28.02.2013 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

tumefikia wa mwisho katika horodha, alikuwa ni Ali Taabu Asaa, ambaye alizungumza. Kwa hivyo, tungependa kumuita Yusuf<br />

Hassan kama yuko. Yuko? Sasa mzee, watu ni wengi, kwa hivyo, dakika zako zitakuwa ni tatu tu, uzungumze kwa haraka<br />

haraka.<br />

Yusuf Hassan: Jina langu ni Yusuf Hassan. Nimetoka katika mtaa wa Mishogoroni, ambaye ninawakilisha kama chairman<br />

wa pale. Na ufungu wangu mkubwa ni juu ya ardi. Naona swala la ardhi, Katiba haiwezi kuingia bila ardhi. Ardhi ndio swala<br />

kubwa katika Kenya yetu hii. Tunataka wafikirie sana mambo ya ardhi, maanake tumepata taabu kuangaishwa na wageni,<br />

ambao hatujui walitoka wapi. Ikiwa mimi ni mwananchi wa hapa, na muzaliwa wa hapa, sina ardhi, mtu ametoka sijui dunia ya<br />

wapi, yeye ana ardhi, na sisi watu wa hapa hatuna ardhi. Ndio maana swala la Majimbo ni lazima liweko. Maana sisi wenyeji<br />

wa hapa, tunadharauliwa sana. Tunaambiwa tungojee maembe. Hii mambo, swala la kuwa sisi watu wa hapa tumezaliwa, na<br />

bado tunaangaishwa na wageni. Hii Katiba iangalie sana kwa line la u-squatter. Sisi sio wale wanyama wanaoitwa “chura”,<br />

maanake, they have no places – hawana makao. Sisi ni watu ambao tumezaliwa hapa, mufikirie sana swala la ardhi. Hatutaki<br />

ardhi irudishwe kwa watu wetu wote hapa nchini. Tunataka sisi wenyeji wa hapa, ardhi zetu zitolewe katika mikono ya wageni.<br />

Zirudishwe kwetu wenyewe.<br />

La pili ni elimu kwa watoto wadogo: naona wakati nilipokuwa mdogo, nilisoma kuanzia shule ya pakitani, mpaka tukaenda<br />

shule la hewa. Tulikuwa tunasoma vizuri sana, na pesa zilikuwa, sio kama hizi siku hizi ukimpeleka mtoto, taabu sana. Watoto<br />

wanaranda randa, hawana elimu. Hawasomeshwi. Hakuna nursery, hakuna namna ya kuwasomesha watoto. Kwa hivyo,<br />

tunataka watoto wasome bure, na warudishiwe maziwa yao kama tulivyokuwa tukinywa, sisi wazee.<br />

Swala la chakula: chakula kiangaliwe, maanake, chakula siku hizi zimepandishwa bei. Hata masikini hawawezi kujimudu.<br />

Tunataka swala la chakula liangaliwe. Food control, maanake, tunaona katika board ya upande wa chakula, ina taabu sana.<br />

Mara huyu anapandisha kile, na huyu anapandisha vingine. Hili swala la chakula liangaliwe. Lakini sio kupandisha “kiolela”.<br />

Iangaliwe katika sherika ya Katiba. Vyakula vyangaliwe vizuri Bwana Commissioner.<br />

Swala la upande wa prisons – jela: tumeona haki …………………………. (inaudible), wanateswa sana. Hawana ……….<br />

na vyakula vimewekwa kama ……………………… (inaudible) tumepewa uhuru, na ni lazima tuhutumie uhuru wetu. Watu<br />

ambao wamewekwa kule, sio wanyama, ni wanadamau. Na hili swala la wa-prison, ni lazima liangaikiwe na lishugulikiwe,<br />

maanake, tuko katika Kenya uhuru. NI lazima wale walio fungwa – wafungwa waangaliwe vizuri afya yao. Sio kuchukua<br />

wafungwa, na mara tunasikia wafungwa wengine wananyongwa. Kwa njia gani? Hau kuna kinyume gani? Kuna njama gani<br />

ya watu wanapelekwa, na huku tunasikia watu wameuwawa katika ma-jela. Twataka kujua kwa nini wanauliwa namna hii.<br />

Hili ndilo swala ambalo linasikitiza sana. Vyakula pia hawapewi, vyakula ki-sawa sawa. Hata wengine wanakuwa ni swala<br />

lingine, ambalo lina aibu pia. Mtu apati chakula mpaka anajitoa yeye mwenyewe kuwa kama………. hivyo ndivyo ni aibu.<br />

Tunataka tuangalie upande wa chakula katika prisons – yaani jela. Jela iangaliwe kwa ……….. (inaudible) kwa wafungwa.<br />

Waangalie sana mambo ya jela.<br />

59

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!