28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

wangu, wanisindikiza wanipeleka kwenye matatu, nikishuka nyumbani tu nashikwa. Msako, mama mimi mtu mzima pengine<br />

naitwa usiku, mjukuu wangu mgonja, narudi. Au ninasahau kitu dukani naenda nunua, ninashikwa. Nashikwa na msako mtu<br />

mzima mimi natafuta nini usiku huu nje hata nishikwa na msako. Hata nikimwambia, we mama wewe huna ID. Nitatokaje na<br />

ID mimi saa zote nitembee na ID, ikipotea? Na kuhusu vitambulisho watoto wetu, watoto wakizaliwa wawe na vitambulisho<br />

vitatu. Passport, birth na ID card. Hizo vitu vitatu lazima watoto, mimi maoni yangu, mtoto anapozaliwa. Na utakuta sisi<br />

wananchi wa hapa hatupati vitambulisho, watoto wetu wanyanyaswa, mtu ana leaving, ana certificate, mimi nina certificate<br />

nimemzaa, amesoma kutoka standard one mpaka form four, ambiwa mtoto yule bado si mkenya. Nakuhusu mzazi mmoja, mtu<br />

aweza kuzaa, mama aweza kuzaa, pengine baba mwenyewe hayuko au baba mwenyewe ashikanta gwara zake halafu mama<br />

akashika mimba. Akizaa yule mtoto anamlea mpaka anakuwa mtu mzima hata kumtolea ID mtoto huwa ni shida, amsumbua<br />

bababe; babake yuko wapi? utamptafuta wapi naye ashashika njia alikwenda zake?<br />

Com. Wambua: Asante, asante mama<br />

Nuru Said: Mimi nina maneno mengi<br />

Com. Wambua: Ndio nina ona mambo sasa yamechemka, lakini wacha nikuulize swali mama. Mama unasema mtoto<br />

akizaliwa, apatiwe ID, apatiwe birth certificate, apatiwe passport. Mama unajua, passport utapataje mtoto aliye zaliwa jana na<br />

ambaye hawezi kuweka sahihi?<br />

Nuru Said: Mzazi wake anaweka<br />

Com. Wambua: Kweli atawekaje, kwa ID ataweka aje kidole na aweke na sign yake, katoto kaliko zaliwa? Au unataka<br />

kumaanisha hivi, mtoto akizaliwa, ndio birth certificate anaweza kupewa kwa maana ni ya baba na mama lakini hivyo vitu<br />

vingine akimaliza miaka yake ile kumi na nane, apewe. Lakini kusema akizaliwa apewe hivyo vitu, mimi ninaona unauliza<br />

ambacho hakiwezekani.<br />

Nuru Said: Right, haiwezekani, lakini twaomba<br />

Speaker: Mwambia ni sawa<br />

Nuru Said: Ni sawa lakini tusisumbuliwe sisi, manake hasa rangi hii mimi nasema wazi, tunasumbuliwa sana na ID na<br />

passport. Vitu hivi viwili vinatuumiza sana, mimi nina mtoto wangu 27, mpaka leo hajapata ID.<br />

Com. Wambua: Mama, haya ni maoni yako. Ikiwezenaka, mtoto akizaliwa apewe birth certificate, passpot na ID<br />

pamoja. Haya ni maoni yako. Asante sana mama, jiandikishe hapo tafadhali. Kwa hivyo tutamuita hapa kabla hatujaita mama<br />

99

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!