verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
(Interjection) Com Pastor Zablon Ayonga: Lakini swali ambalo Commissioner anakuuliza, kwamba kiasi ni nini ambacho<br />
wewe ungesema ukimpiga hivi na hivi, hilo si neno? Haya endelea tu mama, utupe hayo makaratasi na ujiandikishe. Next kuna<br />
Eddy M.<br />
Tafadhali watu ni wengi na ningalipenda ndugu zangu na dada zangu mchukue dakika tatu, tatu kwa kumulika maneno yenu.<br />
Ninataka kila mtu apate nafasi ya kusema kitu, kwa maana watu hawa… unaposema tano, huyu atabaki. Kwa maana nina<br />
majina hapa chungu nzima na yanazidi kuja. Na ninataka kila moja wenu apate nafasi. Njia tu ya kuwezesha kila mmoja wenu<br />
apate nafasi ni kukata dakika, mpaka itafikia wakati nitasema dakika moja, moja. Kwa hivyo ninaposema tatu, hebu tufuate<br />
hizo. Endelea. Hebu utupe mfano wa dakika tatu. Mnyamaze msikize tafadhali.<br />
Eddy Mzungu: Asante sana Bwana Chairman, kwa majina ninaitwa Eddy Mzungu. Jambo la kwanza ninataka<br />
kuwafahamisha wananchi kuwa tunataka Katiba ambayo ni ya wananchi, Katiba ya wananchi. Saa hii ukitupatia dakika tatu,<br />
tatu kuna mpango gani hapo?<br />
(Clapping from the audience)<br />
Katiba tunataka ya wananchi, na ukiangalia katika registration yako, utaona kwamba… hata pengine utapata watu mia tatu.<br />
Kwa hivyo, ninafikiria mngerudi ma-commissioner, mkaanza tena kuhakikisha Katiba ni ya watu, million thelathini sio ya watu<br />
mia tatu hapa, mia mbili kule, hapana hiyo bado…<br />
Com Pastor Zablon Ayonga: Endelea, endelea.<br />
Eddy Mzungu: Katika elimu, ninaguzia hapo katika elimu, ma-Commissioner tafadhali, muwafundishe watu Katiba. Katiba<br />
iandikwe katika kabila arubaini na mbili, kila mmoja apate haki ya kujua vile inaenda.<br />
Tatu, ninataka kusema hivi, Katiba ambayo iko hapa sio kusema ni mbaya, Katiba ambayo tuko nayo sio mbaya vile, lakini ni<br />
utoshelezi, implementation wa hiyo Katiba ndio mbaya. Saa hii pia tunawaona pale nyinyi ni ma-pr<strong>of</strong>essionals,<br />
ma-Commissioners ishirini na tisa. Mumepewa kazi, sijui ilikwenda aje mkauliza miaka mbili. Hata mkiwa mmekosea hesabu<br />
zenu, mnakuja tena kuuliza miaka kumi, hizi hesabu zenu na nyinyi ma-pr<strong>of</strong>essionals, ma-pr<strong>of</strong>essor. Mnakuja kupiga hesabu na<br />
mnazikosa, na mnakuja tena, muko na njama gani? Muko na njama gani nyinyi? Hebu mtueleze. Ikiwa hii Katiba ni Katiba ya<br />
mageuzi ya Serikali mtuambie, sio kuja hapa kutuambia ni Katiba ya wananchi, hapana, iko njama nyinyi mnataka. Mkiwa<br />
mshaandika Katiba pia, mtueleze, ikiwa mshaandika.<br />
(Clapping from the audience)<br />
29