipi ili kwenda kuitisha pesa zake.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Nashukuru. Toa hiyo makaratasi yako. Kaboga Mbeji halafu anafuatwa na (sentence<br />

incomplete)<br />

End <strong>of</strong> Tape 1<br />

Speaker: Sasa ningependa kuzungumzia swala la Katiba. Nina uhakika watu wengi sana mitaani hawajui mambo ya Katiba<br />

yatakayo badilishwa wapi? Katiba yawaathiri vipi? wao wanaambiwa waje watoe maoni hali ya kuwa hawajui ni wapi ya<br />

wagusa. Kwa hivyo Serikali ingefanya mpango wa kuwa, japo mara mbili kwa wiki swala la Katiba lingekuwako la tangazwa.<br />

Watu wanafanya kuelezwa kwamba Katiba yetu ya sema hivi, kipenge hiki cha sema vile. Watu wapate kuelewa kwamba<br />

Katiba ya Kenya iko hivi na inamsaidia raia wake hivi na inamuumiza hivi. Ndio pale watu wakija kaa wakiamua wajadili<br />

Katiba, watakuwa wanajua manazungumza kitu gani.<br />

Swala la pili ni hili la uandikishaji wa kura. Swala la uandikishaji wa kura ingekuwa ni ubora pale mtu anapochukua<br />

kitambulisho, apewe kabisa kadi yake ya kura. Hino itazuia mambo ya kuchukua watu kutoka mji mwingine kuja kuwaleta<br />

waje kuchukulie kura ili ya kuwa wakupitishe, na hali ya kuwa wao si wakaaji wa pale. Na kabisa swala hili litakuwa pia<br />

linapunguza gharama la kwamba kila mwaka ikifika wa kura inakuwa mpaka lazima kuwekwa watu wa Commissioner ya<br />

kuandikisha kura, inakuwa ni pesa zingine zinatoka kwa Serikali kuwalipa wale na hali ya kuwa ni tax tunalipa sisi wananchi,<br />

tunaulizwa kwa kila kitu.<br />

Swala la tatu ni hawa waraia wa makaratasi, ‘citizens by papers’. Hawa ‘citizens by papers’ tunaona kama nchi kama America<br />

vile, wao hawaruhusiwi kupiga kura wala kuchukua kura. Ningependekeza na hapa kwetu swala hilo pia liweko maanake<br />

hawa ndio wanakuwa na influence ya kutuumiza sisi kimawazo, kifikira na kihali ya uchumi. Kutokamana na nguvu zao za centi.<br />

Swala lingine ambalo Ningependekeza ni kwamba, hao wanaogombea ubunge. Lau mtu amepata term yake ya kwanza,<br />

a-serve term mbili peke yake, yaani kipindi cha miaka kumi. Baada ya miaka kumi ile, haruhusiwi tena kugombea ule ubunge<br />

kwa sababu atakuwa akili yake sasa imeshazorota kimaendeleo. Atakuwa sasa yeye ni mtu wa kujinufaisha matumbo yake na<br />

kugandamiza wananchi. Hakuna moja atakalo kufanyia! Mfano mzuri twaona Mvita uko.<br />

Swali lingine ambalo ningependa kuzungumzia ni hili wazungu wasema ‘justice delayed is justice denied.’ Serikali yetu kwa<br />

uhakika ina centi za kutosha na hapa kutokana na kwamba ina centi za kutosha, ingeongeza idadi ya Mahakimu, hawa<br />

Magistrates. Wangeongezwa wakawa wengi na kukawa na transparency ya zile kesi. Sio mtu leo askari anamshika,<br />

amemwona kabisa akitoka dukani, anamuuliza watoka wapi, unaenda wapi? Si ananiona mimi ninatoka dukani ninaenda<br />

23

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!