verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
tumefikia wa mwisho katika horodha, alikuwa ni Ali Taabu Asaa, ambaye alizungumza. Kwa hivyo, tungependa kumuita Yusuf<br />
Hassan kama yuko. Yuko? Sasa mzee, watu ni wengi, kwa hivyo, dakika zako zitakuwa ni tatu tu, uzungumze kwa haraka<br />
haraka.<br />
Yusuf Hassan: Jina langu ni Yusuf Hassan. Nimetoka katika mtaa wa Mishogoroni, ambaye ninawakilisha kama chairman<br />
wa pale. Na ufungu wangu mkubwa ni juu ya ardi. Naona swala la ardhi, Katiba haiwezi kuingia bila ardhi. Ardhi ndio swala<br />
kubwa katika Kenya yetu hii. Tunataka wafikirie sana mambo ya ardhi, maanake tumepata taabu kuangaishwa na wageni,<br />
ambao hatujui walitoka wapi. Ikiwa mimi ni mwananchi wa hapa, na muzaliwa wa hapa, sina ardhi, mtu ametoka sijui dunia ya<br />
wapi, yeye ana ardhi, na sisi watu wa hapa hatuna ardhi. Ndio maana swala la Majimbo ni lazima liweko. Maana sisi wenyeji<br />
wa hapa, tunadharauliwa sana. Tunaambiwa tungojee maembe. Hii mambo, swala la kuwa sisi watu wa hapa tumezaliwa, na<br />
bado tunaangaishwa na wageni. Hii Katiba iangalie sana kwa line la u-squatter. Sisi sio wale wanyama wanaoitwa “chura”,<br />
maanake, they have no places – hawana makao. Sisi ni watu ambao tumezaliwa hapa, mufikirie sana swala la ardhi. Hatutaki<br />
ardhi irudishwe kwa watu wetu wote hapa nchini. Tunataka sisi wenyeji wa hapa, ardhi zetu zitolewe katika mikono ya wageni.<br />
Zirudishwe kwetu wenyewe.<br />
La pili ni elimu kwa watoto wadogo: naona wakati nilipokuwa mdogo, nilisoma kuanzia shule ya pakitani, mpaka tukaenda<br />
shule la hewa. Tulikuwa tunasoma vizuri sana, na pesa zilikuwa, sio kama hizi siku hizi ukimpeleka mtoto, taabu sana. Watoto<br />
wanaranda randa, hawana elimu. Hawasomeshwi. Hakuna nursery, hakuna namna ya kuwasomesha watoto. Kwa hivyo,<br />
tunataka watoto wasome bure, na warudishiwe maziwa yao kama tulivyokuwa tukinywa, sisi wazee.<br />
Swala la chakula: chakula kiangaliwe, maanake, chakula siku hizi zimepandishwa bei. Hata masikini hawawezi kujimudu.<br />
Tunataka swala la chakula liangaliwe. Food control, maanake, tunaona katika board ya upande wa chakula, ina taabu sana.<br />
Mara huyu anapandisha kile, na huyu anapandisha vingine. Hili swala la chakula liangaliwe. Lakini sio kupandisha “kiolela”.<br />
Iangaliwe katika sherika ya Katiba. Vyakula vyangaliwe vizuri Bwana Commissioner.<br />
Swala la upande wa prisons – jela: tumeona haki …………………………. (inaudible), wanateswa sana. Hawana ……….<br />
na vyakula vimewekwa kama ……………………… (inaudible) tumepewa uhuru, na ni lazima tuhutumie uhuru wetu. Watu<br />
ambao wamewekwa kule, sio wanyama, ni wanadamau. Na hili swala la wa-prison, ni lazima liangaikiwe na lishugulikiwe,<br />
maanake, tuko katika Kenya uhuru. NI lazima wale walio fungwa – wafungwa waangaliwe vizuri afya yao. Sio kuchukua<br />
wafungwa, na mara tunasikia wafungwa wengine wananyongwa. Kwa njia gani? Hau kuna kinyume gani? Kuna njama gani<br />
ya watu wanapelekwa, na huku tunasikia watu wameuwawa katika ma-jela. Twataka kujua kwa nini wanauliwa namna hii.<br />
Hili ndilo swala ambalo linasikitiza sana. Vyakula pia hawapewi, vyakula ki-sawa sawa. Hata wengine wanakuwa ni swala<br />
lingine, ambalo lina aibu pia. Mtu apati chakula mpaka anajitoa yeye mwenyewe kuwa kama………. hivyo ndivyo ni aibu.<br />
Tunataka tuangalie upande wa chakula katika prisons – yaani jela. Jela iangaliwe kwa ……….. (inaudible) kwa wafungwa.<br />
Waangalie sana mambo ya jela.<br />
59