“Kuhusu vitendo vya ubakaji ambavyo nimevisikia, ni kweli. Tu<strong>na</strong>mshukuru MheshimiwaMbunge kwa kutuletea taarifa hizo <strong>na</strong> <strong>na</strong>amini wenzangu katika Wizara husika suala hililitachunguzwa kwa sababu kwa vyovyote vile lazima Jeshi litakuwa <strong>na</strong> majirani. Kwa hiyo, <strong>na</strong>dhanitatizo hapa siyo kwamba liko karibu ila ni tabia, kama ni kweli, litashughulikiwa”. Mwisho wakunukuu.Waheshimiwa Wabunge, kwa kuzingatia jibu la Mheshimiwa Waziri, ni dhahiri kwambaMheshimiwa Waziri hakutamka kwamba Wa<strong>na</strong>jeshi wa<strong>na</strong>baka watoto wa shule, bali alichokisemani kwamba Serikali ilikuwa imesikia <strong>na</strong> kumshukuru Mheshimiwa aliyeuliza swali kwa kutoa taarifahiyo Serikalini ili iweze kufanyiwa kazi <strong>na</strong> hatua ziweze kuchukuliwa. (Makofi)Nawaomba Waheshimiwa wote ambao tu<strong>na</strong>jibu maswali au kutoa maelezo humuBungeni kuendelea kuwa <strong>na</strong> umakini ambao tumekuwa <strong>na</strong>o kwa ajili ya kufanya shuguli za Bungeletu kuwa bora zaidi.Waheshimiwa Wabunge, huu ndiyo Mwongozo wangu kuhusu suala hili. Nawashukurunikwa kunisikiliza. Tutaendelea kufafanua Miongozo mingine kadri muda utakavyokuwa ukiruhusu.Kwa sababu ya muda, kabla sijamwita Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu Wizara ya Habari,Vija<strong>na</strong>, Utamaduni <strong>na</strong> Michezo, <strong>na</strong>omba sasa nimwite Mheshimiwa Mwenyekiti wa Bunge,Mheshimiwa Mabumba ili aje kuendeleza hili jahazi hapa mbele. Mheshimiwa Mabumba!I<strong>na</strong>elekea ku<strong>na</strong> mawasiliano kidogo, basi nimwite Msemaji wa Kambi ya Upinzani.MHE. JOSEPH O. MBILINYI - MSEMAJI MKUU <strong>WA</strong> KAMBI YA UPINZANI (WIZARA YA HABARI,VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO): Mheshimiwa Naibu Spika, ni<strong>na</strong> matatizo kidogo ya macho,wakati mwingine u<strong>na</strong>weza ukao<strong>na</strong> machozi ya<strong>na</strong>toka, silii! Ni matatizo kidogo ya macho,nimepata eye infections.Mheshimiwa Naibu Spika, <strong>na</strong>mshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uhai, afya njema <strong>na</strong>kunipa fursa ya kipekee ya kufanya maajabu yenye manufaa kwa taifa langu; kwa baraka zake,niliweza kung’ara kwenye sa<strong>na</strong>a <strong>na</strong> kuwa nyota wa muziki wa Bongofleva, ukipenda – Hip Hop;kwa uwezo wake leo nimekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini <strong>na</strong> kwa mapenzi yake, mimiMsanii wa Bongofleva sasa nimekuwa Waziri Kivuli wa Habari, Vija<strong>na</strong>, Utamaduni <strong>na</strong> Michezo.(Makofi)NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbilinyi, sekunde tu! Sasa, <strong>na</strong>omba kumkaribisha MheshimiwaMabumba ili aweze kuendelea.Mwenyekiti (Mheshimiwa Sylivester Massele Mabumba) Alikalia KitiMWENYEKITI: Mheshimiwa, endelea!MHE. JOSEPH O. MBILINYI - MSEMAJI MKUU <strong>WA</strong> KAMBI YA UPINZANI (WIZARA YA HABARI,VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nakushukuru kwa kunipa<strong>na</strong>fasi hii ya kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kuwasilisha maoni <strong>na</strong> mapendekezo ya KambiRasmi ya Upinzani kuhusu Bajeti ya Wizara ya Habari, Vija<strong>na</strong>, Utamaduni <strong>na</strong> Michezo, kwa mwakawa fedha 20<strong>11</strong>/2012, kwa mujibu wa Kanuni za Bunge Kifungu <strong>cha</strong> 99 (7) toleo la 2007.Mheshimiwa Mwenyekiti, <strong>na</strong>tambua <strong>na</strong> kuthamini imani <strong>na</strong> heshima kubwa niliyopewa <strong>na</strong>wa<strong>na</strong>nchi wa Jimbo la Mbeya Mjini katika U<strong>cha</strong>guzi Mkuu uliopita. Li<strong>cha</strong> ya kuletewa mabomu yamachozi, virungu <strong>na</strong> bado haku<strong>na</strong> yeyote kati yetu aliyeogopa. Uwongo haukuweza kufunikaukweli <strong>na</strong> hata rushwa haikuweza kurubuni akili. Wa<strong>na</strong>nchi kwa umoja wao walijitoa mhangakulinda kura zetu bila woga <strong>na</strong> hatimaye Dunia nzima i<strong>na</strong>jua <strong>na</strong> imekubali kuwa mimi ndiye SUGU<strong>na</strong> CHADEMA si <strong>cha</strong>ma legelege, bali ni Chama makini <strong>na</strong> ki<strong>na</strong>choaminika mbele ya jamii.(Makofi)Mheshimiwa Mwenyekiti, <strong>na</strong>mshukuru <strong>na</strong> kumpongeza kwa moyo wa dhati kabisa KatibuMkuu wa Chama <strong>cha</strong>ngu, Dkt. Wilbrod Peter Slaa <strong>na</strong> Makamanda wote wa CHADEMA nchi nzimakwa kazi kubwa tuliyoifanya katika U<strong>cha</strong>guzi Mkuu uliopita <strong>na</strong> kwa harakati nzito tu<strong>na</strong>zoendelea42
kuzifanya za kuielimisha jamii juu ya haki zao za msingi. Watapiga kelele sa<strong>na</strong> lakini hatutarudinyuma, tu<strong>na</strong>songa mbele mpaka kieleweke. (Makofi)Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima <strong>na</strong> taadhima, <strong>na</strong>mshukuru Kiongozi Mkuu waKambi Rasmi ya Upinzani <strong>na</strong> Mwenyekiti wa CHADEMA, Mheshimiwa Freeman Aikael Mbowe kwakuniamini <strong>na</strong> kuniteua kuwa Waziri Kivuli wa Wizara hii nyeti. Namshukuru pia Naibu KiongoziMheshimiwa Kabwe Zuberi Zitto (Mbunge) <strong>na</strong> M<strong>na</strong>dhimu Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani,Mheshimiwa Tundu Lissu, kwa ushirikiano wao mkubwa wa<strong>na</strong>onipa katika kutekeleza majukumuyangu ya Kibunge.Mheshimiwa Mwenyekiti, <strong>na</strong>chukua fursa hii pia kuwashukuru kwa dhati wadau wote waSekta ya Habari, Vija<strong>na</strong>, Utamaduni <strong>na</strong> Michezo, kwa kutuamini <strong>na</strong> kuthamini kazi kubwa yauwakilishi i<strong>na</strong>yofanywa <strong>na</strong> Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, hata kuamua kutupa ushirikianomkubwa katika maandalizi ya hotuba hii. Naomba niwatambue baadhi ya wadau hao kwashukrani kama ifuatavyo:- Baraza la Habari Tanzania (MCT), Umoja wa Klabu za Waandishi waHabari Tanzania (UTPC), Baraza la Sa<strong>na</strong>a la Taifa (BASATA), Rulu Arts Promotions i<strong>na</strong>yosimamiasa<strong>na</strong>a <strong>na</strong> Wasanii wote waliokuja kuunga mkono hotuba hii ya Kambi ya Upinzani. (Makofi)Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya