28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

kushuhudia kwamba hapana Mola apasae kuabudiwa ila Mwenyezi Mungu pekee yake. Na pia kuamini vitabu ambvyo<br />

Mwenyezi Mungu aliviteremsha kama zaburi, taurashi na injili na mitume wote wa Mwenyezi Mungu ambao walitumwa kuja<br />

kuleta ujumbe, huu ndio uislamu. Na muislamu ni mtu yeyote awe mkikuyu, awe mnandi, awe mjaluo, awe mzungu au ni mtu<br />

gani, ndio uislamu. Lakini sio hii defination iliyotolewa hapa.<br />

Na kwa hivyo wakati wa kufanya drafting ndio mimi nasema haya makabila kwa sababu yalikuwa under British Protectorate,<br />

makabila haya ya kiswahili yaorodheshwe pamoja na makabila mengine arubaine na mbili ya Kenya ambayo yalikuwa<br />

yanahesabiwa bila ya upendeleo.<br />

Sasa katika proposal yangu katika hii wakfu commission pia, nasema Chief Kadhi achaguliwe mtu ambaye ana elimu ya<br />

secondary school. Na katika elimu ya dini awe amesoma ni graduate, awe na masters degree katika elimu ya dini. Halafu <strong>of</strong>isi<br />

hii hii ya Chief Kadhi, iwe extended mpaka katika High Court, appeal zozote za kislamu zisikizwe na Maula wa Kislamu wawe<br />

ndio wanasimamia katika hizo appeal. Na vile vile nikirudi katika mambo ya vitambulisho, majina ya waislamu kama Omari,<br />

Abdala ni majina yameridhiwa tangu zamani. Kwa hivyo isiwe ndio sababu ya watu kukataa kupewa vitambulisho kwa sababu<br />

hawana majina mengine kama Katana sijui nani nani. Haya pia ndio tunapendekeza yasifwatwe haya, maana yake haya majina<br />

yame-exist hapa tangu katika karne ya miaka mia mbili hasa ukristo ulikuwa haujaingia haya majina yalikuweko. Kwa hivyo<br />

sasa ndio tunasema pendekezo hili waisilamu tu-set tukisumbulia. Kwa mfano mswahili ikienda kwa vetting hapa katika<br />

kuchukua kitambulisho, anakuaamba haya makabila hayako, na haya makabila yalitajwa katika wakfu commission. Makosa ni<br />

ile serikali haikuchukua makabila haya yakawaweka pamoja na makabila mengine kwa sababu walitoka katika nchi nyingine<br />

ambayo ilikuwa ni British Protectorate.<br />

Na katika mambo ya uraia mimi nimependekeza pia kama mwenzangu alivyo tangulia kusema mtu yeyote aliye zaliwa katika<br />

nchi hii, apewe kitambulisho bila ya kuambiwa aandamane na mama yake na baba yake. Hili jambo ni ukoloni wa kisasa<br />

ambao unaletwa ambao hatuutaki. Mtoto yeyote akiwa na birth certificate, apewe kitambulisho bila ya kuulizwa baba wala<br />

mama. Kwa hivyo mimi yangu ni mengi nilioandika sitaki kuchukua mda na karatasi zangu ndio hizi hapa ninapeana.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Mzee ujiandikishe kule halafu utupe (inaudible) Dominic Omidi Awuor.<br />

Dominic Abwuor: Asanteni sana macommissioner na wananchi wenzangu. Asubuhi ya leo imekuwa ni fursa nzuri.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Sema majina yako.<br />

Dominic Abwuor: Majina yangu ni Dominic Ongundi Abwuor ambapo kidogo yamesomwa kwa makosa kidogo,<br />

nitarekebisha pale.<br />

7

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!