28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

(Interjection) Com Pastor Zablon Ayonga: Lakini swali ambalo Commissioner anakuuliza, kwamba kiasi ni nini ambacho<br />

wewe ungesema ukimpiga hivi na hivi, hilo si neno? Haya endelea tu mama, utupe hayo makaratasi na ujiandikishe. Next kuna<br />

Eddy M.<br />

Tafadhali watu ni wengi na ningalipenda ndugu zangu na dada zangu mchukue dakika tatu, tatu kwa kumulika maneno yenu.<br />

Ninataka kila mtu apate nafasi ya kusema kitu, kwa maana watu hawa… unaposema tano, huyu atabaki. Kwa maana nina<br />

majina hapa chungu nzima na yanazidi kuja. Na ninataka kila moja wenu apate nafasi. Njia tu ya kuwezesha kila mmoja wenu<br />

apate nafasi ni kukata dakika, mpaka itafikia wakati nitasema dakika moja, moja. Kwa hivyo ninaposema tatu, hebu tufuate<br />

hizo. Endelea. Hebu utupe mfano wa dakika tatu. Mnyamaze msikize tafadhali.<br />

Eddy Mzungu: Asante sana Bwana Chairman, kwa majina ninaitwa Eddy Mzungu. Jambo la kwanza ninataka<br />

kuwafahamisha wananchi kuwa tunataka Katiba ambayo ni ya wananchi, Katiba ya wananchi. Saa hii ukitupatia dakika tatu,<br />

tatu kuna mpango gani hapo?<br />

(Clapping from the audience)<br />

Katiba tunataka ya wananchi, na ukiangalia katika registration yako, utaona kwamba… hata pengine utapata watu mia tatu.<br />

Kwa hivyo, ninafikiria mngerudi ma-commissioner, mkaanza tena kuhakikisha Katiba ni ya watu, million thelathini sio ya watu<br />

mia tatu hapa, mia mbili kule, hapana hiyo bado…<br />

Com Pastor Zablon Ayonga: Endelea, endelea.<br />

Eddy Mzungu: Katika elimu, ninaguzia hapo katika elimu, ma-Commissioner tafadhali, muwafundishe watu Katiba. Katiba<br />

iandikwe katika kabila arubaini na mbili, kila mmoja apate haki ya kujua vile inaenda.<br />

Tatu, ninataka kusema hivi, Katiba ambayo iko hapa sio kusema ni mbaya, Katiba ambayo tuko nayo sio mbaya vile, lakini ni<br />

utoshelezi, implementation wa hiyo Katiba ndio mbaya. Saa hii pia tunawaona pale nyinyi ni ma-pr<strong>of</strong>essionals,<br />

ma-Commissioners ishirini na tisa. Mumepewa kazi, sijui ilikwenda aje mkauliza miaka mbili. Hata mkiwa mmekosea hesabu<br />

zenu, mnakuja tena kuuliza miaka kumi, hizi hesabu zenu na nyinyi ma-pr<strong>of</strong>essionals, ma-pr<strong>of</strong>essor. Mnakuja kupiga hesabu na<br />

mnazikosa, na mnakuja tena, muko na njama gani? Muko na njama gani nyinyi? Hebu mtueleze. Ikiwa hii Katiba ni Katiba ya<br />

mageuzi ya Serikali mtuambie, sio kuja hapa kutuambia ni Katiba ya wananchi, hapana, iko njama nyinyi mnataka. Mkiwa<br />

mshaandika Katiba pia, mtueleze, ikiwa mshaandika.<br />

(Clapping from the audience)<br />

29

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!