verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Lingine, Kenya iwe na mavazi rasmi ya kiheshima. Kwa upande wa eleimu pia, tunaomba elimu iwe ya bure ili kila mwananchi<br />
wa Kenya awe na elimu. Lingine ni kuwa…<br />
(Interjection) Com Pastor Ayonga: hebu maongezi ya kule nyuma, tafadhali tumsikilize huyu mama.<br />
Bahati Musa: Lingine kwa maoni yangu ninaomba kuwa matibabu ya hospitali yawe ya bure ili kila mwananchi apate huduma.<br />
Asanteni.<br />
Com Pastor Ayonga: Asante mama, kama unaweza kutoa hiyo karatasi yako na ujiandikishe. Huyo alikuwa Bahati Musa.<br />
Sasa ni Tumu Hamisi. Halafi anayeitwa Harry, ajitayarishe. Tafadhali tuwe kimwa ili tuyasikia maoni ya mama Tumu Hamisi.<br />
Tumu Hamisi: Hamjambo?<br />
Response from the audience: Hatujambo.<br />
Tumu Hamisi: Kwa majina kamili ninaitwa Mwanatumu Mwinyi Hamisi, ninatoka kwenye kamati ya Ziwa la Ng’ombe<br />
settlement scheme. Nimekuja hapa kutoa maoni.<br />
Maoni yangu ya kwanza yanasema kuwa, mkuu wa sheria achaguliwe na kamati ya bunge na sio Rais. tunataka Serikali ya<br />
majimbo. Miswada yote katika bunge iwasilishwe kwaq Speakeer kwa lugha ya kiswahili na pia igadiliwe Kiswahili.<br />
Madiwani wote wawe na <strong>of</strong>isi katika wardi zao.<br />
Mawaziri wachaguliwe na bunge na sio Rais. kila mbunge na Diwani awe na kamati katika eneo lake, itakay<strong>of</strong>uatilia kazi yake<br />
na yale aliyoahidi kutengeneza wakati wa campaign na awe na <strong>of</strong>isi katika eneo lake. Ni hayo tu.<br />
Com Pastor Ayonga Bahati Musa: Asante mama. Wapi Harry na Bakari Sire awe tayari.<br />
Harry Philip Mbai Njoro Ali: Assalam aleykum!<br />
Response from the audience: Warahmatulahi wabarakat.<br />
Harry Philip Mbai Njoro Ali: Mimi ningependa kwanza kusimama, tafadhali. Sipendi kuketi. Jina langu ni Harry Philip Mbai<br />
Njoro Ali. Mkaaji wa Free town, kabila langu ni Mdigo Mkauma.<br />
Kwanza ninashukuru wote waliotoa maoni, watu wote, wote kwa sababu yale walioyasema ndio niliyoyaandika hapa<br />
35