28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

anayetoa ardhi. Yaani tunataka mtu wa, kama ni mtu wa bara amiliki ardhi bara, mtu wa pwani kwao ili kila mtu awe ana haki<br />

sawa. Maana yake utapata mahali kwingine watu, mtu amezaliwa pale, babu yake amezaliwa pale lakini hana ardhi,<br />

inasemekana sijui mtu fulani kutoka mahali kwingine yeye ndie ana acre mia tatu, na yule mtu wa pale hana. Kwa hivyo<br />

tungeomba hii Katiba iweze kuangalia maswala kama haya. Naona ni hayo tu.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Asante. Unaweza kutoa haya maandishi yako kule na ujiandikishe. E.K. Ngutu. Ngutu<br />

anapokuja nataka John Mcharo awe tayari. Okay chukua nafasi, na Mcharo yuko? Okay akimaliza itakuwa wewe.<br />

Ephantus Ngutu: Kwa majina naitwa Ephantus Kathanka Ngutu. Mimi maoni yangu ni kuhusu wizi. Wizi umeongozeka sana<br />

katika nchi hii. Na mimi nilikuweko wakati wa mkoloni mpaka uhuru tukapata, lakini kwa wakati huu ambaye ni wa uhuru, wizi<br />

umeongezeka sana. Mimi kwa maoni yangu, ninaonelea, watu siku hizi wanapora mali ya uma, pesa za uma, zinaibwa na watu<br />

wawili ama mtu mmoja. Mamilion ya pesa. Mtu yule anapopelekewa mashtaka, badala ya kupelekwa rumande, anaruhusiwa<br />

kuweka bond. Anatoka, sasa anaenda kutumia zile pesa kuweka mawakili mpaka kesi yake itakapoisha. Akipatwa na hatia,<br />

anafungwa kama miaka miwili, anakuja anaanza kutumia hizo pesa za uma. Kwa hivyo maoni yangu ni kwamba kama mtu<br />

anahusika na kuiba pesa za uma, asiruhusiwe kuweka bond. Siku hizi utaona mtu akiwa na pesa anaweza kumyanganya mtu<br />

ambaye hana pesa mali yake. Na atamnyanganya kwa njia gani? Yeye kwa vile ana pesa, atamwekea yule mtu hata mawakili<br />

kumi. Na yule maskini hana pesa, ama pengine ni shamba lake na shamba hilo, ni hilo hilo analo na atanyaganywa na yule mtu<br />

ambaye ana pesa. Kwa hivyo katika Katiba hii ambayo tunaiita ni ya Mwafrika maanake hii ilikuweko, hiyo ilioko sasa ni ya<br />

kizungu, kuwe na sheria kwamba iangaliwe. Ikiwa mtu hana uwezo wa kuweka wakili, na yule ambaye wanashtakiana naye<br />

asiruhusiwe kuweka wakili, wangangane kwa sababu sisi ni waafrika na tukiwa waafrika, tumeiga sana mpaka ikawa mambo<br />

yetu yote tumebakia ngozi tu. Sasa hawa watoto wetu hawa, wamebakia ngozi tu. Hayo mambo mengine yote ni ya kizungu.<br />

Kwa hivyo mtu kama huyo na yeye asiruhusiwe kuweka wakili, wangangane. Wangangane bila wakili. Mimi sina mengi ila tu<br />

nawachia hapo. Asanteni.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Asante sana mzee. Ende kule ujiandikishe. Next atakuwa John Mcharo na John Mcharo<br />

anapojitayarisha nataka Salim Mwambala awe tayari. Unamaandishi?<br />

John Mcharo: Ee kidogo.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Kwa hiyo tumulikie.<br />

John Mcharo: Nina maandishi kidogo. Kwa jina naitwa John Charles Mcharo na nataka kuzungumzia mambo manne tu basi.<br />

Memorandum yangu ni kizungu lakini pale nitakapoweza, nitajaribu kueleza kiswahili. Kwanza nataka kuzungumzia <strong>of</strong>isi ya<br />

Rais halafu nitazungumzia kuhusu polisi, halafu nitazungumzia kuhusu serikali za wilaya yaani local authorities, halafu mwisho,<br />

nitamalizia na one or two general social issues. Kwanza nitaanza na <strong>of</strong>isi ya Rais.<br />

17

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!