28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Aggrey Kilo: Ninashukuru ma-commissioner na wananchi waliojitokeza hapa. Kwa majina mimi ninaitwa Aggrey Kilo, vile<br />

Bwana Chairman alikuwa amesema, na mimi nina vidokezo vitatu ambavyo nitazungumzia.<br />

Kwanza kabisa ni kuhusu nyumba, nyumba za upangaji. Unakuta ya kuwa Kenya sasa, Serikali ama municipaa, sijui kama ni<br />

mkoloni alikuwa anajenga nyumba za upangaji lakini Serikali ya sasa ama municipaa ya Kenya saa hii hawafanyi hivyo na<br />

hatuelewi ni kwa nini. Zile pesa mkoloni alikuwa anaokota ndio zile zile Serikali ya sasa inaokota na unakuta Serikali ama<br />

municipaa hawatujengei nyumba za kupangisha.<br />

Sasa hii imeleta mambo ambapo sasa ni wafanyibiashara fulani wanajenga nyumba na kuna kuwa na wapangaji. Sasa wale<br />

watu wanaweka sheria fulani. Wanasema ukiingia kwa hii nyumba yangu, utalipa deposit ya miezi tatu ama miezi miwili. Sasa<br />

vile unataka kuingia kwa nyumba na una haraka, unampa zile pesa. Ukishampa ile pesa, pengine unachukua transfer kwa<br />

haraka, unamwambia ile pesa yangu nilikupa ya deposit nipe. Inakuwa ni mkutano, zile pesa hupata! Kwa hivyo tungependa<br />

Serikali iangalie hili jambo kwa sababu ukienda kwa watu wa Land Tribunal, wanakwambia ya kuwa hiyo sheria hakuna.<br />

Wanatambua wewe ulipe nyumba, hawatambui deposit. Hizo pesa zaki, itakuwa ni kuvutana na pengine hata uwachane nayo,<br />

kwa vile umepigiwa transfer mbali. Kwa hivyo lazima, Constitution ambayo itakuja, iangalie hili jambo, tuweze kulindwa kwa<br />

haya mambo ya kulipa deposit.<br />

Jambo la pili ni kuhusu elimu. Unakuta ya kuwa tumekuwa na kitu kinaitwa (?) <strong>of</strong>fice ama Divisional fees. Hawa watu<br />

wanatengeneza by-laws zao. Unakuta wanawaita ma head teachers wanawaambia tumepitisha hivi. Na kwa vile ma head<br />

teachers wako chini yao, wakikataa kufuata, watapigwa transfer mahali ambapo hawataki, inabidi wafuate.<br />

Wanakuja na sheria wanasema ni lazima watoto wafanye common exam, Division nzima, ambapo kila shule itakusanya pesa<br />

ipeleke kwa Division. Hizo ni pesa nyingi sana ukiichukua shule zote, karibu shule hamsini. Hizo pesa hatujui zinaenda wapi?<br />

Na wale watu wamelazimishwa, wakikataa transfer. Na ukienda kwa ministry inasema hatutambui hiyo, hamtambui lakini iko,<br />

ina exist. Sasa tufanye vipi? Lazima Katiba mpya ianagalie hawa watu (?) na divisional <strong>of</strong>fices mambo yale<br />

wanafanya na ikuwe legalized, na Serikali ijue zile pesa zinakusanywa zinatumika vipi.<br />

Jambo langu la mwisho ni kuhusu wanabiashara ambao wanjulikana kama Jua-Kali. Jua-Kali wa sasa Kenya unakuta<br />

umemplekea mtu fulani vile mzee alikuwa ameongea, umemepelekea mtu fulani vitu, atatafuta ka kosa kadogo halafu ataruka<br />

kukulipa. Akishakuruka kukulipa, yeye anapesa za kwenda kuchukua advocate, vile yule mzee alikuwa ameongea tu, wewe<br />

hauna pesa.<br />

Sasa ile process ya kwenda kumshataki yule mtu ni ghali na wewe mtu wa Jua-Kali, hana hiyo pesa. Sasa unakauta yule mtu<br />

amedhulumiwa na yule tajiri. Kwa hivyo tena hiyo sheria lazima ianagaliwe ikiwa, au watu watawekewa sheria ambayo<br />

itawasaidia. Ikiwa hana pesa, atasaidiwa vipi? Ili kuweza kuitisha pesa zake.<br />

25

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!