verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Kue na wakubua wa ma judge hapa pwani.<br />
Watoto wa hapa wapewe maharagwe ya bure mashuleni, wapikiwe pale na wale hapo, hapo.<br />
Sheria ya undanganyifu kwa raia wa pwani iondolewe.<br />
Com. Wambua: Mzee malizia tafadhali.<br />
Mzee. Kalume Mumba: Asanteni sana ndugu. Hayo ndio ya mwisho. Kwa sasa time za enda.<br />
Com. Wambua; Asante. Swali mmoja tu. Nani atakae wapatia watu hiyo pombe bure? unapendekeza nini wewe?<br />
Mzee Kalume Mumba: Serikali iruhusu watu wawe wana kunyua tembo ya bure sababu tembo kikwetu sisi hapa, ni ya kizee.<br />
Pahali panapo olewa mtu, lazima tupawe na ile tembo ile na hata pahali matangani, tupawe ili tembo ile, sasa ile ni kinywa cha<br />
ambacho ni cha kizee, kinatakikana kiwekue free.<br />
Com. Wambua: Asante sana. Hii ni kusema kusiwe na kushikua na kutokulipa.<br />
Mzee Kalume Mumba: Kushikwa na askari ama ku -------<br />
Com. Wambua: Asante sana. Jiandikishe pande hio. Kuna Hussein? Hussein ama Hassan? Hassan? Tafadhalini, tafadhali<br />
tutulie ndio tusikize wenzetu. Kuna Hassan? Hassan? Kuna Maua Jini ama Maua. Haya mama kuja hapa. Maua.<br />
Maua Jini: Jini yangu ni Maua Jini na ninakaa Kongowea. Mimi maoni yangu ni hivo ma plot hizo tunapangisha ni ya shida<br />
sana maana yake kukichelewa na hizo pesa wanaanza kuja kuuzia hiyo nyumba. Ndio maoni yangu. Na kisha maoni yangu<br />
ingine tena, kuna Mwarabu alijenga nyuma ya nyumba yangu na ananifungia maji. Sasa vile ananifungia yale maji, yani mvua<br />
kubua ikiija inaweza kuangusha na nyumba yake ni ya gorafa. Kila nikimuambia nilikwenda Municipal kwenda kuseme yale<br />
maneno, nafikiri alipeana kitu kidogo. Na mimi sina chochote. Sasa nyumba ile ikianguka nitailisha naye nini na watoto wangu<br />
jamani? Ndio yayo tu nilie nayo. Sina mengi.<br />
Com. Wambua: Asante sana mama. Jiandikishe huko. Tumeasikia yote hayo. Nitamuita David Chaka. David Chaka.<br />
Yuko? Haya Kuna Johnson Katana? Johnson Katana? Patrick Makalo? Patrick Makalo. Walter Mbotela? Frederick<br />
Kuledi. Okey endelea.<br />
62