28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Kwa hivyo ninaomba serikali ijaribu sana kutufikiria sisi walemavu. Lingine, huu wakati ukifika wa kura, serikali ijaribu<br />

kutuweka karibu walemavu kama watano hivi kwenye bunge. Kidogo tutajisikia pia nasi ni watu. Sababu wale ndio watakao<br />

kuwa wakijua shida zetu, tutakuwa tukienda kwao, tunazungumza nao, tunawambia sisi bwana shida yetu ni hii na hii na kwa<br />

kuwa ni walemavu kama sisi, watatusikia, watatuelewa. Lakini saa hii hata ukienda kwa bunge useme ah basi kule walemavu<br />

hata, hata kwanza hawatakuelewa unazungumza kitu gani. Kwa sababu hakuna mlemavu pale ambaye anajua shida ya<br />

mlemavu. Lingine, katika hizi, tunaitaje hizi, hii mahospitali na, ma hospitali sana sana, tunataka tuwe na free, matibabu ya bure.<br />

kwa sababu walemavu wengin wakati huu kusema ule ukweli hawana uwezo. Na mlemavu aweza kuenda hospitali, ni<br />

mgonjwa kabisa na unamwona huyu mtu ni mgonjwa, lakini inabidi aambiwe atoe pesa. Hizo pesa atapata wapi na ni<br />

mlemavu? Na hana kazi yoyote yule mlemavu ukimfikiria hivi? Unamwambia atoe pesa, atatoa wapi hio pesa? Inabidi yule<br />

mlemavu apate msamaria mwema, asipo pata msamaria mwema, basi yake yanaisha na Mungu. Lingine ni kwa kuwa tujaribu<br />

kuangalia<br />

Com. Wambua: Tafadhali<br />

Peter Msiko: Kidogo nimalize<br />

Com. Wambua: Malizia tafadhali<br />

Peter Msiko: Lingine ni habari ya usafiri. Usafiri, serikali ijaribu kuangalia njia nyingine la kutengezea magari ambayo<br />

mlemavu anaweza kuingia bila matatizo. Hiyo nafikiri itatusaidia kwa njia nyingine. Asanteni sana<br />

Com. Wambua: Asante sana Peter Msiko. Jiandikishe hapo tafadhali, maneno yako yamepokelewa, tutayaangalia vilivyo.<br />

Tutamwita John Nyagaka na yeye pia atoe maoni yake na kwa sasa wale ambao wako na maandishi ama memorandum na<br />

walikuwa wamejiandikisha kutoa maoni, nawauliza walete hiyo memorandum hapa ama maandishi, tutaenda nayo na kabla ya<br />

kurudi hapa kupokea maoni. Kwa hivyo usiende na memorandum kama ulikuja nayo hapa kutupatia. Kwa hivyo kama kuna<br />

mtu yeyote ako na maandishi, alijiandikisha kutoa maoni atoe hapa halafu tutatangaza siku ya kurudi hapa kisauni. Endelea<br />

nanii, John.<br />

John Nyagaka: Wenzangu, habari ya jioni, kwa hakika ni furaha yetu<br />

Speaker: Sema majina<br />

John Nyagaka: Ya kwanza, majina yangu vile mumesikia naitwa Johnstone Nyagaka na ninafanya kazi huko Bombolulu<br />

workshops. Wengi wenu mnaijua na ningependa kuchukua hii fursa hakika kwanza kushukuru huu muda ambapo tumepewa<br />

sisi ili tupate kutoa maoni yetu kama walemavu. Na sijui kwa hakika hapa, vile tume kaa hiki kikao, ni mzazi ama ni wazazi<br />

108

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!