verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Sisi hapa tulipo na Wakenya wote, hakuna mtu asiye na kabila. Mambo machifu katika nchi yetu yameletwa na uchoyo, na<br />
mambo mabaya. Usiseme huna kabila, kabila bado liko na kila kabila ina nia zake, ina madesturi yake. Kwa hivyo kuondoa<br />
haya yote, tunauliza Serikali ile ya mwanzo, Serikali ya majimbo.<br />
(Clapping from the audience)<br />
Tunataka kuondoa P.C. Huu ni mpango wa Serikali. Nani anataka P.C? Nani anataka D.C? Nani anataka chief? Nani<br />
anataka mambo yote hayo? Hatujawachagua hawa watu, kwa hivyo hatuna haja nao.<br />
Katika Serikali ya majimbo, tunataka vyama vinane, kila jimbo na chama chake. Ma-commissioner, mkifanya kazi yenu,<br />
tunataka idadi ya wale wameshiriki katika badiliko la Katiba. Hapo tutajua ukweli, ikiwa Katiba ilikuwa ya wananchi au<br />
ilikuwa ya Serikali ya KANU.<br />
Pia, katika elimu, tunataka nini, tunataka Katiba ienezwe kila pahali. Hospitali, kuna mama wengine hapa hata Pwani na kila<br />
pahali. Utakuta mama, yeye ni mwenye kichaa lakini mama yule ukimwangalia pia utamkuta yuko na mimba. Akifika hospitali,<br />
anarushwa rushwa huku, anaraushwa rushwa huko, haeleweki. Kwa hivyo, wale ambao wako na kichaa, wakina mama ambao<br />
wako na kichaa na wako na mimba, tafadhali Katiba ije na mtindo mwema wa hudumiwe.<br />
Disabled, hawa ni watu wetu. Zamani tulikuwa hatujui lakini sasa naomba katika Katiba wajengewe ma-estate yao ambayo<br />
watakuwa kule, wawe na infrastructure zao, tunajua pia wanataka viti, tunataka ma-crutches. haya ni mambo ya kupewa bure,<br />
kwa maana tunafahamu Serikali iko na pesa na iko na pesa kweli kwa maana hata commissioner pale, zile anachukua pia sio za<br />
kawaida.<br />
Mbunge: Mbunge wa kulala hatuna haja naye. Kwa hivyo mimi nina-propose, mbunge yeyote ambaye hafanyi kazi yake sawa,<br />
wananchi wale wale wamepiga kura, wawe na uwezo through the Ombudsman wa kumwita na kumfuta kazi.<br />
(Clapping from the audience)<br />
Tatu, mayor achaguliwe na wananchi. Local Government yetu iwe ni ya wananchi wenyewe. Hapa tumesema tunataka<br />
majimbo kwa hivyo hatuna haja na Rais, tuko na haja na Prime Minister. Prime Minister kazi zake ninampatia ni tatu tu.<br />
Defence, taxation and foreign affairs.<br />
Majaji, tutawaandika sisi wenyewe katika region kwa maana tumesema majimbo. Kwa hivyo katika majimbo tunataka<br />
governor na ma-senator ambao kila mtu atamchagua kutoka jimbo lake. Prime Minister ni mmoja tumesema na ikiwa tunataka<br />
kuwakilishwa, tutachagua wenyewe huyo Prime Minister.<br />
30