28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

yake ni A, B, C. Chief haruhusiwi kuchukua pesa za harambee, Chief haruhusiwi kusikiza kesi ambayo inayoweza kwenda<br />

mahakamani, Chief haruhusiwi kusema wewe fanya hivi, kutoa instructions. Mambo ambayo yangepelekwa kotini, Chief<br />

anatoa judgement yake pale pale kwa kua amekula mbuzi mbili zimekuja, we should not have this in the Constitution. If the<br />

Chief has to be there, we should know exactly what the Chief is supposed to do. Akija akiniitisha mbuzi, nimwambie sikupi<br />

mbuzi, nataka unifanyia kazi yangu, mtoto wangu anataka kitambulisho na hupati mbuzi na hupati pesa za harambee.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Asante. Umebakisha dakika moja tu. Moja tu kwa hio ona vile ambavyo (inaudible)<br />

John Mcharo: Haya Police. Mimi ningesema polisi wapewe mshahara mzuri na pia wachukulie polisi waliyo soma. Saa hizi<br />

tuna polisi hawakusoma, mtu hakusoma amepewa bunduki, wanatuonea sana huku mitaani. Na ningetaka Mayor achaguliwe<br />

directly by the people. Na Mayor awe amesoma, amefika form four na ame-pass. Sio amefika form four na amepata E. Na<br />

mambo ya burials permit, wedding permits. Sisi tuko na matanga, tuko na mwili pale polisi wanaingia wanasema iko wapi<br />

permit. Permit ya nini unatuona tunalia na mwenzetu ndio yule pale amefariki? Harusi. Unaona bwana harusi na bibi harusi<br />

wako pale, polisi wanaingia wanasema lete permit. Permit ya kazi gani kwa shughuli kama hizi? Hatungependa mambo ya<br />

permit katika shughuli ambayo they are so obvious kama matanga na harusi.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Thank you.<br />

John Mcharo: I am not even half way.<br />

Com. Pastor Zablon Ayonga: Kuna watu wengi ambao wangependa kuongea na kwa hivyo lazima tuwe fair. Unaweza<br />

kwenda kule ujiandikishe na utupe maandishi yako. Omar Yahi. Endelea, sema majina yako na uendelee.<br />

Omar Yahi: Mimi ni Omar Z. Yahi. Maoni yangu kwa Tume hii ni kuhusu KWS ambayo inatunyanyasa sisi wananchi wa<br />

hapa na tunaona inatudhulumu sana. Nikisema hivi kama mimi nina port yangu kule na-chargiwa 400/= per person na KWS.<br />

Na mimi namcharge mgeni shilingi mia nane. Wakichukua mia nne nimebakishwa na mia nne. Mia nne ile nitatoa commissioner<br />

150 kwa (inaudible) nikabakiwa na 250. 250 nimlipe captain wangu 30% na ninunue mafuta, na nilipe nakruu, nikishtuka<br />

mimi nimebakiwa na (inaudible) KWS na sijui pesa zinakwenda wapi. Nawanachukua mamillion ya pesa kule, na<br />

sisi wananchi wa pale tumezorota, kulikuwa kuna ma-boat karibu arubaini, sasa zimebakia kama boat nne. Nyingine zimeoza<br />

zote. Nataka (inaudible) zaidi ya mia moja, sasa zimebakia kama kumi. Naona hapa tutaomba mtufikirie sana sisi<br />

wananchi wa hapa tunaponyanyaswa na KWS na hajui kitu chochote pale kuja kwake anakwita kama jibwa. Wakati<br />

umechukua mgeni ukija, yeye yuko juu huku anafanya kukuita, we kuja hapa. Unampelekea pesa za bure, na hawana heshima<br />

wala hawana (inaudible) vibaya sana. Kwa hivyo naomba maoni haya mwakilishe kwa makini maanake tuko katika hali<br />

mbaya, tumeshindwa kujimudu sasa kimaisha. Pesa zote zinaliwa na KWS na hatujui zinakwenda wapi. Ninaushaidi huku<br />

wakutosha si pesa kidogo, mamillion ya pesa wanachukua. Sio kama mimi kwa port kwa mwaka napata tisaini na tano elfu.<br />

19

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!