habari, weledi <strong>na</strong> maadili ya uandishi wa habari. Vyombovya habari ni taasisi muhimu sa<strong>na</strong> katika ujenzi wa Taifa lenye kufuata misingi ya demokrasia <strong>na</strong>utawala bora. Vyombo vya habari vi<strong>na</strong> dhima kubwa ya kutoa habari <strong>na</strong> taarifa kwa umma waWatanzania kuhusu mambo ya<strong>na</strong>yohusu maisha yao <strong>na</strong> vilevile kutoa elimu <strong>na</strong> burudani. Vyombovya habari ni kiungo muhimu <strong>cha</strong> kuunganisha jumuiya mbalimbali, kujenga Utaifa, umoja <strong>na</strong>kuhimiza maendeleo.Mheshimiwa Mwenyekiti, vyombo vya habari kwa ujumla wake, ni taasisi yenye nguvu. I<strong>na</strong>uwezo mkubwa wa kujenga <strong>na</strong> vilevile kubomoa ikiwa vitatumiwa <strong>na</strong> kujiendesha vibaya aukuingiliwa uhuru wake. Hivyo basi, wakati vyombo vya habari vi<strong>na</strong> wajibu wa kufanya kazi kwakuzingatia umakini, weledi <strong>na</strong> maadili ya uandishi wa habari, Serikali <strong>na</strong>yo i<strong>na</strong> wajibu mkubwa wakuhakikisha uhuru <strong>na</strong> haki za kutafuta <strong>na</strong> kupata habari vi<strong>na</strong>lindwa.Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiotiliwa shaka kuwa baadhi ya vyombo vya habarivimekuwa vikikiuka kabisa maadili ya uandishi wa habari. Ki<strong>na</strong>chosikitisha zaidi ni pale ambapobaadhi ya Waandishi wa Habari <strong>na</strong> baadhi ya Vyombo vya Habari <strong>na</strong> ambavyo vimepewadhama<strong>na</strong> kubwa <strong>na</strong> jamii wa<strong>na</strong>pokubali kutumiwa <strong>na</strong> baadhi ya watu wenye nguvu ama zakisiasa au za kifedha ili kuendeleza ajenda zao bi<strong>na</strong>fsi. Hili ni jambo lisilopendeza hata kidogo <strong>na</strong>hali<strong>na</strong> mustakabali mzuri kwa amani <strong>na</strong> maendeleo ya nchi yetu.Mheshimiwa Mwenyekiti, ki<strong>na</strong>chosikitisha zaidi, vyombo vya habari vya Serikali <strong>na</strong> hapa<strong>na</strong>lizungumzia Gazeti la Serikali Daily News kuongoza katika ukiukwaji wa maadili ambapo katikakipindi <strong>cha</strong> m<strong>cha</strong>kato wa U<strong>cha</strong>guzi Mkuu uliopita, gazeti hili lili<strong>cha</strong>pisha tahariri ya uchocheziiliyosema, “Kamwe Dkt. Slaa hatakuwa Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.”Maoni haya ya Mhariri yalilenga kuleta uchochezi <strong>na</strong> kujenga hoja kwamba hata kamaWatanzania watam<strong>cha</strong>gua Dkt. Slaa kuwa Rais wao, lakini kamwe hatakabidhiwa jukumu lauongozi, jambo ambalo ni la hatari kwa usalama wa Taifa. (Makofi)Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la hatari zaidi hapa ni kwamba walioendesha vitendo hivivya uchochezi ni Wahariri wa Gazeti la Serikali ambalo lilitakiwa kuwa mfano wa kuigwa kwavyombo vingine vya habari nchini.Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi ya upinzani i<strong>na</strong>itaka Serikali ilieleze Bunge hili Tukufuimemchukulia hatua gani Kaimu Mhariri Mtendaji wa gazeti hilo ambaye aliidhinisha ku<strong>cha</strong>pishwakwa tahariri hiyo? Je, Idara ya Habari Maelezo iliwahi kuandika barua kwa Mhariri huyu kumuonyakama ambavyo imekuwa ikifanya hivyo kwa magazeti mengine; hata kabla ya habarihaijaandikwa, tayari barua i<strong>na</strong>kuwa imeandaliwa <strong>na</strong> ki<strong>na</strong>chosubiriwa ni gazeti ku<strong>cha</strong>pishwa <strong>na</strong>barua hiyo kufika kwa wahusika? Kama Serikali haijamchukulia hatua, Waziri a<strong>na</strong>weza vipi kuwa<strong>na</strong> mamlaka ya kuadhibu vyombo vingine vi<strong>na</strong>vyodaiwa kukiuka maadili ya uandishi wa habari43
- Page 7 and 8: Mheshimiwa Naibu Spika, lakini umeg
- Page 11 and 12: NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiw
- Page 13 and 14: NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA
- Page 15 and 16: Pili, Wakurugenzi na Wakurugenzi wa
- Page 17 and 18: MHE. JOHN J. MNYIKA: Naomba unisiki
- Page 19 and 20: inaongozwa na Mbunge wa Jimbo la Pe
- Page 21 and 22: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuha
- Page 23 and 24: Mheshimiwa Naibu Spika, Baraza la H
- Page 25 and 26: katika kukuza na kuimarisha Demokra
- Page 27 and 28: wakiwa ni Baraza Kuu la Michezo Bar
- Page 29 and 30: · Kusimamia usambazaji wa machapis
- Page 31 and 32: · Kutoa taarifa katika magazeti ku
- Page 33 and 34: · Kufanya tathmini na ufuatiliaji
- Page 35 and 36: 2011 wakati wa vikao vya Kamati vil
- Page 37 and 38: na Mfuko wa Vyombo vya Habari na Ba
- Page 39 and 40: · Serikali itenge fedha za mafunzo
- Page 41: Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, nape
- Page 45 and 46: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na um
- Page 47 and 48: wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UD
- Page 49 and 50: (iii)(iv)(v)(vi)(vii)Chuo Kikuu cha
- Page 51 and 52: kuendelea kufanya vibaya na kuambul
- Page 53 and 54: Serikali, sasa sisi tayari Umoja wa
- Page 55 and 56: iangaliwe. Tena nashukuru hii Wizar
- Page 57 and 58: kunichagua kuwa Mbunge wao kwa mara
- Page 59 and 60: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpira wa mig
- Page 61 and 62: na Academy yake, huyu ndiye mtu wa
- Page 63 and 64: matangazo ya kudhalilisha nchi yetu
- Page 65 and 66: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingin
- Page 67 and 68: Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi ni
- Page 69 and 70: namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa
- Page 71 and 72: Bunge. Mheshimiwa Waziri Mkuu alipo
- Page 73 and 74: pombe tu, wanaishia kunywa pombe, b
- Page 75 and 76: Nishukuru wafadhili na hasa TBC bas
- Page 77 and 78: ushuru kwenye vifaa vya michezo. Vi
- Page 79 and 80: Mheshimiwa Mwenyekiti, niende TBC,
- Page 81 and 82: Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna
- Page 83 and 84: Je, hawa watu wapo na wanafanya kaz
- Page 85 and 86: hapa Bungeni, yupo kule kwenye ofis
- Page 87 and 88: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza natak
- Page 89 and 90: tunakwenda Wizara ya Utamaduni kwa
- Page 91 and 92: MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Wale wen
- Page 93 and 94:
jambo hili la kuhakikisha kwamba ku
- Page 95:
na yakizungumza habari ya interest