wakati yenyewe imeshindwa kuwajibisha Wahariri wa gazeti lake? Uchochezi huu u<strong>na</strong>paswakukemewa <strong>na</strong> kila Mtanzania kwa nguvu zetu zote. (Makofi)Mheshimiwa Spika, ku<strong>na</strong> tabia imezuka ya viongozi wa Serikali kuvitisha vyombo ya habaripale vi<strong>na</strong>potoa udhaifu wa Watendaji Serikalini, kama ilivyotokea hapa Bungeni hivi karibuniwakati Mheshimiwa Waziri Ofisi ya Rais (Mahusiano) alipotoa vitisho kwa gazeti la Mwa<strong>na</strong>nchi.Kambi ya Upinzani i<strong>na</strong>laani kitendo hicho <strong>na</strong> kuitaka Serikali iache mara moja vitisho kwa vyombovya habari. (Makofi)Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni jambo ambalo wote tu<strong>na</strong>takiwa tulikemee kwa nguvu zetuzote <strong>na</strong> kila i<strong>na</strong>powezeka<strong>na</strong> tuwaumbue <strong>na</strong> tuwataje wale wote wa<strong>na</strong>oshiriki katika matendohaya ambayo haya<strong>na</strong> nia njema sio tu kwa tasnia yenyewe ya habari kwa kuipa ji<strong>na</strong> baya <strong>na</strong>kuipaka matope, bali pia kwa nchi yetu kwani tu<strong>na</strong> mifano dhahiri hapa Afrika <strong>na</strong> kwinginekoduniani juu ya athari ambazo zimewahi kutokea vyombo vya habari vilipotumika vibaya. Sotetu<strong>na</strong>kumbuka yaliyofanywa <strong>na</strong> vyombo vya habari vya Serikali kule Rwanda <strong>na</strong> maafayaliyotokea.Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Haki ya Kupata Habari. Haki ya kupata habari ni haki yamsingi ya bi<strong>na</strong>damu <strong>na</strong> i<strong>na</strong>lindwa <strong>na</strong> Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano waTanzania. Ni haki ambayo i<strong>na</strong>mhusu kila Mtanzania bila ya kujali wadhifa au daraja lake kwenyejamii, umri au jinsia. Mwaka 2006, <strong>na</strong>taka niamini kwa nia njema kabisa, Serikali ilianzisham<strong>cha</strong>kato wa kutunga Sheria ya Uhuru wa Habari kwa kutoa Rasimu ya Muswada wa Sheria hiyo.Hata hivyo Rasimu ya Muswada huo ilikataliwa <strong>na</strong> wadau kwa sababu haikukidhi haja walaviwango vya Sheria kama hiyo vi<strong>na</strong>vyotakika<strong>na</strong>. Mwaka 2007, Serikali iliitikia wito wa Wadau waHabari <strong>na</strong> Haki za Bi<strong>na</strong>damu wa kutaka kuwepo <strong>na</strong> sheria mbili tofauti <strong>na</strong> kutenganisha Rasimuyake ya Muswada wa Sheria ya Uhuru wa Habari <strong>na</strong> kutengeneza Rasimu mbili, moja ya Sheria yaHaki ya Kupata Habari <strong>na</strong> nyingine ya Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari.Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya kutenganisha Muswada huo ilikuwa <strong>na</strong> bado ni muhimusa<strong>na</strong> kwa sababu Sheria ya Haki ya Kupata Habari ni mtambuka <strong>na</strong> i<strong>na</strong>husu haki ya Kikatiba yaWatanzania wote. Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ni ya kisekta <strong>na</strong> i<strong>na</strong>husia<strong>na</strong> zaidi <strong>na</strong>kutoa mwelekeo wa jinsi vyombo vya habari vitakavyofanya kazi nchini.Mheshimiwa Mwenyekiti, m<strong>cha</strong>kato huo ulipata mwitiko mzuri kutoka kwa Wadaumbalimbali wa Habari <strong>na</strong> Wa<strong>na</strong>harakati wa Haki za Bi<strong>na</strong>damu ambao kwa umoja waowalitembea nchi nzima kukusanya mawazo <strong>na</strong> mapendekezo ya wa<strong>na</strong>nchi kuhusu Sheria ya Hakiya Kupata Habari. Walipeleka mapendekezo yao kwa Serikali ili yaweze kujumuishwa katikam<strong>cha</strong>kato wa utungaji wa Sheria.Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi rasmi ya Upinzani i<strong>na</strong>sisitiza kuwa Sheria hii ni muhimusa<strong>na</strong>, kwani itaimarisha utawala wa wazi <strong>na</strong> uwajibikaji. Utawala ulioshamiri katika mila za usiri ndioulioifikisha Tanzania yetu mahali pabaya. Ndio <strong>cha</strong>nzo <strong>cha</strong> mikataba mibovu <strong>na</strong> kushindwa kwauwajibikaji kwa sababu tu Watendaji wabovu wa<strong>na</strong>weza kujifi<strong>cha</strong> katika kinga ya usiri.Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikitoa ahadi mwaka hadi mwaka kuhusum<strong>cha</strong>kato wa utungaji wa Sheria hii muhimu lakini hadi leo hatujao<strong>na</strong> Muswada wa Sheria hiyoukia<strong>cha</strong> ule ambao wadau wamependekeza. Kambi Rasmi ya Upinzani tu<strong>na</strong>itaka Serikali kuuletaBungeni Muswada wa Sheria hiyo ndani ya mwaka huu, ili tuujadili <strong>na</strong> kupitisha Sheria hiyo bila yakukawia zaidi.Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi Rasmi ya Upinzani tu<strong>na</strong>itahadharisha Serikali kuwa isijaribuku<strong>cha</strong>kachua hata kidogo maoni hayo ya wadau kwa sababu tumejiridhisha kuwa ya<strong>na</strong> msingi<strong>na</strong> dhamira ya dhati ya kuboresha tasnia nzima ya habari <strong>na</strong> uhuru wake. Tu<strong>na</strong>chukua fursa hiikuwataarifu mapema wadau wote wa habari kwamba tutakuwa pamoja <strong>na</strong>o wakati wote waharakati za kushinikiza Muswada huo uletwe Bungeni ndani ya mwaka huu. Tu<strong>na</strong>taka Sheria hiyoipatikane mapema iwezekavyo ikiwa imebeba maoni yote ya wadau.44
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja <strong>na</strong> umuhimu wa kupata Sheria Mpya ya Vyombo vyaHabari, ni muhimu pia kuwapo kwa Sheria i<strong>na</strong>yokidhi mahitaji <strong>na</strong> i<strong>na</strong>yokubalika kwa jamii yote yawa<strong>na</strong>nchi. Sheria ya Habari katu si mali ya Waandishi wa Habari <strong>na</strong> wamiliki wa vyombo vyahabari pekee yao. Ni Sheria ya Watanzania wote. Hii ni kwa sababu, haki ya kupata <strong>na</strong> kutoahabari, ni haki ya asili.Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa<strong>na</strong>nchi wa<strong>na</strong>subiri Sheria mpya ya Habari, Kambi yaUpinzani i<strong>na</strong>itaka Serikali kuleta Bungeni Muswada wa kufuta Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976kwa kuwa Sheria hiyo ni kinyume <strong>na</strong> Katiba.Mheshimiwa Mwenyekiti, Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari. Katika Sera ya Habari<strong>na</strong> Utangazaji iliyotolewa <strong>na</strong> Serikali <strong>na</strong> kupitishwa <strong>na</strong> Bunge lako Tukufu mwaka 2003, kipengele<strong>cha</strong> 2.2.2 ki<strong>na</strong>elekeza kwamba; “Sheria mbovu za habari ambazo zimekuwa zikikosolewa <strong>na</strong>kulalamikiwa kwa kuwa haziendani <strong>na</strong> misingi ya kidemokrasia zitadurusiwa, kurekebishwa aukufutwa.” Hivyo basi, Serikali iliahidi kuwa itatunga Sheria mpya zi<strong>na</strong>zoenda<strong>na</strong> <strong>na</strong> wakati <strong>na</strong> kukidhimahitaji ya kidemokrasia ya wa<strong>na</strong>nchi.Mheshimiwa Mwenyekiti, tu<strong>na</strong>sisitiza kuwa mapendekezo ya wadau ya<strong>na</strong>kidhi kwakiwango kikubwa ahadi hiyo ya Serikali <strong>na</strong> wadau walizipitia Sheria 27 zi<strong>na</strong>zogusa habari <strong>na</strong>kupendekeza Sheria 17 miongoni mwa hizo ama zidurusiwe, zirekebishwe au kufutwa. Kambi Rasmiya Upinzani i<strong>na</strong>itaka Serikali isiendelee kusuasua katika jambo hili <strong>na</strong> ilete Muswada Bungeni waSheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ndani ya mwaka huu wa fedha.Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa Shirika li<strong>na</strong>lo<strong>cha</strong>pisha Magazeti ya Serikali (Daily News<strong>na</strong> Habari Leo) hali<strong>na</strong> Mtendaji Mkuu, toka alipoondolewa Mtendaji aliyekuwepo. Tangazo lakumtafuta Mtendaji mpya mwenye sifa <strong>na</strong> hadhi ya kuongoza liliondolewa katika mazingiratatanishi. Hivi sasa Shirika hilo limeyumba kiuongozi jambo ambalo limesababisha kushuka kwauzalishaji. Kambi ya Upinzani i<strong>na</strong>itaka Serikali kuanzisha m<strong>cha</strong>kato wa kumpata Mtendaji Mkuu waShirika hilo mwenye sifa <strong>na</strong> hadhi, kabla ya mwaka huu haujamalizika.Mheshimiwa Mwenyekiti, maendeleo ya vija<strong>na</strong>. Benki ya Taifa ya Vija<strong>na</strong> ianzishwe.Sehemu kubwa ya watu wa Taifa hili ni vija<strong>na</strong>, tukiendeleza vija<strong>na</strong> basi tutakuwa tumeendelezasehemu kubwa ya Taifa. Ni muhimu kama Taifa tuweke vipaumbele vya makusudi vya kibajeti vyakuhakikisha vija<strong>na</strong> wa<strong>na</strong>pewa kipaumbele <strong>cha</strong> kutosha <strong>na</strong> kujengewa mazingira mazuri yakujikomboa.Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuanza kujenga mazingira mazuri ya kuchochea ajira nyingikwa vija<strong>na</strong> kupitia shughuli za ujasiriamali <strong>na</strong> shughuli nyingine za kiuchumi, Kambi Rasmi yaUpinzani, i<strong>na</strong>itaka Serikali ianzishe Benki ya Taifa ya Vija<strong>na</strong>. Tu<strong>na</strong>pendekeza kuwa m<strong>cha</strong>kato wakuanzishwa kwa benki hiyo uanze ndani ya mwaka wa fedha wa 20<strong>11</strong>/2012 <strong>na</strong> benki hiyo iwe <strong>na</strong>masharti <strong>na</strong>fuu kwa manufaa ya vija<strong>na</strong>.Mheshimiwa Mwenyekiti, m<strong>cha</strong>kato wa Baraza la Vija<strong>na</strong> la Taifa. Kwa mara ya kwanzaSerikali iliahidi kuanzisha Baraza la Taifa la Vija<strong>na</strong> kupitia Sera ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka1996 <strong>na</strong> tangu wakati huo kila mwaka Serikali imekuwa ikiahidi hivyo hivyo lakini hadi leo haku<strong>na</strong>kilichofanyika.Mheshimiwa Mwenyekiti, Kambi Rasmi ya Upinzani haiko tayari te<strong>na</strong> kuo<strong>na</strong> Serikali hiiikiwapotezea muda vija<strong>na</strong> wa nchi hii. Tu<strong>na</strong>mtaka Waziri atoe kauli ya moja kwa moja yakuhakikisha kuwa m<strong>cha</strong>kato