verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Ali Omari Majimbo: Asante. Mimi sina mengi, yangu ni machache<br />
Speaker: Jina yako tafadhali<br />
Ali Omari Majimbo: Jina langu ni Ali Omari Majimbo, hilo jina maarufu sana hilo. Mimi nazungumza kwanza mambo ya<br />
ardhi. Hii mambo ya ardhi ni mambo moja ambayo tulidhulumiwa na hao waliotudhulumi mpaka dakika hii tunao. Kwa hivyo,<br />
ningeomba mambo ya ardhi haya yachukuliwe haraka sana ili ardhi hii irudi kwa wananchi wenyewe. Kwa sababu, hapa tuna<br />
ushahidi kamili kwa sababu sitaki kusema neno holela. Huyu, bi Sultani, huyu Sultani aliyekuja hapa kutoka Yemen na watu<br />
wake na akanyakua aridhi yote akawapa watu wake. Hawa kununua, sasa leo sisi wananchi kwa nini tununue ardhi hii?<br />
Speaker: Kweli<br />
Ali Omari Majimbo: Ikiwa hawa hawa kununua huyu ndiye angekuja kuwapatia watu wake? Ndiye alitawala hapa na<br />
kwa nini ha kununua na sisi leo twambiwa tuuziwe. Tuuziwe na nani? Ukweli ni kwamba, ikiwa wewe umenunua, si kusema eti<br />
ni tajiri sana, hakuna jina la kuwa karibu na............................(inaudible) ardhi wala suma neno la ardhi, wala mwakio ni nani,<br />
hakuna. Kwa hivyo walinyakuwa, kwa hivyo ni haki yetu ardhi hii tupate, hilo ni jambo la kwanza. Jambo la pili,<br />
mweheshimiwa ni mambo ya hii majimbo. Tunataka majimbo na tunaona ni aibu sana katika nchi za kiafrica, leo hii pwani peke<br />
yake. Nisha tembea Tanzania, Uganda, wapi, sikuona mtu yeyote squatter. Nimetembea Kakamega, Western kule wapi, bara<br />
nzima. Kenya nimetembea, sikuona squatters, ajabu squatter ni hapa. Kwa hivyo hii mambo nataka tukomeshe. Kama serikali<br />
haiwezi kukomesha, tutakomesha wenyewe kwa sababu imefika wakate. Mimi sitasema zaidi maanake naambiwa wasemaji ni<br />
wengi na mimi nashukuru kwa kunipa nafasi hii.<br />
Com. Wambua: hizi ..............................(inaudible) za mwisho ni zako kabisa<br />
Ali Omari Majimbo: Tena ninakuletea kitambulisho sasa hivi hapo<br />
Com. Wambua: Jina lenyewe ni Majimbo<br />
Ali Omari Majimbo: Hilo ndilo linajulikana sana hilo<br />
Com. Wambua: Na wewe unataka serikali ya majimbo<br />
Ali Omari Majimbo: Serikali ya majimbo manake ndio italeta amani katika nchi nzime<br />
105