verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Aggrey Kilo: Ninashukuru ma-commissioner na wananchi waliojitokeza hapa. Kwa majina mimi ninaitwa Aggrey Kilo, vile<br />
Bwana Chairman alikuwa amesema, na mimi nina vidokezo vitatu ambavyo nitazungumzia.<br />
Kwanza kabisa ni kuhusu nyumba, nyumba za upangaji. Unakuta ya kuwa Kenya sasa, Serikali ama municipaa, sijui kama ni<br />
mkoloni alikuwa anajenga nyumba za upangaji lakini Serikali ya sasa ama municipaa ya Kenya saa hii hawafanyi hivyo na<br />
hatuelewi ni kwa nini. Zile pesa mkoloni alikuwa anaokota ndio zile zile Serikali ya sasa inaokota na unakuta Serikali ama<br />
municipaa hawatujengei nyumba za kupangisha.<br />
Sasa hii imeleta mambo ambapo sasa ni wafanyibiashara fulani wanajenga nyumba na kuna kuwa na wapangaji. Sasa wale<br />
watu wanaweka sheria fulani. Wanasema ukiingia kwa hii nyumba yangu, utalipa deposit ya miezi tatu ama miezi miwili. Sasa<br />
vile unataka kuingia kwa nyumba na una haraka, unampa zile pesa. Ukishampa ile pesa, pengine unachukua transfer kwa<br />
haraka, unamwambia ile pesa yangu nilikupa ya deposit nipe. Inakuwa ni mkutano, zile pesa hupata! Kwa hivyo tungependa<br />
Serikali iangalie hili jambo kwa sababu ukienda kwa watu wa Land Tribunal, wanakwambia ya kuwa hiyo sheria hakuna.<br />
Wanatambua wewe ulipe nyumba, hawatambui deposit. Hizo pesa zaki, itakuwa ni kuvutana na pengine hata uwachane nayo,<br />
kwa vile umepigiwa transfer mbali. Kwa hivyo lazima, Constitution ambayo itakuja, iangalie hili jambo, tuweze kulindwa kwa<br />
haya mambo ya kulipa deposit.<br />
Jambo la pili ni kuhusu elimu. Unakuta ya kuwa tumekuwa na kitu kinaitwa (?) <strong>of</strong>fice ama Divisional fees. Hawa watu<br />
wanatengeneza by-laws zao. Unakuta wanawaita ma head teachers wanawaambia tumepitisha hivi. Na kwa vile ma head<br />
teachers wako chini yao, wakikataa kufuata, watapigwa transfer mahali ambapo hawataki, inabidi wafuate.<br />
Wanakuja na sheria wanasema ni lazima watoto wafanye common exam, Division nzima, ambapo kila shule itakusanya pesa<br />
ipeleke kwa Division. Hizo ni pesa nyingi sana ukiichukua shule zote, karibu shule hamsini. Hizo pesa hatujui zinaenda wapi?<br />
Na wale watu wamelazimishwa, wakikataa transfer. Na ukienda kwa ministry inasema hatutambui hiyo, hamtambui lakini iko,<br />
ina exist. Sasa tufanye vipi? Lazima Katiba mpya ianagalie hawa watu (?) na divisional <strong>of</strong>fices mambo yale<br />
wanafanya na ikuwe legalized, na Serikali ijue zile pesa zinakusanywa zinatumika vipi.<br />
Jambo langu la mwisho ni kuhusu wanabiashara ambao wanjulikana kama Jua-Kali. Jua-Kali wa sasa Kenya unakuta<br />
umemplekea mtu fulani vile mzee alikuwa ameongea, umemepelekea mtu fulani vitu, atatafuta ka kosa kadogo halafu ataruka<br />
kukulipa. Akishakuruka kukulipa, yeye anapesa za kwenda kuchukua advocate, vile yule mzee alikuwa ameongea tu, wewe<br />
hauna pesa.<br />
Sasa ile process ya kwenda kumshataki yule mtu ni ghali na wewe mtu wa Jua-Kali, hana hiyo pesa. Sasa unakauta yule mtu<br />
amedhulumiwa na yule tajiri. Kwa hivyo tena hiyo sheria lazima ianagaliwe ikiwa, au watu watawekewa sheria ambayo<br />
itawasaidia. Ikiwa hana pesa, atasaidiwa vipi? Ili kuweza kuitisha pesa zake.<br />
25