verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Com Paul: Asante sana Muhammed Bashua, jiandikishe hapo tafadhali, nitawauliza akina mama wawili, watatu hivi, lakini<br />
kabla ya hapo, nitamuita Abubakra ni takupatia nafasi kwa maanake ulikuwa unataka kwenda kumuona Daktari, lakini tafadhari<br />
dakika nitakupatia ni mbili tu, kama una memorandum utuachie tusome, halafu uguzie yale muhimu.<br />
Interjection inaudible.<br />
Abubakra Awali : ( in venacular) Kwa majina naitwa Abubakra Awali, na maoni yangu ni kama yafuatavyo, ningependelea<br />
na system ya Government ifuatayo, tuwe na National Parliament na pia tuwe na Jimbo Parliament, kwenye National Parliament,<br />
yule atakayepigania uRaisi , awe atakuwa ki Katiba amewajibika kutangaza Mawaziri wake ambao atakuwa nao kwenye<br />
Serikali yake peke yake wakati wa campaign, halafu naibu wa Waziri watateuliwa katika wale waBunge kulingana na Political<br />
Consideration, isiwe waziri amewekwa kwasababu ya kisiasa, iwe ni kwasababu ya kuendesha nchi kikamilivu, mkubwa wa<br />
Jimbo pia naye atateuliwa na ile jimbo ambayo inahusika nawe ataisomea, na wale ma Councillor wote watakaa pamoja<br />
waunde sheria za jimbo lao katika mambo Fulani, na mambo Fulani yataendeshwa na Serikali kuu, Serikali kuu itahusika tu na<br />
mambo ya foreign policy, military policy, na physical policies na Nation budget, mengine yaachiwe Serikali za Mkoa. Mali<br />
yanayopatikana katika mikoa, Yawe yatashikwa na mikoa ile ila tu 30% zipelekwe kwa Serikali kuu ambayo itaendeshwa<br />
mambo ya nchi nzima.<br />
Kwa upande wa Mwananchi wa Kenya, Mwananchi wa Kenya iwe ni wakusaliwa, hata kama Mwananchi ule amezaliwa na<br />
mgeni maadamu amezaliwa katika Nchi ya Kenya, awe ni Mkenya. Na Mkenya akiwa amesafiri na amezaa mtoto nje ya<br />
Kenya lakini maadamu ule mzee ni Mkenya, basi mtoto ule pia awe Mkenya. Pia dual citizenship ikubalike katika sheria. Na<br />
ikiwa kuna mgeni ambaye amekaa Kenya kwa muda wa miaka mitano na amejulikana mambo yake ni ya kisawasawa, basi<br />
jimbo liweze kurecommend kwamba Mwananchi yule apewe uraia wa Kenya.<br />
Jambo lingine, ningependa kusema kwa kifungo cha Sheria ambayo kianaitwa right to recall, kwamba mfanyi kazi wa Serikali<br />
yoyote au mtu ambaye anayechaguliwa akiwa ni Mbunge ma ni Councillor awe ataitwa arudi kwa Raia ikiwa amefanya<br />
makosa, na kiti chake kichukuliwe na kipigiwa kura mara ingine. Indipendent Candidates wakubalike, kwa sababu Wananchi<br />
wanapata taabu wanaona vyama vingi haviendi kimivumo ya kiphilosophia mbali ni mivumo ya kijambazi. Kuwe na kifungo cha<br />
sheria kinachosema katika Katiba zote mbili, iwe ya jimbo ama iwe ni ya Serikali kuu, kwamba kusiwe na sheria ambayo<br />
itakwenda zidi na imani na matumaini ya Mwananchi yoyote, yani Mwananchi asilazimizwe, kufuata jambo ambayo ni kinyume<br />
na dini yake ama ni kinyume na utamaduni wake.<br />
Jambo jingine ni ardhi, ardhi imepigiwa kelele sana, ningeomba kuwe na sheria maalumu, kwamba ardhi zote ambazo zimetoka<br />
kwa unyanganyivu, zirudi katika mikono ya Serikali, Serikali ya majimbo iwe na sehemu yake na Serikali kuu iwe na sehemu<br />
yake. Kasha kupangwe sheria kupitia kwa Serikali za majimbo, na Serikali za nchi kuu iangalie ardhi ile itatumika namna gani<br />
kwa masilaha ya Wananchi wanaohusika na area zile. Jambo jingine ni Kadhis Court, napendekeza kwamba juridicing yake<br />
iongezwe iwe kuanzia low court, high court, mpaka court <strong>of</strong> appeal kufuatia sheria za kislamu, isiwe mtu ameenda kwa kadhi na<br />
87