28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Ikiwa kazi yeyote inatokea kupeleka hata mtu wa Kenya nje, awe ni Mpwani-Mkenya harisi. Ndio tunaona, Mabalozi wetu<br />

ambao wanatoka hapa, wanatoka wageni tena, ndio wanaenda nchi za kigeni.<br />

Tukipata kwa wenye kuenda Tanzania – kwa Bunge, wanapeleka mgeni, na watu wa Kenya wanakaa hapa. Hiyo nilionelea,<br />

ikiwa mtu kama huyo anapenda kazi kama hiyo, hata akienda kwa councillor, hata akienda kwa Mbunge, awe mtu wa Kenya<br />

harisi. Na familia yake yote iwe ya Kenya.<br />

Com. Pr. Ayonga: Asante sana Mzee Okwiri. Huyo ni Okwiri. Sasa nataka mama Asha Athumani Juma. Asha Athumani<br />

Juma? Tafadhali tupunguze sauti, ili mama Asha Athumai Juma aanze. Mama unaweza kuanza, nimekupa dakika tatu tu.<br />

Wakati mama anapojitayarisha, nataka ……. Mama endelea.<br />

Asha Athumani Juma: Jina langu ni Asha Athumani Juma. Mimi Asha Athumani Juma, kilio changu ambacho<br />

nikachokitoa hivi leo, ni sisi Waislamu. Waislamu sisi, tunasema, wananchi wa hapa, tunataka tupate Jimbo letu. Na hili Jimbo<br />

letu nalo, tukishalipata, maanake, Jimbo ndio msingi tutakay<strong>of</strong>anya mambo yetu, au tuseme maneno yetu, ambayo yatajulikana.<br />

Jimbo hili tulilonalo hapa, maneno yote yashazungumzwa, yale nilikuwa mimi nataka kuzungumza. Lakini sasa, maoni yangu ni<br />

hivi. Hili Jimbo wakati tukishalipata hapa, tutakusanya zile pesa zetu zote zilizoweka hapa. Ikiwa ni airport, ikiwa ni kilindini,<br />

tukishazipata, robo tatu tutamia wenyewe kwa miradi yetu. Tutapata robo moja tukapeleka makao makuu, kwa sababu ile<br />

miradi, kisha tushapata ile Jimbo letu, na zile pesa robo moja tumepeleka kule, hizi robo tatu tutajenga ma-shule yetu, na halafu<br />

tukipanga mambo yetu, tutayapeleka makao makuu tupate kuidhinishwa kule. Halafu miradi ile, ndiyo tutakuja kuifanya hapa.<br />

Kuhusu serikali zetu, sisi wanawake wa Kiislamu tuna haki zetu. Na zile haki zetu hatujapatiwa, kina mama Wakiislamu,<br />

wakati unapokwenda kujifungua hospitali generali, unazalishwa na wanaume, na haki ya Kiislamu yakataza kabisa. Maanake<br />

mwanamke ukizaa, uko hali mbaya, uwezekani kwa kitabu chetu cha dini cha Mwenyezi Mungu, mwanamke kuonekana na<br />

waume wengine isipokuwa mumeo. Isipokuwa wataka uonekane na mumeo pekee.<br />

Kuna mwanaume wa Kiislamu, yuko pale, yuadungwa shindano na mwanamke ambaye pia hausikani, kidonda kiko pahali<br />

pabaya, yuaoshwa na mwanamke, ambaye hauzikani. Kwa hivyo, twataka sisi Waislamu, wanawake wazalishwe na Waislamu<br />

……………. (inaudible) wao, na Wanaume watipiwe na wanaume………. (inaudible) yao.<br />

Nikiendelea mbele, kuna ma-shule yetu. Ma-shule yale tulionayo, wanawake wa Kiislamu wasichana wavaa nguo fupi, skirt ya<br />

kufika hapa. Na Wanaume nao, ni siruari zao fupi. Twataka Waislamu wawe na mavazi siruari zao ndefu, ma-shirt ya mikono<br />

mirefu, mwanamke awe na “hijabu”. “Hijabu” mwanamke awe nayo, na mwanaume suruari ndefu na k<strong>of</strong>ia ya msikitini. Hapo<br />

tutakuwa tushatimia kwa Waislamu.<br />

53

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!