verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Com. Wambua: Asante sana mzee, jiandikishe hapo.<br />
Ali Omari Majimbo: Asante, kidogo tu, neno moja, neno moja tu babangu tafadhali. Kwa sababu ukaona nchi za kiafrica,<br />
vita.......................(inaudible) haviishi sababu hakuna majimbo na majimbo inaleta haki kwa wananchi. kwa hivyo naiomba<br />
tafadhali serikali ya majimbo kila watu jimbo lao. Lakini kitu nataka ni kwamba, serikali kuu lazima mjue iko. Na serikali kuu<br />
tunataka iwe raisi awe ni mthamini wa nchi juu, pesa zikija kwa wafadhili, kila jimbo wagawanyiwe zao ili waweze kutumia,<br />
wakitaka kulipa walipe, sisi hatutaki celi kama hii. Pesa zaja zaingia mfukoni kwa watu, utaona watu wa Kakamega walipa,<br />
watu wa Kisumu walipa, watu wa Pwani wa lipa, lakini twalipa kitu ambacho hakutumia sisi. Hii ni dhambi kabisa. Ndio<br />
maana tunasema tunataka majimbo. Asanteni.<br />
Com. Wambua: Asante sana Mzee, kabla hatujawaita ndugu zetu ambao wameingia sasa, tutamsikiza mwingine mmoja,<br />
Said Abdul, dakika chache tu, mbili ndio tuwapatie nafasi wengine. Excuse me, who is the translating<br />
................................(inaudible)<br />
Speaker: He will do it.<br />
Said Abdul: Asante sana ma-commissioners na watu wote waliohudhuria hapa. Kwa majini naitwa Said Abdul Athman,<br />
leader <strong>of</strong> youth, Kisauni...........................(inaudible). Asalaam Maleikum. Langu haswa ni kuzungumzia habari ya ardhi<br />
kwanza. Makao ni muhimu na mimi ni mzaliwa wa hapa na tangu nizaliwe mpaka sasa nimesoma sehemu nyingi lakini najikuta<br />
niko katika hali moja ya unyonge kwamba jina langu ni squatter. Na nikitoka huko nikirudi hapa mpaka sasa sina makao kwa<br />
hiyo makao ni muhimu sana. Tunaomba kila mtu apatiwe haki yake, apate tittle deed yake ajisikie naye pia ni mtu wa hapa<br />
Kisauni. Nikija katika upande wa kazi, vijana wengi hapa Kisauni hawana kazi na hii ni <strong>constituency</strong>. Naongea kwa niaba yao<br />
kwasababu nimefanya research na nina statistics kwamba vijana elfu 30-hapa Kisauni hawana kazi. Hii ni idadi kubwa sana<br />
kwa hivyo ningependa asli mia 75% ya kazi zote hapa pwani ikiwa Bamburi, ikiwa ni beaches, ikiwa ni KPA wawafikirie hawa<br />
vijana. Ama kama sio hivyo, mimi pamoja na vijana wenzangu tutaunga hata kama ni kutumia nguvu ili sisi tuweze kujiendeleza.<br />
Upande wa afya, tunasema kwamba huduma za afya lazima ziwe bure kwa sababu sasa ukiangalia kama Kisauni, vijana<br />
hawana kazi, utapata wapi mapeni ya kuwasaidia wazazi wao au ndugu zao katika chochote? Kwa hivyo afya iwe bure. elimu<br />
vile vile tunaomba iwe bure na upande wa polisi. Upande wa polisi tumeona kwamba hiyo kazi wana<strong>of</strong>anya ni kama ule muda<br />
wao wako training sio wa kutosha, kwa hivyo kama ilikuwa ni miezi tisa, labda waongezewe miaka moja u nusu manake<br />
wajidumishe vizuri kwa sababu hawajifundishi jinsi ya kuishi vizuri na vijana wenzao. Wakishika vijana hapa, hauna hatia, wewe<br />
ni shida moja kwa moja na ukifika kule wewe huna kazi lakini utaulizwa utoe.................(inaudible) utazitoa wapi? la pili,<br />
tunaona kwamba kuna watu wengi ambao serikali yetu imepate ma-rais wawili tangu ijinyakulie uhuru ambao ni Bwana<br />
Kenyatta na vile vile Bwana Moi, hatujui atakaye kuja sasa. Hii tabia ya kubadilisha pesa, tunaomba kwamba ikome. Pesa<br />
zote ziwe na sura ya kiongozi wa kwanza kabisa ili iwe ni historia kila mwananchi ambaye atakuwa pia hakumwona aweze<br />
106