wa kuanzishwa kwa Baraza la Taifa la Vija<strong>na</strong> u<strong>na</strong>anza mara moja <strong>na</strong>Baraza li<strong>na</strong>patika<strong>na</strong> ndani ya mwaka huu wa fedha.Mheshimiwa Mwenyekiti, haja ya mabadiliko Idara ya Maendeleo ya Vija<strong>na</strong>. Kambi Rasmiya Upinzani i<strong>na</strong>amini kuwa hali mbaya ya maendeleo ya vija<strong>na</strong> nchini, pia i<strong>na</strong><strong>cha</strong>ngiwa <strong>na</strong>uongozi dhaifu usiokuwa <strong>na</strong> ubunifu wa kutosha wa Idara ya Maendeleo ya Vija<strong>na</strong>, ambao kwatakribani miaka 10 umekuwa <strong>na</strong> watu walewale kwenye nyadhifa takribani zote ikiwemo ile ya45
- Page 7 and 8: Mheshimiwa Naibu Spika, lakini umeg
- Page 11 and 12: NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiw
- Page 13 and 14: NAIBU WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA
- Page 15 and 16: Pili, Wakurugenzi na Wakurugenzi wa
- Page 17 and 18: MHE. JOHN J. MNYIKA: Naomba unisiki
- Page 19 and 20: inaongozwa na Mbunge wa Jimbo la Pe
- Page 21 and 22: Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuha
- Page 23 and 24: Mheshimiwa Naibu Spika, Baraza la H
- Page 25 and 26: katika kukuza na kuimarisha Demokra
- Page 27 and 28: wakiwa ni Baraza Kuu la Michezo Bar
- Page 29 and 30: · Kusimamia usambazaji wa machapis
- Page 31 and 32: · Kutoa taarifa katika magazeti ku
- Page 33 and 34: · Kufanya tathmini na ufuatiliaji
- Page 35 and 36: 2011 wakati wa vikao vya Kamati vil
- Page 37 and 38: na Mfuko wa Vyombo vya Habari na Ba
- Page 39 and 40: · Serikali itenge fedha za mafunzo
- Page 41 and 42: Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, nape
- Page 43: kuzifanya za kuielimisha jamii juu
- Page 47 and 48: wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UD
- Page 49 and 50: (iii)(iv)(v)(vi)(vii)Chuo Kikuu cha
- Page 51 and 52: kuendelea kufanya vibaya na kuambul
- Page 53 and 54: Serikali, sasa sisi tayari Umoja wa
- Page 55 and 56: iangaliwe. Tena nashukuru hii Wizar
- Page 57 and 58: kunichagua kuwa Mbunge wao kwa mara
- Page 59 and 60: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpira wa mig
- Page 61 and 62: na Academy yake, huyu ndiye mtu wa
- Page 63 and 64: matangazo ya kudhalilisha nchi yetu
- Page 65 and 66: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingin
- Page 67 and 68: Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi ni
- Page 69 and 70: namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa
- Page 71 and 72: Bunge. Mheshimiwa Waziri Mkuu alipo
- Page 73 and 74: pombe tu, wanaishia kunywa pombe, b
- Page 75 and 76: Nishukuru wafadhili na hasa TBC bas
- Page 77 and 78: ushuru kwenye vifaa vya michezo. Vi
- Page 79 and 80: Mheshimiwa Mwenyekiti, niende TBC,
- Page 81 and 82: Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna
- Page 83 and 84: Je, hawa watu wapo na wanafanya kaz
- Page 85 and 86: hapa Bungeni, yupo kule kwenye ofis
- Page 87 and 88: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza natak
- Page 89 and 90: tunakwenda Wizara ya Utamaduni kwa
- Page 91 and 92: MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Wale wen
- Page 93 and 94: jambo hili la kuhakikisha kwamba ku
- Page 95:
na yakizungumza habari ya interest